Kuanzia Julai 1, 2021 rasmi CHADEMA wanarejea kwenye ukorofi

Kuanzia Julai 1, 2021 rasmi CHADEMA wanarejea kwenye ukorofi

Jikite kwenye hoja kamanda
Hadi hapa usalama upo kwa wengi,ikiwa ni kwa hata fisi wakijani, achilia mbali kitoweo cha fisi, au nyumbu hakuna kutekana, hakuna kubambikiana kesi, hakunawasiojulikana na vile vile mnanuna kwa mageuzi kabambe yanayofanywa, na bado mengi yaja.
 
Tupo hapa JF kuweka kumbukumbu
Mbona chadema inakuwasha Sana? Chadema bungeni hawapo lkn bado akina ndugai na kibajaj hawalali usingizi...wenzako ambao walijaribu kuisumbua chadema wameishia kuanguka kisiasa
 
  • Thanks
Reactions: nao
Kamanda acha udikteta
Umeanzisha uzi kuihusu cdm, lengo ni uzi wako upate wachangiaji wengi maana unajua uzi kuhusu ccm hauna wachangiaji wengi kwani wengi ni wazee, na vyama vingine havina wafuasi wengi. Nenda huko kunakofanyika upuuzi uitwao uchaguzi, cdm ndio chama cha kupatia kura, maana wapiga debe wa vyama vinavyoshiriki wasipoitaja hawapati mvuto. Kwa maneno marahisi cdm imekuwa SI Unit ya kufanyia siasa nchi hii.
 
Mama anacheka na Nyani Wakati ana shamba la Mahindi. Nikikumbuka siasa za 2012-2015, naisikitikia nchi yangu, nawasikitikia zaidi boda boda kwa sababu, kwenye maandamano yoyote wao ndio hutangulizwa mbele. Anyway, kazi iendelee# This is the era of survival for the fittest.
 
Ndugu zangu,

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 Freeman Mbowe aliutangazia ulimwegu jinsi alivyohusudu utawala mpya wa Jakaya Kikwete huku akiwaponda wanasiasa wengine kama Prof. Lipumba aliyelalamikia madhaifu ya tume ya uchaguzi. Mbowe na CHADEMA walirukaruka kama ndama wakifurahia Serikali mpya ya "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania"

Wakati Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani mwaka 2015 siku 100 za mwanzo aliibuka Salum Mwalim akaitangazia Dunia kuwa Serikali ya "Hapa Kazi Tu" kwa asilimia 100 ilitekeleza sera za UKAWA.

Na sasa ndani ya siku mia moja za Rais Samia makamanda ghafla wanalazimisha kuonekana wenye furaha, wakigonga tano wakiamini Serikali ya "Kazi Iendelee" inatekeleza sera zao.

Vituko haviishi hadi kufikia tarehe 1.7.2021 tutaanza kuona na kusikia mitambo ya matusi ikiwashwa upya dhidi ya Serikali ya Rais Samia (CCM) na hapa rasmi Chongolo na Shaka nao wataanza kusakamwa na makamanda kama ilivyokuwa Dr. Bashiru na Polepole walipotekeleza majukumu ya kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola.

Muda utasema!
Big up
 
Hivi Polepole na Bashiru wameenda Kigoma? Siku zinakimbia sana.
Waende kufanya nini wakati wazandiki waliwaengua kwa mbwembwe za kusuka upya kikosi cha siasa uchwara?

Kwanini CDM hamjashiriki uchaguzi Buhigwe na Muhambwe?
 
Ndugu zangu,

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 Freeman Mbowe aliutangazia ulimwegu jinsi alivyohusudu utawala mpya wa Jakaya Kikwete huku akiwaponda wanasiasa wengine kama Prof. Lipumba aliyelalamikia madhaifu ya tume ya uchaguzi. Mbowe na CHADEMA walirukaruka kama ndama wakifurahia Serikali mpya ya "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania"

Wakati Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani mwaka 2015 siku 100 za mwanzo aliibuka Salum Mwalim akaitangazia Dunia kuwa Serikali ya "Hapa Kazi Tu" kwa asilimia 100 ilitekeleza sera za UKAWA.

Na sasa ndani ya siku mia moja za Rais Samia makamanda ghafla wanalazimisha kuonekana wenye furaha, wakigonga tano wakiamini Serikali ya "Kazi Iendelee" inatekeleza sera zao.

Vituko haviishi hadi kufikia tarehe 1.7.2021 tutaanza kuona na kusikia mitambo ya matusi ikiwashwa upya dhidi ya Serikali ya Rais Samia (CCM) na hapa rasmi Chongolo na Shaka nao wataanza kusakamwa na makamanda kama ilivyokuwa Dr. Bashiru na Polepole walipotekeleza majukumu ya kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola.

Muda utasema!

Ungemalizia kwa kusema "asema nabii Tito" ungeeleweka vizuri zaidi.

Ila wewe kama si nabii huyo si mbaya ukiyajua haya bayana:

Hadi sasa mama kama binadamu anakwenda vizuri. Akiendelea hivyo ataendelea kuungwa mkono zaidi na zaidi.

Tusitegemee mama kuzinguliwa na waungwana unaowalenga kama ataendelea kusimamia haki, uhuru na zaidi sana asiposahau kutoa mrejesho na kuchukua hatua stahiki kwenye:

1. Ripoti za CAG zikiwamo za TPA na BOT Mar 2021.
2. Ripoti ya tume ya wataalamu kuhusiana na Corona.
3. Lile kundi dhwalimu lililotaka kumzimia yeye urais.

Akitufikisha kwenye hatima ya mzizi wote wa fitina yaani kupatikana kwa katiba muafaka mbona mama atastahili mitano tena baada ya 2025 ya heshima na taadhima.

Eeh mola wetu hebu ukamjalie hekima na busara rais wetu aendelee kuyaumbua manyang'au haya yasiyomtakia mema.
 
Malengo makubwa ya viongozi wa kile chama ni ruzuku tu, hawana mpango wa kuingia ikulu. Ila bahati mbaya wanachama na wapenzi wa kile chama wanahadaiwa.. hawajui walifanyalo. wanashangilia makonda akifukuzwa, Sabaya akishughulikiwa nk

Wanapenda kuona matatizo tu, ukijenga reli unatukanwa, ukijenga hospitali unatukanwa, ukijenga barabara utapondwa. Wanapenda kusikia mambo ya chuki, kufa, kufukuzwa kazi nk. Ni watu wa ajabu sana...
Kutwa wanajadili ya jirani wao hawana ofisi hata moja waliyoijenga, hawana mradi wowote wa maendeleo, pesa za ruzuku na makato ya wabunge ni mwenyekiti na mtu wa fedha ndio wanajua. Wapo kama nyumbu.. mmoja akianza wote wanafuata. Kwa mtindo huu CCM itatawala milele.

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Duh tusubiri
Malengo makubwa ya viongozi wa kile chama ni ruzuku tu, hawana mpango wa kuingia ikulu. Ila bahati mbaya wanachama na wapenzi wa kile chama wanahadaiwa.. hawajui walifanyalo. wanashangilia makonda akifukuzwa, Sabaya akishughulikiwa nk

Wanapenda kuona matatizo tu, ukijenga reli unatukanwa, ukijenga hospitali unatukanwa, ukijenga barabara utapondwa. Wanapenda kusikia mambo ya chuki, kufa, kufukuzwa kazi nk. Ni watu wa ajabu sana...
Kutwa wanajadili ya jirani wao hawana ofisi hata moja waliyoijenga, hawana mradi wowote wa maendeleo, pesa za ruzuku na makato ya wabunge ni mwenyekiti na mtu wa fedha ndio wanajua. Wapo kama nyumbu.. mmoja akianza wote wanafuata. Kwa mtindo huu CCM itatawala milele.

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Kamanda umejiunga lini Chadema?
Ungemalizia kwa kusema "asema nabii Tito" ungeeleweka vizuri zaidi.

Ila wewe kama si nabii huyo si mbaya ukiyajua haya bayana:

Hadi sasa mama kama binadamu anakwenda vizuri. Akiendelea hivyo ataendelea kuungwa mkono zaidi na zaidi.

Tusitegemee mama kuzinguliwa na waungwana unaowalenga kama ataendelea kusimamia haki, uhuru na zaidi sana asiposahau kutoa mrejesho na kuchukua hatua stahiki kwenye:

1. Ripoti za CAG zikiwamo za TPA na BOT Mar 2021.
2. Ripoti ya tume ya wataalamu kuhusiana na Corona.
3. Lile kundi dhwalimu lililotaka kumzimia yeye urais.

Akitufikisha kwenye hatima ya mzizi wote wa fitina yaani kupatikana kwa katiba muafaka mbona mama atastahili mitano tena baada ya 2025 ya heshima na taadhima.

Eeh mola wetu hebu ukamjalie hekima na busara rais wetu aendelee kuyaumbua manyang'au haya yasiyomtakia mema.
 
Back
Top Bottom