Kuanzia Julai 1, 2021 rasmi CHADEMA wanarejea kwenye ukorofi

Kuanzia Julai 1, 2021 rasmi CHADEMA wanarejea kwenye ukorofi

Ni kawaida ya nyumbu kudhani yuko salama mbele ya simba.

Acha waendelee kumshangilia rais Samia
Hivi ugomvi wa nguruwe mwitu na nyumbu ulianziaga wapi?

Mpaka leo sijajua nini chanzo cha ugomvi wenu...
 
Kwa vile Jiwe sio rais wa nchi hii, vyovyote itakavyokuwa sawa tu!
 
Waende kufanya nini wakati wazandiki waliwaengua kwa mbwembwe za kusuka upya kikosi cha siasa uchwara?

Kwanini CDM hamjashiriki uchaguzi Buhigwe na Muhambwe?

Hatushiriki maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Kamanda jikite kwenye hoja sasa,Rais Samia ni CCM

Kwa vile umeona ujikite kwenye hoja sasa ni jambo la kheri. Tatizo ni kuwa hata kwenye mambo serious mnaweka ushabiki na hata bila ya kujali athari zake.

Hii nchi tusingeweza kweli kuvuna sote yaliyo bora zaidi? Kwani watanzania wote ni mashabiki wa vyama vya siasa kama wa Namungo tu?

Nikikurejea kwenye hoja kumbuka zaidi sana ya uCCM na uChadema, kuna na watanzania wazalendo pia ambao ni wengi tu. Kiasi kuwa nani alijiunga lini wapi inakuwa na maana labda kwako tu, kama ungali na wenge la msiba kuliko wafiwa wenyewe.

Baada ya kukupa utangulizi huo mfupi, napenda sasa nikupe msingi wa hoja kama nilivyokuwa nimekupa pale awali:

"Kwa utabiri wako ungemalizia kwa kusema 'asema nabii Tito' ungeeleweka vizuri zaidi.

Ila wewe kama si nabii huyo si mbaya ukiyajua haya bayana:

Hadi sasa mama kama binadamu anakwenda vizuri. Akiendelea hivyo ataendelea kuungwa mkono zaidi na zaidi.

Tusitegemee mama kuzinguliwa na waungwana unaowalenga kama ataendelea kusimamia haki, uhuru na zaidi sana asiposahau kutoa mrejesho na kuchukua hatua stahiki kwenye:

1. Ripoti za CAG zikiwamo za TPA na BOT za Mar 2021.
2. Ripoti ya tume ya wataalamu kuhusiana na Corona.
3. Lile kundi dhwalimu lililotaka kumzimia yeye urais.

Akitufikisha kwenye hatima ya mzizi wote wa fitina, yaani kupatikana kwa katiba muafaka mbona mama atastahili mitano tena baada ya 2025 iliyo ya heshima na taadhima kubwa?

Eeh mola wetu hebu ukamjalie hekima na busara rais wetu aendelee kuyaumbua manyang'au haya yasiyomtakia yeye na nchi hii taratibu mema."

Ni hayo tu mkuu. Karibu.
 
Ungemalizia kwa kusema "asema nabii Tito" ungeeleweka vizuri zaidi.

Ila wewe kama si nabii huyo si mbaya ukiyajua haya bayana:

Hadi sasa mama kama binadamu anakwenda vizuri. Akiendelea hivyo ataendelea kuungwa mkono zaidi na zaidi.

Tusitegemee mama kuzinguliwa na waungwana unaowalenga kama ataendelea kusimamia haki, uhuru na zaidi sana asiposahau kutoa mrejesho na kuchukua hatua stahiki kwenye:

1. Ripoti za CAG zikiwamo za TPA na BOT Mar 2021.
2. Ripoti ya tume ya wataalamu kuhusiana na Corona.
3. Lile kundi dhwalimu lililotaka kumzimia yeye urais.

Akitufikisha kwenye hatima ya mzizi wote wa fitina yaani kupatikana kwa katiba muafaka mbona mama atastahili mitano tena baada ya 2025 ya heshima na taadhima.

Eeh mola wetu hebu ukamjalie hekima na busara rais wetu aendelee kuyaumbua manyang'au haya yasiyomtakia mema.
Anaenda vizuri sio, tazama mkuu wa TAKUKURU aliyeteuliwa na mkuu wa mkoa wa Dar wa sasa akimridhi Kunenge aliyehamishiwa Pwani

Wanaosimikwa kwa sasa ni Laissez Faire Leaders na sio Transformative & Strategic leaders opened up your eyes to see how the universe is currently orbiting (anti-clockwise or clockwise) after time lapses.
 
Ndugu zangu,

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2005 Freeman Mbowe aliutangazia ulimwegu jinsi alivyohusudu utawala mpya wa Jakaya Kikwete huku akiwaponda wanasiasa wengine kama Prof. Lipumba aliyelalamikia madhaifu ya tume ya uchaguzi. Mbowe na CHADEMA walirukaruka kama ndama wakifurahia Serikali mpya ya "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania"

Wakati Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani mwaka 2015 siku 100 za mwanzo aliibuka Salum Mwalim akaitangazia Dunia kuwa Serikali ya "Hapa Kazi Tu" kwa asilimia 100 ilitekeleza sera za UKAWA.

Na sasa ndani ya siku mia moja za Rais Samia makamanda ghafla wanalazimisha kuonekana wenye furaha, wakigonga tano wakiamini Serikali ya "Kazi Iendelee" inatekeleza sera zao.

Vituko haviishi hadi kufikia tarehe 1.7.2021 tutaanza kuona na kusikia mitambo ya matusi ikiwashwa upya dhidi ya Serikali ya Rais Samia (CCM) na hapa rasmi Chongolo na Shaka nao wataanza kusakamwa na makamanda kama ilivyokuwa Dr. Bashiru na Polepole walipotekeleza majukumu ya kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola.

Muda utasema!
Hamna siasa za hivyo hizo ni hisia za kijinga
 
Back
Top Bottom