Kuanzia Jumatatu, menu za simBanking zitaanza kutozwa

Kuanzia Jumatatu, menu za simBanking zitaanza kutozwa

leo nimeamka na hii
Ndugu Mteja, kuanzia 26 Julai 2021 kila uingiapo kwenye menyu yoyote ya Bank utatozwa Tsh100 kwenye salio lako la muda wa maongezi. Kwa taarifa zaidi piga 100

kazi iendeleeee
Kuepuka hayo tumia App ya benki husika japo lazima uwe na bando ya internet. Mfano CRDB wana App ya Simbanking na NMB wana App ya Benki mkononi.
 
Nchi HAIENDI bila ya makusanyo ya KODI/TOZO.....

Tubadilishe "mentalities" kwa KUJIFUNZA HULKA MPYA ya KULIJENGA taifa letu kwa gharama ya jasho letu......

Hizo TOZO zinakwenda katika mfuko MAALUM.....CAG atakuwa anaukagua na TAARIFA TUTAPEWA.....

#KaziIendelee
#NchiKwanza
✓Huyo CAG nae no binadamu kama wewe ataziiiba tuuu izo pesa
 
Wala Sishangai Kama Benki inatumia network / infrastructure ya kwenye Simu ili kufanya Biashara yake ambayo hata simu inafanya (Competition) yaani transaction za kwenye Simu; Kwanini isiwachaji kwa hio huduma tena tusipoangalia wanaweza kupandisha mpaka hio huduma isiwe convinient kwa mtumiaji...., Hio wanaita Tit for Tat

Haya ni matatizo ya Government meddling na kujifanya wanaweza ku-plan something as complicated as economy
 
NMB Kitambo sana huwa wanakata huku kwa airtime nakule bank pia
 
Vodacom ukiingia CRDB "*150*03#" wanakata 500.

Siku zote!
Hapana boss, Voda wanakata sh 100 kwa kila login ya hiyo crdb simbanking, tangu wameanza nadhani, angalau kwa muda wote niliokuwa natumia kabla sijaamia internet banking ambapo nako wamenitoa.
 
Hapana boss, Voda wanakata sh 100 kwa kila login ya hiyo crdb simbanking, tangu wameanza nadhani, angalau kwa muda wote niliokuwa natumia kabla sijaamia internet banking ambapo nako wamenitoa.
Ukidownload app ukawa unatumia simbanking ya app ambayo haina USSD nako pia wanakata ??? Kama wanakata tujue sisi tutatafuta njia zote kuhakikisha tunajirahishia maisha. Nimewapigia tigo hawajanipa majibu direct hao wa voda wanaolipa 500 kwa kila login aisee hapana hayo maisha nisingeweza.
 
Nchi HAIENDI bila ya makusanyo ya KODI/TOZO.....

Tubadilishe "mentalities" kwa KUJIFUNZA HULKA MPYA ya KULIJENGA taifa letu kwa gharama ya jasho letu......

Hizo TOZO zinakwenda katika mfuko MAALUM.....CAG atakuwa anaukagua na TAARIFA TUTAPEWA.....

#KaziIendelee
#NchiKwanza
Hauko siriasi mkuu, mfuko maalum? CAG? Ndio nini akikagua? Itatokea nini? Miaka 60 kodi zinalipwa na hakuna kinachotokea, ndo ije kuwa tozo za miamala? Kama kweli mnajali na mna huo uzalendo, ya nini kulibebesha taifa gharama za kijinga kwa fahari ya wasio fanya kazi?

Kipi kimewahi kuboreshwa/kuzuiwa na bungwe kisitokee kwa maslahi mapana ya nchi? Kama hakuna, nini tija ya kuwa na wabunge wengi wenye kulipwa mamilioni yasiyokatwa kodi, na viinua mgongo vya kufuru kila miaka 5 plus magari mazito mazito kila baada ya miaka 5?

Kwanini tusitumie gari za cc ndogo tu, mathalani 2000cc kwa mawizara na taasisi zote za umma kupunguza initial, operation na maintenance cost, nchi imefunguliwa kwa lami tayari, sehemu korofi tumia cruiser mkonge, ONDOA depreciation factor ya miaka 5, nenda na gari hata miaka 15, si tunanunua zero km na kulitunza? Nimeona gari la shirika flani likianza na km 9 mpaka 600,000 na bado liko barabarani.

Ondoa posho zisizo na maana serikalini zisizokatwa kodi, fanya consolidation ya mishahara, piga PAYE kama wanavyofanyiwa private sector, sio unamlipa mshahara sh 445,000 ambayo inakuwa taxed halafu unampa posho za sh 1,500,000 tax free. Mpe mshahara wa sh 1,945,000 kisha piga tax yote.

Ongeza uzalishaji, sio kunyang'anya masikini ili ukawarundikie wakina Ndugai!

Achana na ruzuku za vyama, wapambanie gharama za kujiendesha wenyewe ili watumie akili kuzalisha kisha waongee yaliyo kweli, sio tuandamane kisha wao wako London na familia zao.
 
Ukidownload app ukawa unatumia simbanking ya app ambayo haina USSD nako pia wanakata ??? Kama wanakata tujue sisi tutatafuta njia zote kuhakikisha tunajirahishia maisha. Nimewapigia tigo hawajanipa majibu direct hao wa voda wanaolipa 500 kwa kila login aisee hapana hayo maisha nisingeweza.
Kama huwezi Hamia Burundi. Simple!
 
Huyu mama ni bure kabisa.

First gentlement kwani ukikaa na mama private hauwezi kumshauri kiuwandani?
 
Ukidownload app ukawa unatumia simbanking ya app ambayo haina USSD nako pia wanakata ??? Kama wanakata tujue sisi tutatafuta njia zote kuhakikisha tunajirahishia maisha. Nimewapigia tigo hawajanipa majibu direct hao wa voda wanaolipa 500 kwa kila login aisee hapana hayo maisha nisingeweza.
Sijawahi kutumia app ya simbanking ila nadhani makato ya mtandao(sh 100) yatakuwa ni ya mtandao tu na benki watakuwa wanakata kwa kila transaction unayofanya kwa simbanking ambayo itaonekana kwenye statement yako.
 
Jiwe alikausha hazina kabisa
Hii sababu haitoshi kuwafanya kuwa narrow-minded. Mkapa alipoingia madarakani, tuliambiwa, hakukuta kitu hazina, ajabu hata soda tu aliiacha sh 250 kutoka 150, mkate 200, nauli ya daladala ilikuwa sh 50 kwa sh 150, sembe kilo sh 600, sukari kilo 600 n.k Yeye akamuachia Mkwere kitita hazina, Mkwere akatuachia bei ya soda sh 750 na mkate sh 1,500 sukari, sembe n.k sijui ngapi
 
Mmmmmmhmn sijui nini kinaendelea serikalini. Ila ni upuuzi sana huu.
Screenshot_20210724_105116.jpg
 
Back
Top Bottom