Kuanzisha biashara ni jambo gumu sana kuliko kutafuta ajira

Nawashukuru sana Ndg zangu Kwa michango yenu, wengi wameuliza nimeipataje hii 40m. Nimeipata Kwa kazi ya consultancy na bado nadai hela nyingine kama 23m kama italipwa nitakuwa na ka hela kengine jumala ntakuwa na around 50M hivi karibuni.

Baadhi ya mashauri ya wengi yanaonyesha wengine hawajawahi kufanya biashara kabisa.

Mkuu@chenchele ameanalyse vizuri but that too academic, in practice haifanyiki hata kidogo.

Tanzania mtoa rushwa anapata tender nyingi sana kuliko anayefanya biashara kitaaluma.

Kwa ufupi Ukiingia uringo wa biashara ndipo unaweza kuongea vyema.

Ukiwa na hela mkononi unashangaa kila opportunity uliyokuwa unaweza unaanza kuona haitekelezeki kabisa.

Naomba tuendelee kushauriana tafadhali mkizingatia bado Niko na 33m na week hii naweza kudraw 1M Kwa matumizi yangu binafsi itabaki 32m na Kuna 23 nadai italipwa muda wowote.

Karibuni
 
Nimejaribu kuja PM nimeshindwa ila ninachosema kwamba mimi sio tapeli wala mwizi ndio maana nimesema wazi hapa kwambs nilikuja PM.

niko na experience na inshu fulani ambayo nina hakika na nimeifanya kwa muda mrefu sana ila kwa sasa sina mtaji wowote so sijaweza kuendeleza.

Sihitaji mtaji mkubwa,mtaji ninaouhitaji ni mdogo tu kiasi kwamba haitokuwa ni risk kwa upande wako.

SIna mtaji kwa sasa,nina experience ya biashara,sijasema nina idea ya biashara noooo nimesema nina experience ya biashara.

Kila mtu anaweza kuwa na idea ya biashara kwani ni wazo tu,ila experience ndio kitu kikuu ambacho kinanifanya nijiamini kuja kukuandikia hapa hadharani.

Kumbuka : SIHITAJI KIASI KIKUBWA CHA PESA YAKO usije dhani ukija kwangu nitataka milioni 10, au milioni 5 yako au milioni 4 yako au milioni 3 yako au milioni 25 yako au milioni 30yako HAPANA.

KWa wakati huu ni hatari sana kwako kuingiza pesa kwenye IDEA ya biashara,bali kwa sasa ingiza pesa yako pale kwenye EXPERIENCE ya bishara.

Usitoe mtaji kwa mtu ambaye ana idea ya biashara,toa mtaji kwa mtu mwenye experience ya biashsra.

kama hautokuja PM naomba nikushauri kitu kifuatacho ili usitoke patupu,ni hivi kama unataka kuwekeza kwa sasa au kufanya bishara basi hakikisha kwamba lengo lako kuu ni kutafuta experience na sio fedha.

kwa sababu experience ndio itakufanya udumu kwenye game kwa muda mrefu.

Hakuna biashara mbaya ila tu watu wanaziita ni biashara mbaya kwa sababu walikimbia kuexperience changamoto za biashara hiyo.

Karibu sana INBOX tuyajenge

@political Engineer 2

 
Bro nakushauri kitu kimoja..

Kama uko Dar pesa ipo kariakoo.

Narudia Tena pesa ipo kariakoo.


Kama una mtu , ndugu au jamaa alie kariakoo anza kumtembelea pale kariakoo.

Kwa huo mtaji unaweza kuwekeza nusu ya hiyo Hela kwenye frame halafu bidhaa unapewa Bure na wadau utakuwa unarudisha Hela weekly au monthly. Yani nusu ya hiyo Hela ni Kodi tu mzigo utapewa. Ila hapo kwenye kupewa mzigo ingia kariakoo tafuta network sio Kila jambo utapata online. Maduka ya vipodozi jumla, maduka ya matajiri na rims za magari , nguo, spare za pikipiki Kwa jumla. Narudia Tena Kwa jumla. Toa tips ndogo ndogo za mawinga kariakoo wanaokutafutia wateja mikoani.


Baada ya miaka niwili utaanza kuwa unaenda wewe mwenyewe nje kufunga mizigo ila kwasasa anzia migongoni Kwa watu. Kipengele ni namna ya kuaminiwa upewe mizigo. Tafuta connection na watu.


Ushauri wangu ni huo.
 
Uje inbox nikupe bia 2 tuuu basi
 
Nina tatizo kama lako ila mimi nataka kubadilisha tu biashara. Nilifanya biashara nimapata ziaid ya milion 21.

Kwa sasa nataka kubadilisha biashara. Amini usiamini huu ni mwezi wa 7 sijajua biashara nyingine ya kufanya.

Nipo tu, mzigo ulikuwa milion 21 kwa sasa nimebakiza 16.
 
Ukimwambia mtu asiye na hizo hela anakushangaa
 
Hawawezi kuelewa hii struggle ya kutafuta biashara ya kufanya ukiwa na mzigo tayari.

Anyways, kwa sasa wewe una wazo gani la biashara?
Kwa Sasa natafuta Eneo zuri nifungue biashara ya pesa, bank na mitandao ya simu ili niwe naingiza chochote wakati nikifanya negations mbaalimbali za kuwekeza.

Uzuri kama nikipata project inayoeleweka Nina uwezo wa kupata hela nyingine from other sources sasa mpaka upate hiyo project ni mtihani
 
Uko sahihi na Ugumu zaidi ni kuifanya hiyo biashara kuanza kuleta faida
 
Kuna jamaa yuko UK huwa ananunua ile mizigo ya Old stock kwenye supermarket ya Aldi then anaziingiza Zanzibar ambapo Ana Warehouse kubwa pale.

Ukielewana nae unaweza kwenda kuchukua mzigo kwake wa Home appliances kwa bei kitonga then ukauza Bongo. Hii inatoa mega profit maanankila item unapata faida double.

Yeye kwa mfano Air fryer anakuuzia 60 hadi 50 .. wewe Dar unauza 120k na ni brand new kwenye Box lake.

Therefore kama unanunua mzigo wa kutosha na unafungua Warehouse yako Dar. Ni mapema tu unadouble mtaji wako.

Hii ndio nilifanya nikapata my ule mzigo. Ila changamoto inakujwa kwa sasa kupata mzigo pale ni ishu. Maana unakuta container limefika na kuna Tycoon mmoja analipia lote Cash almost milion 70. Kwa hiyo kama una mtaji wa milion 21 unabakia kuwa mpenzi mtazamaji tu.

Ila kama una mtaji pale unapiga pesa vizuri tu.

Ukiwa tayari njoo mimi nitakuguide na kukuongoza na nitakukutanisha na Bosi mwenyewe mkae kama kamati mezani.
 
just start you will figure it out when you face challenges!
I wonder how you that long ukiwa uko na capital alafu hujui biashara ya kufanya?
Wakati I always meet people ambao wapo na very sensitive business idea but they don't know how they'll fund it!
Kweli hupewi vyote!!!![emoji851]
 
just start you will figure it out when you face challenges!
I wonder how you that long ukiwa uko na capital alafu hujui biashara ya kufanya?
Wakati I always meet people ambao wapo na very sensitive business idea but they don't know how they'll fund it!
Kweli hupewi vyote!!!![emoji851]
 
Mkuu ebu nisome kwenye post no 249 nimekuquote.

Kama uko interested njoo inbox tufanye inshu,nitakuwa tayari kukupa detail zangu zote kuhakikisha kwamba sikutapeli.

Ninachohitaji na mimi ni mtaji kidogo lakini baada ya wwe kupata faida.

I am serious mkuu
 
Mda mwingine ukiona biashara inasumbua unaweza ukanunua viwanja na kuanza kujenga,ili uendelee kuwaza namna ya kuanzisha biashar

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…