Kubeba majeruhi kwenye gari za wazi (Pickup) badala ya gari za wagonjwa (ambulance) kwenye tukio la kuanguka ghorofa K/Koo ni sahihi?

Ccm wanacho jua ni wizi wa kura na kusifia tuu. Kwenye mambo serious hawako
 
Mengine mbwembwe tu wafike hospital....haraka
 
Yaani mkuu umeongea ukweli kabisa..
Kuna watu humu just wanaandika tu kwa kuwa hawakuwa sehemu ya tukio..
 
Kuna maiti ziliwahi kutengenezewa majeneza ya mabanzi
 
Ungekua eneo la tukio usingeongea hayo mkuu..
Mkuu; Umenena sawia. Tuseme "Kwa kuwa hakuna binadamu aliye mkamilifu; basi kila atakachofanya binadamu nacho kitakuwa sio kamilifu".
Kila juhudi njema imefanyika hapo lakini bado anajitokeza mtu from no where anakuja kukosoa. Dah! Tuvumiliane tuu.
 
Hayo πŸ‘† πŸ‘† ndo baadhi ya madhara ya kuzaliwa mjini, Kukulia mjini, Kusoma shule za English medium, shule unapelekwa na kurudishwa kwa gari........... n.k. Hiki ndo Kizazi kisichojua kuna wakati wa shida na kuna wakati wa hali shwari- kawaida. Hawajawahi kuona mgonjwa kawekwa juu ya kitanda kafungwa kwa kamba ili asianguke akikimbizwa Hospitali iliyo umbali wa zaidi ya Km 8 na vijana barubaru huku vijijini. Mgonjwa akipona huja kutoa mbuzi kama zawadi/shukrani kwa vijana hao.
Sasa tuombe Mungu awafanyie wepesi hao waathirika wapone halafu tuone kama watalalamika kwamba mbona au kwa nini walipakiwa kwenye pick up.
Tukiendekeza hayo ipo siku utashangaa mtu anadai chopa ingetumika.
 
Hatuna Fedha za kununulia magari ya kubeba wagonjwa. Tunazo pesa za kununulia magari ya VX ya kuwabeba watawala wanasiasa tu pamoja na magari ya Polisi ya maji ya kuwasha ili kuwadhibiti waandamanaji.
Je, wewe kwani ulikuwa unatakaje????
 
Ungekua eneo la tukio usingeongea hayo mkuu..
Ambulance zilikuwa ziwepo mkuu, zenyewe zina first aid.
Labda km hamna tuambizane ukweli
Angalia chopper hio imemtoa mgonjwa Nungwi, kumpeleke hospital Lumumba Zanzibar.
Zanzibar kila jimbo lina ambulance mkuu. Na ukipiga simu tu fasta imefika
 

Attachments

  • VID-20241110-WA0027.mp4
    4.3 MB
Ambulance zilikuwa ziwepo mkuu, zenyewe zina first aid.
Labda km hamna tuambizane ukweli
Angalia chopper hio imemtoa mgonjwa Nungwi, kumpeleke hospital Lumumba Zanzibar.
Zanzibar kila jimbo lina ambulance mkuu. Na ukipiga simu tu fasta imefika
Mkuu kwa kweli hatuwezi katiza uokoaji kwa kusema tusubiri ambulance...

Lawama zote kuhusu kuwahi au kuchelewa kwa ambulance ni bora zikaanza baada ya kumaliza harakati za uokoaji
 
Lkn hatupaswi kuridhika. Sio hali ya kawaida katika karne hii.
Hapo kwa uchache kulitakiwa kuwe na ambulance walau 10. Ni hali ya dharura
Hata hospital za private wangejitolea ambulance zao kusaidia. Ndio professionalism
 
Mkuu kwa kweli hatuwezi katiza uokoaji kwa kusema tusubiri ambulance...

Lawama zote kuhusu kuwahi au kuchelewa kwa ambulance ni bora zikaanza baada ya kumaliza harakati za uokoaji
Sawa. Lkn mleta mada ana haki ya kushangaa. Sio hali ya kawaida.
Tusiridhike na hali ambazo zinaweza kuwa amended na serikali yetu. Like serious majeruhi wanapakizwa kwenye pickup km tupo vita ya pili ya dunia
 
Sawa. Lkn mleta mada ana haki ya kushangaa. Sio hali ya kawaida.
Tusiridhike na hali ambazo zinaweza kuwa amended na serikali yetu. Like serious majeruhi wanapakizwa kwenye pickup km tupo vita ya pili ya dunia
Daaah ndo hvo tena....
Hakuna option nyingine...

Nje ya mada mkuu naweza kukuulizwa swali...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…