Kuchapwa watoto kiasi hiki ni sawa?

Kuchapwa watoto kiasi hiki ni sawa?

huko madrasa wanapochapwa wanaishi kwa uoga kumwogopa mwalimu zaidi hata ya mzazi ndio maana matukio mengi tu uwa yanaripotiwa watoto kubakwa na kulawitia na waalimu wa madrasa. ni bora wawe regulated.
 
Kuna vitu viwili. Huwa navisema humu kila siku

1.) Mtu akishakuwa Muislam, hata awe professor, reasoning yake ni sawa na mtu wa darasa la pili, maana hata umwambie mtoto wa miaka 9 aolewe, atatetea kwamba ni sawa. Hata watoto wachanga kama hawa kupigwa hivi, litatetea kwamba ni sawa.

2.) Ukimpiga hivyo mtoto wangu, nakuuwa.
Try finding a husband to marry, Papa Francis has given permission, As time passes your ability to think seems to be diminishing.
 
Kukariri hiyo michoro si mchezo.

Madrasa karibia zote kuna bakora sema video hazijavuja tu.
ndio maana watoto wanamwogopa mwalimu wa madrasa kuliko chochote na baadhi ya waalimu wanatumia hiyo opportunity kuwabaka na kuwalawiti. kesi kibao tu zimeripotiwa humu.
 
Ijulikanavyo Quran kukariri bila fimbo ni ngumu labda kama pana njia mbadala but kumchapa mtoto hivyo lazima atachukia kuja madrasa
 
Mbona anawachapa kisaatarabu sana,watu tumechapa katika umri kama huo kwa kuninginizwa juu ya kama za kufulia.

Wazazi wa siku hizi,mnajifanya hamuwadhibu watoto ndio mnakuja kujenga watoto mashoga na makahaba.

Mtoto wa kiafrika ni fimbo tu,lasivyo tujiandae kizazi cha badaye kiwe kama cha wazungu.
Na mimi nashangaa nilidhani ametembeza fimbo mwili mzima +ngumi nk.
Yani amemchapa kikawaida kabisa sema wazazi wa kisasa wanalia lia ndio maana maadili kwisha.
 
Mbona anawachapa kisaatarabu sana,watu tumechapa katika umri kama huo kwa kuninginizwa juu ya kama za kufulia.

Wazazi wa siku hizi,mnajifanya hamuwadhibu watoto ndio mnakuja kujenga watoto mashoga na makahaba.

Mtoto wa kiafrika ni fimbo tu,lasivyo tujiandae kizazi cha badaye kiwe kama cha wazungu.
Hakuna kitu kama hicho, ingekuwa wote tumefanyiwa hivyo nadhani
Mbona anawachapa kisaatarabu sana,watu tumechapa katika umri kama huo kwa kuninginizwa juu ya kama za kufulia.

Wazazi wa siku hizi,mnajifanya hamuwadhibu watoto ndio mnakuja kujenga watoto mashoga na makahaba.

Mtoto wa kiafrika ni fimbo tu,lasivyo tujiandae kizazi cha badaye kiwe kama cha wazungu.
Kumbe ndiyo maana kuna mambo magumu Sana kwenye kuelezea tu jamii ielewe twende mbele kwa kuwa wengi tunaamini kwenye kusukuma kwa nguvu, kwa kuwa ndiyo mifumo tumekulia, sasa umri wa utu uzima mtu anaamini kwenye kusukuma, nani atamsukuma tena na ana misuli yake? Kumbe saikolojia hii ndiyo inafanya mambo yawe magumu magumu tu mahala pengi, tumeathirika utotoni wengi wetu. Hatuwezi kuendelea hivi
 
Na mimi nashangaa nilidhani ametembeza fimbo mwili mzima +ngumi nk.
Yani amemchapa kikawaida kabisa sema wazazi wa kisasa wanalia lia ndio maana maadili kwisha.
Hayo maadili mbona pia yanavuniwa na watu wazima wa kale kabisa. Kwani umefanya uchambuzi wa wavunja maadili ukaona huko hawako watu wa kale? Mbona kibao
 
huko madrasa wanapochapwa wanaishi kwa uoga kumwogopa mwalimu zaidi hata ya mzazi ndio maana matukio mengi tu uwa yanaripotiwa watoto kubakwa na kulawitia na waalimu wa madrasa. ni bora wawe regulated.
Na ndiyo maana watoto wengi hawasemi ukatili wanaopitia maana anaona akisema ni kupigwa, ninayo kesi hivi Leo ya Tanga mtoto kapigwa kaumizwa na baba mdogo baada ya kwenda kusema ukweli mahakamani. Hizi gharama za uongo na uoga na hofu ya kupigwa
 
Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anaona ni sawa mtoto kuadhibiwa kiasi hicho.

Anaesapoti mwanae achapwe kiasi hicho anyoshe mkono juu!
mashuleni kuna adhabu za bakora zaidi ya hizo na sioni watu wakipost kabisa.

Hata kitabu cha biblia kinasema kuwa upumbavu umefichwa katika moyo wa mtoto hivyo fimbo ndio hutumika kuuondoa. Ikaenda mbele ikasema kuwa mzazi asiyemchapa fimbo mwanawe ,hampendi.

“Usimnyime mtoto wako mapigo; maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na kuzimu” (Methali 23:13-14)
Mithali 22:15
"Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto,

bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye."

methali 20:30
"Mapigo na majeraha huusafisha ubaya,

nayo michapo hutakasa utu wa ndani"

methali 13:24
"Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema."
 
Daaa imeniuma ..
Mwanangu mm si mcharazi kwa hasira namna hii ,lkn kuna mkubwa mwenzangu anapiga haswa kama sio mzazi.

Huyu ni mmoja kati ya mia moja na zaidi wanaotenda kwa ukatili namna.
 
hii mitandao ya kijamii sikuizi jau sana, nikikumbuka zamani tulivokua tunaadabishwa kwa viboko nyumbani na shuleni na nikilingnisha na iyo video naishiwa nguvu

yan uto tuboko ndo twakupost mtandaoni kweli? sipati picha maadili ya kizazi kijacho cha kina Gee na Jr yatakua vipi
 
mashuleni kuna adhabu za bakora zaidi ya hizo na sioni watu wakipost kabisa.

Hata kitabu cha biblia kinasema kuwa upumbavu umefichwa katika moyo wa mtoto hivyo fimbo ndio hutumika kuuondoa. Ikaenda mbele ikasema kuwa mzazi asiyemchapa fimbo mwanawe ,hampendi.

“Usimnyime mtoto wako mapigo; maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa. Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na kuzimu” (Methali 23:13-14)
Mithali 22:15
"Upumbavu umefungwa ndani ya moyo wa mtoto,

bali fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali naye."

methali 20:30
"Mapigo na majeraha huusafisha ubaya,

nayo michapo hutakasa utu wa ndani"

methali 13:24
"Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema."
ndugu yangu, mimi nilishadeclare interest humu kuwa ni mwanasheria na nimeshawakilisha kesi nyingi sana za mauaji, hicho kipigo cha mithali kwenye Biblia, ndio kipigo kikubwa kama kile? ndio kupiga mtoto kama unauwa nyoka, mahakamani huko kuna kesi nyingi tu za mzazi kuua mtoto, anafikiri anaadhibu, wengine wanapiga mateke, wengine ngumi, wengine anampiga mtoto kofi nzito, anadondoka, anasubiri wee kwamba ataamka, mtoto ndio amekufa hivyo. kesi nyingi sana zipo huko mahakamani wazazi kuua watoto na wanaishia masononeko maisha yao yote.

zaidi ya yote, mtoto anayepigwa kama hao kwenye madrasa anaingiziwa roho ya hofu na ukatili kana kwamba hata akifanyiwa kitendo kibaya akatishiwa kwamba asiseme akisema atashughulikiwa, hata ufanyeje ataificha hiyo siri. siri hizo za kubakwa na kulawitiwa n.k, ambazo mtakuja kuzijua akiwa mtu mzima ameshaharibika yupo upande mwingine wa shilingi.

sisi sote watoto huwa tunawaadhibu, ila unamkalisha, mnajadili na kumweleza kosa alilofanya na unamwadhibu kistaarabu sio kumkomoa ila kumrekebisha. unampa na mtoto nafasi ya kujieleza kwa nini amekosea, mara nyingi watu wanapiga watoto kwa sababu wamejipakulia mboga hasa nyama, kumbe mtoto alikuwa anaona njaa, ungemuuliza angesema mama nimekula nyama hiyo kwa sababu nilikuwa na hamu au niliona njaa, na kwa sababu umezoea kumpigapiga hata ukirudi hatakwambia "mama nimekula nyama" kwa sababu anajua utampiga, ila kama wewe ni rafiki, ukirudi tu atakwambia unajua nini maza nimeona njaa nikala nyama.

watoto hao wa shule wengine wanapitia mateso makubwa kwa wazazi wao, wengine wakirudi nyumbani wanajitafutia vyakula, wazazi wapo ulevini huko au wapo kutafuta maisha wanarudi usiku, watoto wanaosha vyombo, wanafanya kazi zote mama akifika pawe panaeleweka, wanachoka, na bado shuleni wanahcapwa viboko, nyumbani wanachapwa, madrasa wanachapwa sasa wakimbilie wapi? ndio wanabaki na mioyo ya sugu na ukatili unazaliwa. mi nilifikiri huko madrasa ndio lingekuwa kimbilio kwa watoto kwa sababu wanaenda kufundishwa mambo ya Mungu, sasa huko nako wanaumizwa wakimbilie wapi sasa? si ndio maana wanakimbilia mtaani?
 
hii mitandao ya kijamii sikuizi jau sana, nikikumbuka zamani tulivokua tunaadabishwa kwa viboko nyumbani na shuleni na nikilingnisha na iyo video nnakosa cha kusema.

yan uto tuboko ndo twakupost mtandaoni kweli? sipati picha maadili ya kizazi kijacho cha kina Gee na Jr yatakua vipi
usipende maisha ya kishamba na kibushiparty uliyokuzwa wewe na watoto wako wakuzwe hivyo. kama haujui, mtoto anayechapwa chapwa huwa anapoteza kwanza uwezo wa kujieleza, na uwezo wa kujiamini. hao ndio wamejaa hata makazini ukimwambia simama hapo mbele jieleze hawezi, na hajiamini, kwa sababu alikuzwa kwa hofu na woga mtupu. na inawezekana wewe ndio mtu wa aina hiyo. don't pass that to your kids please! baki nazo wewe peke yako.
 
Back
Top Bottom