Kuchapwa watoto kiasi hiki ni sawa?

Kuchapwa watoto kiasi hiki ni sawa?

NInyi walimu muwe wa madrasa au wa mashule ya kawaida, jueni kuwa tabia yenu ya kuchapa watoto ovyo kuna siku itawatokea puani. hao watoto kila mmoja amezaliwa kivyake na ana ustahimilivu wa kipeke yake, wengine wadhaifu unagusa tu amedondoka. kuna mtu namfahamu kabisa alikuwa mwalimu, alichapa mwanafunzi akafariki, na alikuwa anachapa kikawaida tu. alisota miaka 3 gerezani kusubiria kesi, ikaisha kwa manslaughter, na amebaki na historia ya kuua mtu maishani mwake. na amekuwa adui wa milele wa wazazi wa mtoto. ipo sheria ya viboko kwa wanafunzi, nani achape, viboko vingapi na kwa namna gani. sio kila mwalimu anatakiwa kuchapa, mkifanya vinginevyo jueni sheria ipo itawanyoosha. kuna sheria ya mtoto, kuna Penal code na masheria mengine ya elimu huko. Mungu awasaidie muelewe.
 
Nimeshindwa hata kuelezea, naomba kufahamu kama ni sawa jaman,. Kuna mtoto mdogo hapo nimemuonea huruma sana.

Lakini serikal imekataza kuchapa watoto wawapo mashule, sasa swali, hapo ni wanaruhusiwa kuchapwa namna hiyo? Hakuna adhabu nyingine kwani ya kuwafanya wasirudie kosa?

Nawasilisha.
Cc: Doroth Gwajima
Dah hii mbaya sana tuikemee kwa pamoja
 
Aise tulivyokuwa wadogo muda wa madras sisi wakristo tulijaribu kwenda siku moja kuwasindikiza wenzetu ili wakimaliza elimu yao tuendelee kucheza na mpira wetu wa matambara.
Aisee kipondo walichokuwa wanakipata pale hatukuenda tena!
Kwanza tukashangaa mbona mafundisho yetu ya komunio na kipaimara hatushushiwi kipigo vile?! Eti kisa wenzetu wamekosea kukariri alfu be te....
Maustadhi wanakosea sana. Ni kama ma stress yao wanayaleta pale au labda ni wakatili tu!
 
usipende maisha ya kishamba na kibushiparty uliyokuzwa wewe na watoto wako wakuzwe hivyo. kama haujui, mtoto anayechapwa chapwa huwa anapoteza kwanza uwezo wa kujieleza, na uwezo wa kujiamini. hao ndio wamejaa hata makazini ukimwambia simama hapo mbele jieleze hawezi, na hajiamini, kwa sababu alikuzwa kwa hofu na woga mtupu. na inawezekana wewe ndio mtu wa aina hiyo. don't pass that to your kids please! baki nazo wewe peke yako.
Mkuu, Unayaita maisha waliokulia na kulelewa wazazi wako ni ya kishamba na kibushiparty? Yan walikuwa na maisha hayo halafu wakaweza kukuzaa, kukulea hadi leo umekuwa mtu mzima mwenye akili timamu then unadiriki kuinua kalamu na kuandika kwamba eti hayo yalikuwa ni maisha ya kishamba na kibushiparty? Kweli?
Mimi nadhani kilichokuwa sahihi ni kuyaangalia maisha hayo na kuchota yale yaliyokuwa mambo mazuri, yenye kuboresha na kuheshimisha kizazi cha sasa. Hizo ni Tunu za maisha. Yale unayoona sio sawa uyaache- chukua yale mema na uyaendeleze.
Mtoto, hata mtu mzima hustahili kuadabishwa (ndio haki yake au malipizi yake). Tukumbuke adhabu sio zawadi na lengo la adhabu ni kumfanya mhusika aone, achukie na kutubia kosa lake; tena ajitahidi kwa bidii zote kutokurudia tena kosa alilotenda. Kutokutoa adhabu kwa mkosaji ni kosa kubwa sana kwani mkosaji huyo ataona ni kawaida tuu atazembea na atarudia-rudia kosa hilo na hatimaye atajenga tabia. Je, hiyo ni sawa?
Kwa mfano mtoto wako wa kike (darasa la 5) anaanza mazoea ya kukutana na wavulana wanampa vizawadi e.g. pipi au fedha faraghani na anawaruhusu wamshike-shike makalio au chuchu(kama zipo) halafu ww mzazi siku moja unabahatika kumkuta live. Ukimhoji ulikuwa unafanya nn anakujibu "sio kitu". Unarudia swali tena kwa ukali lakini bado anakujibu anakuangali macho makavu "miye sijafanya kitu"
Mara paap! Anatokea mamaake na akiwa bado yu mbali kidogo anakuambia: "mwache huyo mtoto mbona alikuwa anacheza tuu? .....
Dah! hapo ujue siku yako imeshaharibika. Utaendeleaje? Kucheka? Kununa? au kutafuta mwarobaini?
Mwisho: Inakuwaje "wazazi mashabiki" tukio la kawaida kabisa mashuleni linapigwa vid.clip na linasambazwa mitandaoni kwa maneno mazito eti ni ukatili uliopitiliza ili kuamsha hisia ndani ya Jamii na tena kuamsha hisia za chuki baina ya familia ya mtoto na mwl. aliyetoa adhabu hiyo? Hilo ni kwa lengo Ovu. Kwani kulikuwa na shida au ugumu gani kuripoti tatizo hilo kwenye uongozi wa shule ili kuwezesha kulipatia ufumbuzi at local level na under field conditions? Tunakuza jambo dogo kiasi hicho utadhani mtoto amechunwa ngozi hadi kwa Mufti, Polisi na kwa waziri Mh. Dr. D. Gwajima.
Je, mtoto aliyechapwa aliumia/alidhurika kiasi hadi akalazwa Hospitali? Hakuna watoto wengine waliochapwa siku hiyo? Je, madrasa hiyo haina uongozi au msimamizi (ukimwacha huyo mwl)? Kooote huko "wazazi mashabiki" mmeona hakufai ila ni kumlipua mwl.
 
Kuna vitu viwili. Huwa navisema humu kila siku

1.) Mtu akishakuwa Muislam, hata awe professor, reasoning yake ni sawa na mtu wa darasa la pili, maana hata umwambie mtoto wa miaka 9 aolewe, atatetea kwamba ni sawa. Hata watoto wachanga kama hawa kupigwa hivi, litatetea kwamba ni sawa.

2.) Ukimpiga hivyo mtoto wangu, nakuuwa.
Mtoto anapoteza confidence akiwa anapigwapigwa
 
Mbona anawachapa kisaatarabu sana,watu tumechapa katika umri kama huo kwa kuninginizwa juu ya kama za kufulia.

Wazazi wa siku hizi,mnajifanya hamuwadhibu watoto ndio mnakuja kujenga watoto mashoga na makahaba.

Mtoto wa kiafrika ni fimbo tu,lasivyo tujiandae kizazi cha badaye kiwe kama cha wazungu.
Zaa wako wachape wafunge juu ya mti juu ya dari chapa na sisi tuko na wewe hadi uwaumize wakose confidence wasikupende wakuchukie wampende mama yao wasikusaidie ukizeeka na sisi tutakupigia makofi, tuko na ww kwenye agenda yako mpaka mwisho wa dahari
 
Back
Top Bottom