Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kwanza maisha ni magumu, halafu wewe unaongeza ugumu kwa kufunga laini za simu.

Wapiga kura wako, wengi wapo vijijini na hawajawahi kupata namba za NIDA. Octoba wanaenda kukuchinjia baharini (au una plan B ya kushinda?)

Unaenda kuvunja mahusiano ya watu, kuzuia miamala yote ya fedha na kujenga chuki kati yako na wananchi.

Ulitakiwa kuwawajibisha viongozi wa NIDA wala si wananchi. Nyota yako inazidi kufifia. Kwanini kila unachogusa kinafeli?

Je, mbona mnakomalia namba, tutaishia kupata namba tu bila vitambulisho?

Tarehe 20 ni usiku huu, lets wait and see if mzee wa font fed atafanya yake.
Nani alikuambia Magufuli angekuwa Rais mzuri?
Kuna mabaya mengi mno yanakuja hili la line ni cha mtoto, acha watanzania wakione cha moto na hadi wote wakome kuishabikia CCM.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania tuna tatizo la kutokuwa na sera za taifa. huduma, elimu, uchumi afya na usalama zinatakiwa kuwa sera za taifa hata aje kichaa gani angebanwa na katiba na sheria lakini aya mambo ya kufata matakwa ya mtu mmoja ndio yanatughalimu kama nchi.

Unamwambia babu wa miaka 70 akajipange foleni nida kujaza form ya kusajili line seriously? mzee atoke kijijini kwenda wilayani kutafuta namba? unakuta mtu anatembea km 50 kwa baiskeli au kwa miguu nenda rudi nenda rudi bila mafanikio. huduma ni haki ya kila mtu kuwafungia watu line kwanza ni uvunjifu wa katiba.
Umenena vyema Mkuu, tatizo huyu MUHUNI kutokana na UBOVU WA KATIBA YETU ameiweka mihili yote MFUKONI.
 
Vitambulisho vya NIDA kupata ni kama vile mtu unaomba VISA ya kwenda peponi, mtu unaombwa vyeti vya kuzaliwa vya watu ambao hata hujawahi kuwaona wala kujua majina yao, mtu anakuambia eti leta cheti cha kuzaliwa bibi mzaa bibi (mtu kafa kabla ya vita ya kwanza ya dunia tena alizaliwa kijijini kwenye banda la kuku).

Yani kuanzia 2015 viongozi wana complicate sana maisha ya raia, kodi zimepanda (ukiagiza gari unalipa kodi kuliko thamani ya gari, unachangia mpaka umeme), raia wanabambikizwa kesi, raia wanafilisiwa mali zao, raia akimiliki hela bank anaitwa kuhojiwa, trafic & DPP wamekua kama TRA kukusanya mapato, starehe zimefungiwa zenye kuleta mzunguko wa fedha (muda wa kufanya starehe saa 6, muda wa kuanza jioni, kuzuia shisha n.k).
 
Hakuna mantiki ya kutekeleza hili la kufungia lines kwa haraka hivi. Kwanini asiwape deadline NIDA na kuwaongezea nguvu kazi & vitendea kazi ili wafanye kazi kwa weredi? Kwanini watu wasiruhusiwe kusajiri line kwa kutumia pasipoti au driving licence? Kuna madhara gani kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiintelijensia kusogeza deadline mpaka Sepr 2025?
 
Mimi nashangaa watu kila kitu rais magufuli,lakini pia tambua kuwa usajili huu ni muhimu sana,wewe nenda kasajili laini yako ,rais aliongeza 20 days,kulia lia huku mitandaoni won't help any more,hutaki achakusajili,but serikali haita sitisha wala kuongeza muda,full stop.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kazi yako ni kumwabudu Magufuli na kumsifia tu, huna jingine kichwani hujasoma hata msingi wa Topic na kujua maudhui yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mimi nilijiandikisha mwaka 2017. Tatizo wabongo wengi wanapenda kusukumwa awapendi kufanya kwa hiyari. wazime tu mbona simu fake walizima na maisha yanasongo bado, walizima mfumo wa Tv wa analogy wakawasha digitali kuna walioshindwa kuifuata digital lakin maisha bado yanasonga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bongo naijua mwenyewe

~kusajili laini ni bure japo hatujisajili,na ingekuwa kusajili kuna gharama basi bado tungelalamika hali ni ngumu na lawama tele kwa bashite

~Watz tumezoea kwenda kwa shurti...how come kusajili laini kungekuwa sio lazima bali ni amri,wote hao wangeshasajili

~waliojazana kwenye foleni ndio hao hao waliokuwa wanadhania hawana muda

Sent using Jamii Forums mobile app
wamejazana kwenye foleni kwa sababu hawakupata namba za NIDA uelewe logic, acha kukurupuka Kama malaya wa CCM

Sent using Jamii Forums mobile app
 
maJIWE worshiper sijui mnatumiaga nini kuwaza! utamani jamaa wa NIDA watumbuliwe kwasababu gani? kwani vitambulisho wanatangeneza woa? ikiwa serikali hawajatoa hela unategemea wao watafanya nini
Kesho ndio siku ya mwisho ya kusajili simu kwa njia ya alama za vidole kwa mujibu wa agizo lililotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Magufuli.

Nini kitafuatia?

Stay tuned!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
shida fingerprints kwa nini passport isutumike kwenye usajili wa line? Injii hii pasua kichwa.
 
ukienda airtel wanakwambia netwok ipo down njoo kesho... ukifika kesho wanakwambia ipo pending njoo kesho
aliyetoa siku 20 haja calculate haya ya njoo kesho sijui mtandao uansumbua. dah mashaka haya mpaka lini sijui
Hawa airtel ndio hovyo kabisa. Wananiambia ati line yangu niyazamani hivyo inasumbua usajili. Wanadhani ni wao tu wenye mawasiliano. Nimetupa kule line yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nashangaa watu kila kitu rais magufuli,lakini pia tambua kuwa usajili huu ni muhimu sana,wewe nenda kasajili laini yako ,rais aliongeza 20 days,kulia lia huku mitandaoni won't help any more,hutaki achakusajili,but serikali haita sitisha wala kuongeza muda,full stop.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo Rais wako alitoa wapi mamlaka ya kuongeza siku za kusajili laini za simu?

Kwahiyo watu milion sitini wawe wanaishi kwa KUDRA za magufuli?

Nenda umueleze, wananchi wanaomba HISANI ya siku ishirini zingine!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aliyekwambia bure nan?njoo mbeya mjini uone mawakala walivojiongeza,kukamilisha usajili tsh1000 na kusajili line mpya 1000,
Jana nmemsajilia
Bongo naijua mwenyewe

~kusajili laini ni bure japo hatujisajili,na ingekuwa kusajili kuna gharama basi bado tungelalamika hali ni ngumu na lawama tele kwa bashite

~Watz tumezoea kwenda kwa shurti...how come kusajili laini kungekuwa sio lazima bali ni amri,wote hao wangeshasajili

~waliojazana kwenye foleni ndio hao hao waliokuwa wanadhania hawana muda

Sent using Jamii Forums mobile app
Jirani yangu na imekubari akatoa buku kuliko tabu ya kwenda NIDA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom