Kuelekea siku 30 za kuishinikiza Serikali kuachana na mkataba wa DPW na kudai katiba Mpya, tunaomba assurance kutoka kwa mawakili

Hao wako busy na miradi chungu mzima. Kule hakuna mijadala mirefu ya kifala ni action tu kwao. Kama bandari ya dar haiko tayari kuna fursa mahali pengi. Kalieni tu uchumi mpaka akili itakapo kaa sawa
Mkuu Kila kitu kifanyike kwa utaratibu,pasipo janjajanja ya kuchezea karamu
 
Haitatokea hakuna mtu mjinga wa kuacha shughuli zake za kujitafutia riziki eti akaandamane, sahau
Nahisi awamu hii itaandikwa historia katika hili mkuu
 
Mtani mbona kama mmekumbuka shuka kukiwa tayari kumepambazuka! Miaka yote 60 mlikuwa wapi tangu Uhuru hadi Leo?
 
Askari waliuwa watu 27 Pemba waliokuwa wakiandamana.
 
At least umeonyesha kuwa hata wenzetu mlioko ktk vyombo vya usalama mnakerwa na mpo pamoja na ndiu zenu wananchi kupinga huu unyonjaji na ukandamizaji wa haki za raia, ikiwa kama hili andiko ni l kweli.

Lakini, hamuihitaji Mawakili, fanyeni kama walivyofanya wanajeshi na mapolisi wa Mistri... walipoambiwa wawatoe watu kwa Road, wakasema hawa watu ni wengi mno, yanaweza kutokea mauaji ya watu wengi sana, khy ninyi watawala wajibuni hao wananchi hoja zao ili warudi majumbani.

Maandamano yalipofika hadi IKULU na watu wakataka kuvamia ndani, na kwa umati ule kwa ha kika Jeshi lisingeweza fanya lolote, badala yake likamshauri Rais resign, ipusha hii dhoruba na maisha ya Wana wa Misri.

Mamlaka ikatii.....Mkifanya hivyo mtakuwa hamana kosa kabisa na hata utawala ujao utaendele kufanya kazi nanyi. Ila mkiona mnatumwa na Mabosi wenu kufanya vitu vya kiharamia na kuwauumiza watanzania wenzenu, gomeni..mbona ninyi ndio wengi na mnaweza kuwa na maamuzi ya busara zaidi kuliko huyo Bosi wenu mmoja.

Kila la kheri!
 
DP World anaanza kazi mapema Novemba pale TPA, unaposema uachane nae unao utayari pia wa kuachana na waendeshaji ambao barua zao za kutangaza zabuni zinaendelea kuweka hadharani kila kukicha?.

Hii ni aibu sio ya kwako pekee bali ni ya uongozi wa juu wa kanisa letu katoliki la mitume.
 
Hakuna mwananchi anaejitambua ataenda huko aache mambo yake ya msingi ili kuwapa kiki watu wasiojielewa, walioshindwa kuongeza hata familia zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…