Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

Angetajwa kwa mema usingesema kuwa acheni kumtaja mfu ila kwa kuwa anatajwa kwa maouvu yake ndio unakereka kwa sababu hatujui huenda ulikuwa mnufaika wa hayo.
Biblia inasema usimwache mwovu ashuke kaburini kwa amani.
Nahisi ndicho kinachowndelea kwa yule mtu kwa sasa kama ilivyo kwaFarao, Hitler, Musolin, Beneto, Bokasa nk.
 
Anaandika, Robert Heriel

Sikuwa mshabiki wa Magufuli Kutokana na namna alivyokuwa anaongoza, sisemi Kuwa Magufuli hakuwa na mambo Mema aliyoyafanya, yapo mengi mazuri Sana hasa ya miundombinu, lakini pia yapo Mabaya ambayo aidha aliyafanya au kuyafumbia macho, ambayo ndio yalinifanya nimuone kama kiongozi asiyefaa.

Ninashangazwa na kile kinachoendelea hasa Kwa upande wa Upinzani kuendelea kumtaja taja MTU ambaye tayari anasiku nyingi ameshafariki.

Wabaya Waliohai wapo wengi, Kwa nini mhangaike na Watu waliokwisha Kufa wasio na chochote cha kuchangia katika Ulimwengu wa Waliohai? Wema Waliohai pia wapo wengi.

Hatuwezi kuongoza nchi Kwa kuangalia Wafu, na hatutataka nchi yetu iongozwe na watu wenye mawazo na Matendo ya Wafu.

Tunahitaji viongozi ambao wanaongoza nchi Kwa kuangalia Maisha ya kizazi kijacho kitaishije,
Nchi inaongozwa Kwa mahitaji yajayo sio mahitaji yaliyopita. Nchi inaongozwa Kwa maslahi ya Watu wa kesho sio Kwa maslahi ya Watu wa Jana na juzi waliokwisha Kufa.

Wanaoishi Wasiwe watumwa wa Wafu, Watu waliokwisha Kufa. Hivyo ndivyo taifa hili linapaswa kujengwa na kuongozwa. Kwa sababu tunaenda Mbele na sio Nyuma.

Sijui Fulani alikuwa Nani akasema nini, hiyo haina maana yoyote Kwa wakati au kizazi kijacho, kitakachoangaliwa ni manufaa ya kizazi kijacho.

Hata Mungu tunayemuabudu ni MUNGU aliyehai na Mungu wa Waliohai sio Mungu wa Wafu.

Wanasiasa mnaomtaja taja Magufuli Kwa ubaya mnayohaja ya kujitafakari, kama mnaagenda zenu za Siri Sawa lakini eleweni kuwa haitasaidia Jambo LOLOTE lile.

Acha nipumzike SASA.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Makanya, Same, Kilimanjaro.
Kama hujui unakotoka hutaweza kujua unakokwenda. Adolf Hitler anatajwa na ataendelea kutajwa kila siku. Wanaomtaja ni wapuuzi? Hakika wewe ni mpuuzi wa kiwango cha juu.
 
Usipanic hapa tunajadiliana kwa hoja tu wala usifikiri kuna mtu atakulazimisha kitu, mwisho wa siku ni uamuzi wako hata ukiamua utembee uchi barabarani na kusema ni kwa sababu ya kumlaani Magufuli hiyo ni wewe ila sie tutasema umechanganyikiwa kwa sababu hoja yako ya kukufanya utembee uchi ya kipuuzi.
Hakuan kupanic mtu hapa. Muuaji atabaki kuwa muuaji na ni lazima akumbukwe kwa mauaji aliyofanya pamoja na ujinga mwingine mwingi, mpaka wa kukataa uwepo wa korona na hiyo hiyo korona ikaja kumuondoa.
 
Well, huwezi kumpangia mwenye maumivu namna ya kulalamika. Kama inakukera, then fuatilia yanayokuhusu.
Hata haya yananihusu pia kama yasingenihusu basi hayo malalamiko wangekuwa wanalalamika majumbani kwao kwa wake na waume zao na mue nisingeyasikia. Lakini anayezungumziwa hapa alikuwa kiongozi wa nchi ya Tanzania na mie ni mtanzania.

Mie nina rafiki yangu nae anakiri kuguswa na uongozi wa Magufuli ila hakutaka kuniambia aliguswa vp ila watu kama hawa ndio kutwa kumnanga Magufuli kumbe ni hasira zake binafsi na si kwamba anachukia maovu.
 
Kama hujui unakotoka hutaweza kujua unakokwenda. Adolf Hitler anatajwa na ataendelea kutajwa kila siku. Wanaomtaja ni wapuuzi? Hakika wewe ni mpuuzi wa kiwango cha juu.
Hata Nyerere anatajwa ila mbona hatajwi kwa mabaya kama alivyomchambua Lissu bungeni? Mwisho wa siku Lissu akaonekana anamkosea heshima baba wa taifa.
 
Kikubwa mwanadamu yoyote hupaswi kuwa mwovu na usijiinue sana hadi kujifananisha na malaika na kujiuona hukosei, Magufuli alipitiliza kujiona yeye ni yeye na hakuna kama yeye.
Kipi hicho cha ajabu sana alichofanya hadi useme alijiona yeye ndio yeye na hakosei? Kwamba alipitiliza.
 
Hakuan kupanic mtu hapa. Muuaji atabaki kuwa muuaji na ni lazima akumbukwe kwa mauaji aliyofanya pamoja na ujinga mwingine mwingi, mpaka wa kukataa uwepo wa korona na hiyo hiyo korona ikaja kumuondoa.
Ndio msipanic hapa ni hoja tu, kuendelea kutumia muda mwingi kujadili maovu ya Magufuli kuliko kujadili maovu yanayoendelea kutendwa na waliyo hai hilo ndio jambo ambalo mleta mada anaona halina faida kwa taifa ni suala la kihisia watu kupunguza tu hasira zao. Tungekuwa tunajadili makosa na maovu ya Nyerere hadi sasa sidhani kama tungesonga mbele.
 
Wanaomsema magufuli, na Kwa usahihi zaidi sio kumsema bali kuonyesha 'sura' yake halisi, sio upinzani. Ni watu wote ambao sio wanafiki, wanaopenda ukweli.

Sura yake halisi Watu wengi wanajua,
Nafikiri tungejikita kwenye ishu za msingi kama Katiba Mpya,
 
Kwa Nyerere, mazuri yake ni mengi kuliko mabaya..
Kwa jiwe ni kinyume chake!
Kwahiyo hapa mnaangalia idadi ya maovu au athari zake hata kama hayo maovu yalikuwa machache? Na kama wewe ndio una mtazamo huo kwa Nyerere basi pia wengine wana mtazamo tofauti na wewe kwa Magufuli na hata Nyerere.
 
Usitushangae Mkuu,

Uwezo wetu ndo umeishia hapo. Hushangai mpaka Leo tunalaumu ukoloni hata baada ya miaka 60 ya uhuru. Hatufiki mbali kwa sababu Kila muda tunaangalia nyuma kutafuta wa kumlaumu badala ya ubunifu wa kupambana kutatua changamoto zinazotukabili.

Na hili ndio tatizo la wengi wetu.
Kulaumu mambo yaliyopita ilhali yaliyopo tukiyafumbia macho
 
Wewe endelea na makala za kuelimisha vijana na mahusiano upo vizuri, huku tuache wenyewe huna upako huo.

Magufuli tutaendelea kumsema Kwa maovu aliyowatendea Watanzania tangu kuumbwa Kwa ulimwengu huu, udikteta na utawala wa mkono wa chuma tulikuwa tunausikia tu Kwa wenzetu na kusoma kwenye historia, lakini yule Mrundi wa Chato akaja kutuonesha dhahiri.

Hadithi kama hii usithubutu kwenda kuiogea kwenye familia ya Ben Saanane utakimbizwa na mashoka.

Hebu tuache, huyu tunaye liwe fundisho Kwa waovu wote kwamba ukiishi Kwa Ubaya utasemwa daima Kwa Mabaya yako na mema yako tutayasahau.

Imagine Profesa mzima Kabudi leo anatuambia eti yeye na Magufuli walitudanganya kuhusu pesa za Makinikia halafu unataka tukae kimya?
Kama hatakuelewa basi
 
Ndio msipanic hapa ni hoja tu, kuendelea kutumia muda mwingi kujadili maovu ya Magufuli kuliko kujadili maovu yanayoendelea kutendwa na waliyo hai hilo ndio jambo ambalo mleta mada anaona halina faida kwa taifa ni suala la kihisia watu kupunguza tu hasira zao. Tungekuwa tunajadili makosa na maovu ya Nyerere hadi sasa sidhani kama tungesonga mbele.
Mwalimu Nyerere alisema TUJISAHIHISHE yamkini hayo mabaya ya sasa Yana msinginwake kwa yaliyopita sio we have to identify the mistakes before we correct them.
 
Mungu ndiye anayejua Zaidi.
Kila Jambo limekadiriwa,
Samehe nawe usamehewe.
Kama unataka kuwa bingwa wa kusamehe, msamehe na Shetani! Matendo ya Jiwe yalikuwa ya Kishetani kwa Watanzania, tutaendelea kumkemea kama tunavyomkemea Shetani kila siku.
 
Kama unataka kuwa bingwa wa kusamehe, msamehe na Shetani! Matendo ya Jiwe yalikuwa ya Kishetani kwa Watanzania, tutaendelea kumkemea kama tunavyomkemea Shetani kila siku.
Duhh, lakini tuliopo ndio turekeshe tunavyoishi na tuangalie matendo yetu pia badala ya kuishia kulalamikia matendo ya Mtu mwingine huku bila ya kujifunza kupitia yeye na kuishi na kutenda vyema vile tupasavy
 
Sisi Tunachojua, kuna siku Magufulification itaingizwa kwenye Mtaala wa Elimu yetu, na hayo ndio Mafanikio na mwanzo wa Utambuzi wa Kweli kwa vitukuu vyetu kesho.
True Legend.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Ndio nimekwambia hata Nyerere huwa anatajwa sana ila sio kwa aina ile aliyomzungumzia Tundu Lissu bungeni ikazua maneno, sasa huwezi kumtenganisha mtu na matendo yake basi tungekuwa tunamzungumzia Nyerere hadi leo kwa mabaya yake kama alivyoyaelezea Lissu lakini mbona haipo hivyo?
Hujazuiawa kuyataja mabaya yake kama unaona yaliwaumiza watanzania au wewe binafsi
 
Kuna kitu kinaitwa "closure". Kwa kiswahili cha mtaani tunaweza kuita "kufunga mafaili" ya jambo au suala. Katika utawala wa Magufuli kuna mambo mengi mabaya sana yaliyofanyika ambayo hadi leo hayajapatiwa majibu au tuseme bado yako gizani. Kwa mfano, mauaji ya Akwilina, Lwajabe, miili iliyookotwa kwenye viroba, kupotea kwa Azori, Ben Saanane, risasi za Lissu, kutekwa kwa Mo, Roma, Magoti, wizi wa uchaguzi 2019, 2020. kuzima vyombo vya habari, vyama vya upinzani, ukwapuaji wa fedha za watu benki, bureau de change, n.k. Na majuzi Rais wa sasa kaongezea ufisadi kwenye pesa za "plea bargain" zisizojulikana zilipo.

Yote hayo bado yako gizani. Serikali ya CCM bado haionyeshi utashi wa kuleta CLOSURE kwenye kadhia hizi.

Lazima mkondo wa sheria ufanye kazi, ukweli ujulikane, hukumu sahihi itolewe (hata posthumously ikibidi) na hatua zichukuliwe kwa wahusika waliopo. MUHIMU ZAIDI kwa amani na utulivu wa nchi ni vyema kuwa na mchakato wa maridhiano ya kitaifa (truth and reconcilliation process). Hiyo ndiyo namna bora ya kupata CLOSURE. Maridhiano yanayoendelea ni hatua nzuri lakini haitoshi. Kinachosikitisha sana ni kwamba miaka ya karibuni serikali ya CCM imezidi kuendesha propaganda hatarishi za kuwagawa wananchi.

Kwa wale watakaodai hata awamu zilizopita zina matatizo ya aina hiyo wako sawa ingawa ni wazi kuwa Rais wa awamu ya tano aliyafikisha kwenye kiwango cha kutisha. Yaliyotokea kwa Mwangosi, Zona, Ulimboka na Kibanda awamu ya nne nayo bado "yananing'inia". Hayajapata CLOSURE. Ni doa kubwa kwa serikali ya CCM. Wahenga hawakukosea waliposema "damu ya mtu haipotei bure". Yote haya yataendelea kulitesa taifa kwa miaka mingi ijayo.

Walio na shauku kubwa kutaka Magufuli asisemwe au asitajwe basi waiombe serikali yao ya CCM ichukue hatua kuleta CLOSURE na UTANGAMANO kwa wananchi wote nchini. NA pia wajue wakianzisha mada za kumsifu Magufuli katika mazingira haya ambapo kadhia nyingi za utawla wake hajipata CLOSURE basi wasishangae kujibiwa na wenye kero zao. Waingereza wanaita kujibiwa "in kind".
Mwenye kuelewa na aelewe ufafanuzi huu mujarabu
 
Back
Top Bottom