Kuendesha boda boda ni kazi kama kazi nyingine msichukulie poa

Hiyo ni kazi ya laana tu matatizo ya kujitafutia kuvunjika miguu na mabega mlivyo wajeuri skuizi mnaendesha na mziki juuuuu yaani ukiona mtu anaisifia hii kazi hayupo sawa kwenye ubongo
Sio kweli mkuu, kazi za laana ni wizi, umalaya, ulaghai n.k ila sio bodaboda. Hawa jamaa wanatafuta mkate kwa haki kabisa sema wengi wao hawana leseni ya udereva, ni wavuta bangi, malaya na wachache hushirikiana na wezi. Ila ni kazi nzuri mtu akiwa anajitafuta akiwa makini na kumuomba Mungu
 
Kuwemi na discipline basi muwapo barabarani. Pia acheni watoto washule wasome, mnashindwa hata kuwahonga wakubwa wenzenu. Ila endeleeni kuwapa tu lift wake zetu mnajiona wajanja Sana eee. Yaan mabwana wa wake zetu mnawajua kuliko mnavyozisaka pesa🤣🤣
 
Muwe mnawapa nauli ili wasipewe lift
 
Ikifanyika kwa akili,weledi na kuheshimu sheria za barabarani ni kazi nzuri tu. Yupo bodaboda namtumia kwa delivery anaingiza hela nyingi sana kwa siku.
 
Sidhani kama bodaboda ni kazi kama zingine. Ile ni hatari zaidi, kazi kidogo
 
Hujiulizi kwanini nchi zinazojielewa hamna huo ujinga wa boda boda?
 
Wanakuwaga na tabia za kihuni mno.

Ingawa kuna waaminifu ambao ni wachache sana ila wahalifu wengi wamejificha humo kwenye hiyo kazi.

Wanapora watu na kuwaumiza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…