Kufanya kazi vijijini nilikuwa nasikiaga tu kwa jirani

Kufanya kazi vijijini nilikuwa nasikiaga tu kwa jirani

Hapana mi ni msafi sana mazingira tu sio mazuri chumba ni gofu tu ukideki Asubuhi ukirudi job SAA Tisa chini mchwa washajenga,sema nyumba zao ni za zamani sana,chumba ninacholala kina ufa juu mpaka chini nakiogopa sijui kama hakitanidondokea na mvua zinazoanza na upepo mkali acha tu rafiki angu usicoment ivi mimi naishi mazingira magumu sana mshahara laki mbili tu.

Dah Laki mbili tu nikiangalia mimi nimeingiza hio pesa kwa siku na bado natamani ingezidi zaidi ya hivyo
Mungu akufanyie wepesi,usichoke kumuomba
 
Mkuu,vumilia.Ajira zenyewe ni ngumu mnoo.Wakati naajiriwa mara ya kwanza nilipangwa kikazi wilaya fulani vijijini.Kwa ujana,sijui ni utoto,niliondoka na kuacha kazi kwa urahisi/ujinga tu.Kilichofuata baada ya mwaka mmoja tu,nilijuta.Usifanye kosa nililolifanya miaka zaidi ya 22 iliyopita.Vumilia na utafunguliwa njia yenye neema tu.
 
Kuna fursa ya hela mfano mazao au hakuna?

Kama kuna fursa ya kilimo na mazao, hayo mengine ni ya kawaida tu wewe ndio unatakiwa uyabadilishe hayo mazingira.

Chumba ulipe elfu tano halafu ushindwe kukarabati na kupulizia dawa, huku ukijipanga kujenga yako huko huko?

Mshahara unalipwa halafu ushindwe kufungua saluni ya kisasa?

Usikubali mazingira yakutawale, bali yatawale mazingira.
 
Kuna zahanati ipo simiyu..ina manesi wawili tu...kila daktari akipangiwa kule anakimbia....
Umeme upo
Network hakuna yakutafta tafta
Wananchi wanaanzia kwa waganga kwanza alafu zahanati
Maji ya bwawani
Kijijini pasikie tu kwa mwenzio..kijana ukienda uko hutoboi
Hao manesi kama ni ke na dk ni me panakalika vizuri sana.
 
Hivi na Nyie mnaamuamini huyu?
Kuna Ajira gani Ya 200k? Hata Mwl wa Cheti sidhani kama anapata chini ya 400k.
 
OK acha kazi urudi nyumbani kuna umeme.
 
Tafuta dawa ya wadudu kuna ile ya unga inasaidia sana kukimbiza wadudu, pia tafuta solar ndogo kwa ajili ya taa na back up umeme ukikatika

Mwisho wa siku pambana tu, bora wewe upo leo 2023 sisi wazee wetu walisomeshwa miaka hiyo ya 60's baada tu ya uhuru

Sasa pata picha ya vijiji vya enzi hizo, mbona sasa hivi kuna afadhali kubwa sana hivyo komaa tu
Nimependa saana ushauri wako. Kuna watu wanbwabwaja tu humu hata hawana la maana kumshauri jamaa..

Kuna jamaa alifika kijijini kuripoti, ndo kijijini kwangu na mimi nikiwa huko.

Aliponiona akaona nafanana kuongea naye. Akaniulizia shule ya sekondari ilipo. Sikuwa na noma, nikaazima boda ya mshikaji. Nikamkimbiza hadi shuleni bure.

Kwa siku chache nikiwa kijijini alikuwa karibu nami akilalamikia mazingira. Nilimshauri anunue lau eka moja apande miti, itamsaidia.

Kweli, jamaa alifanya hivyo. Siku hizi ukimwambia ahamie mjini kawa mkali kama mbogo. Ana ekari za miti kama 100 hivi na ameshaamua kustaafia huko. Kanunua kiwanja, kajenga na ana biashara yake inayolinda mshahara wake. Kifupi kaniacha kimaisha.

Siku zote ukifika mahali usianzie kugundua udhaifu wa mazingira. Anza kugundua nguvu au uwezo wake (fursa). Anza kupambana. Mengine yakukute ukiwa vitani.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Hapana mi ni msafi sana mazingira tu sio mazuri chumba ni gofu tu ukideki Asubuhi ukirudi job SAA Tisa chini mchwa washajenga,sema nyumba zao ni za zamani sana,chumba ninacholala kina ufa juu mpaka chini nakiogopa sijui kama hakitanidondokea na mvua zinazoanza na upepo mkali acha tu rafiki angu usicoment ivi mimi naishi mazingira magumu sana mshahara laki mbili tu.
Kwanini usisakafie vema, piga dari safi, dawa za mchwa zipo. Panda maua na mboga nje hadi wenyeji wakuone kweli wewe mwalimu.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Yamenikuta natamani kulia, nimepata ajira somewhere jamani chumba ni wadudu tu mda wote hata raha hamna masisimizi kibao hadi kitandani, kipindi cha mvua kinaanza chumba kinavuja, majongoo yanaingiaga ndani unaweza sema Niko nje network hakuna ni baadhi tu ya maeneo network inakamata.

Ajira ajira za vijijini ni mateso hapa ninavyoongea umeme hamna nimebakiwa na asilimia 5% umeme umekata tangu SAA 5 Asubuhi.

Nilikuwa nasikia tu ajira za vijijini sasa najionea kwa macho huduma za kijamii chache mateso!!! mateso!!! Saluni zao za kunyoa sasa ha ha ha jamani jamani mchwa wametawala chumba cha kinyozi hakuna capeti ni vumbi mlangoni limewekwa pazia tu unaweza sema uko mgahawani.
nyie si ndo mnaimba Tz ya samia inawaka waka ....kula chuma hicho.
 
Back
Top Bottom