Kufanya ngono kabla ya ndoa ni dhambi au sio dhambi?


Pale mlimani walisemwa wazinzi tu, waasherati hawahusiki 😂

Au labda inaingia kwenye “usitamani vitu vya jirani yako”?
Mwenye kujua ni dhambi ama la ni Mungu siku ya hukumu. Ila nikuhakikishie, hilo siyo kosa kamwe.
 
Soma 1Wakorintho 7:1-4

Kwa msaada wa Bwana nakuandikia;

1 Wakorintho 7:1-4
[1]Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.


[2]Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.

[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.

[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.

Ukisoma mstari wa pili, imetaja neno zinaa. Na kwa tafsiri nyepesi ya lugha ya Kiswahili,

Zinaa ni kitendo cha kushiriki mapenzi (ngono) nje ya ndoa. Yaani, iwe umeoa au kuolewa ama kushiriki na yule asiye mwanandoa mwenzako.

Katika zile amri Kuu za Mungu, amri ya Usizini ipo.
 
Hebu kwanza kasome kuhusu dhambi, yaani dhambi ni nini then turudi sasa nikufafanulie kwann kufanya mapenzi kabla ya ndoa ni dhambi ama la.
 
Umeongea vizuri sana. Utakuwa babu mzuri sana kwa wajukuu zako one day.
 
pasina urongo urongo Ngono kabla ya ndoa ni dhambi
 
Kwa waislam mtoto akisha balehe na kuvunja ungo, ni haki yake kuoa au kuolewa, ole wako mzazi umkataze kuoa, dhambi zake zote utazibeba wewe, mzazi.

Na iwapo likimpata la kumpata Kwa kumzuia kuoa au uharibifu au mabaya atakayofanya Kwa kumzuia kuoa ni juu yako mzazi na utambebea madhambi yake.

Ndo maana Kwa upande wa waislam wanaoa na kuolewa wakiwa wadogo sana.

Kwahiyo kisheria za MUNGU mtu anapo balehe anatakiwa aoe au aolewe na ndo zilikuwa tamaduni za watu wa kale,

Kwa sasahivi utandawazi na mabadiliko ya Dunia hayataki hayo lazma upitie process za kidunia kama elim kwanza ndo mengine yafuatie.
 
Daahh nilikuwa naumia sana kunyimwa utelezi alafu cku za ckukuu nakutana na vidogo vya 2009 vinanyanduana mpaka kero dada zangu huruma tafadhali nimechoka upweke hu am 27 now nimekamiliza kila kitu cjuh kuna mtu alinitupia jini
 
Je, madhara yanakuwa makubwa eneo gani, eneo ambalo vijana na mabinti wanaofunga ndoa before 20 years na kuanza familia mara moja au eneo ambalo mabinti na vijana wanakulana kienyeji hadi umri uende ndipo watafute ndoa?
 
Yes ni dhambi, Mtume Paulo alisema waasherati hawataingia mbinguni.

1 Kor 6:9-11
1 Kor 6:9-11 SUV
Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi. Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu
 
"mmesikia ya kwamba imenenwa,Msizini.

Lakini Mimi nawaambieni, Kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani,amekwishazini nae moyoni mwake".

Mathayo 5:27-28.

Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala ...


Uasherati -
Uzinzi -

Naona shida ni watu hamuelewi maana ya haya maneno

Leteni Dictionary
 
wewe lengo lako ujihalalishie ngono
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…