Kufuata Bidhaa hapo China kusikufanye ukajiona umeyapatia maisha ukadharau watu!

Hyo hua ipo sana unakuta saa sita umelipia order Labda katoni 15 Kila pisi 6500 baada lisaa mchina anaupdate 5500 Kila pisi hapo tayar ni loss kwako; mara nyingi mchina anafanya hvo akiona speed ya mzigo kununuliwa ni ndogo, anataka asafishe store, anataka kuingiza mzigo mpya ambao hauna tofauti kubwa na iliyopo
 
Aiseee kufilisika ni kugusa tu upo sahihi..
Unajua kwanini nasisitiza Mungu?
Mungu anaweza akakuepusha na hasara yoyote Ile trust me....yaani niamini Mimi atakupa hisia tu...
Unajua Kuna jamaa flani maarifu huko insta kafata bidhaa china as we speak yupo china ila jina lake sio huyo hasan WA umughaka.....
Sasa Nina supplier wangu nachukuaga mzigo mkubwa kwake....akanitext picha ya jamaa yupo kwenye factory Yao....anasema....Yuko na wateja wanakuja mpaka hapa ila wewe Bado tunakupa special price...
Embu imagne..
Naapia Kwa Mungu I have those texts as we speak na jamaa kapost zile bidhaa maana ni wale wanaofunga order ila bei aliyoweka ni kubwa mno....means kapewa bei kubwa.
Hivi unawajua wachina Wahuni sana?
Naamini yawezekana kaniambia vile kunipanga ila Kwa kiasi flani hii comment yako imenifikirisha..
Mchina wakumlia timing sana ila yote Kwa yote Mungu anatakiwa akupe 6th sense ujue namna ya kudeal nae
 
Huu Uzi umenifanya nipate hamu ya kuanzisha Uzi....nafikiri next jumapili....
Ila wafanyabiashara wenzangu mlioko huku...
Cha kwanza muamini Mungu...usiwe mtupu huna Kinga wenzako wanachinja Hadi ndugu zao....wewe huna Kinga yoyote zaidi ya Mungu.
Cha pili. Mindset....amini katika ushindi uta attract aura ya mauzo....usiisemee bidhaa kwamba sijui kama itatoka....yaani amini katika ushindi.
Mungu awatangulie....afungue popote palipofungwa.
 
Mungu ni wamuhimu sana na nakubaliana nawe kwenye hoja hiyo 100% na mifano ipo.

Wachina nawajua kwa uchache sana ila ni watu wanaozingatia maokoto sana ndio maana mambo yao usimamizi ni wao wenyewe.

wana uwezo wakuzalisha bidhaa kwa kucopy design ya awali, ukisikia kufilisika ndio kugusa ndio huku sasa, bidhaa inakaribia ubora wa ile ya awali alafu bei inapungua kidogo, kifuatacho hapo ni ITV.
Unahemea mzigo kwa gharama kubwa alafu ghafla bei inashuka, yasikieni tu kwa wengine omba yasikukute.
Au unachukua bidhaa haitoki ng'ooo hata ukiuza kwa hasara haipati wateja kutokana kuwepo na mbadala wake.
 
Yaani nikiwaga nasali naongea na Mungu kama vile yaani dah nafeel special.,
Mungu anaweza akakupambania ni kumuamini ti...
Na kua na mindset ya ushindi....
Remember Kila kitu uanzia kichwani
Dah kama upo hyo stage hongera dadangu mi nimeanguka kiimani ni vle tu naenjoy upendo wa agape
 
1000 kwenye biashara ni kubwa mno na wengine wanaoinunua kwa 5,500 wanakuja kuiuza 6,000 sasa jiulize wewe wa 6,500 hiyo hasara utaiepuka vipi?
 
Dah kama upo hyo stage hongera dadangu mi nimeanguka kiimani ni vle tu naenjoy upendo wa agape
Kwenye biashara trust me..
Watu sio weupe
Nakuchauri chagua upande usipokua na pa.
kuegemea Kuna watu watakuchezea sana..
Yaani unakua na Mungu mpaka siku mtu anafikiria kukutapeli au kukufigusi Hadi anaugua analala ndani.
Unajua Kuna watu wanakwenda lala makaburibi Kwa ajili ya frem moja ya biashara k koo au UWINGA?
trust me muamini Mungu ndo Kinga yangu ya biashara na Haina madhara wala songombingo nyingi....
 
Balaa...
 
Hii kwenye blenders za heavy duty...kutoka kuuza laki na nusu mpaka Sasa hivi inauza 60,000 tena ikiwa jagi mbili...mchina acha kabisa
 
Kuna mtu humu aliambiwa na baba yake sehemu ambapo hakuna majungu na fitna usikae hapo hamna hela #ubayaubayatu
 
Asante
Kwa hiyo ni kwamba mimi natoka mkoa nakuja Dar kuchukua mzigo wa viatu au mazagazaga ya simu ni lazima niwatafute mawinga?
Kwani hakuna maduka ya jumla yanauza? au mawinga wana mzigo uliongia kimagumashi na bei inakuwa rahisi zaidi?
Mpaji Mungu nisaidie kumjibu huyu
 
Hii kwenye blenders za heavy duty...kutoka kuuza laki na nusu mpaka Sasa hivi inauza 60,000 tena ikiwa jagi mbili...mchina acha kabisa
Timing, timing biashara inahitaji umakini na ujanja mwingi, kuna watu hawalipii mzigo kwa hela zao, hawa ni wale waliowin uaminifu kwa wateja wao kwahiyo hilo haliwasumbui ila kuna wale wanaolipia ili wauze kwa bei zao baada ya kupokea mzigo ndio changamoto. Ikitokea hali kama hiyo hapo kama mzigo ni mkubwa unaweza chizika.
 
Sio kwamba sisali ila sijafikia level unayosemea! Kuhus hayo ya kulala makaburini nayaelewa na marafiki zangu wengi wanafanya sana hayo mambo kuna sehemu tulikua tunapambania maslahi watu walisafiri Tanga, Moro goro hadi Njombe
 
Mleta mada na mungu where and where au hujasoma stori zake
 
Asante
Kwa hiyo ni kwamba mimi natoka mkoa nakuja Dar kuchukua mzigo wa viatu au mazagazaga ya simu ni lazima niwatafute mawinga?
Kwani hakuna maduka ya jumla yanauza? au mawinga wana mzigo uliongia kimagumashi na bei inakuwa rahisi zaidi?
Huko kwenye maduka ya jumla kote kumejaa mawinga. Unaemuona boss nae winga, unaemuona kama winga ni boss, hawaeleweki, kwa ufupi ukiingia k/koo kama sio mzoefu uwezi kuwakwepa mawinga mkuu, kikubwa uwe makini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…