Kufuatia kutumbuliwa kwa DC wa Sumbawanga, kuna vitu havipo sawa nchini na ni lazima visemwe

Kufuatia kutumbuliwa kwa DC wa Sumbawanga, kuna vitu havipo sawa nchini na ni lazima visemwe

blogger

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2012
Posts
12,112
Reaction score
15,060
Kwanza kabisa naanza kwa kumsalimia Rais wetu kipenzi Samia Suluhu Hassan kwa heshima zote kabisa maana najua atasoma uzi huu kwani anapita humu na tupo naye.

Ni swali la moja kwa moja tu, kama ni kweli yule DC wa Sumbawanga katolewa kwa igizo lile basi hatuna budi kujitafakari upya lakini pia kuwa watu wa kuhimili mihemko yetu.

Shida ilikuwa ni nini? Kuuvaa uhusika wa kimamlaka kuu au kuleta taharuki? Je, taharuki ilitokea? Kama ishu ilikuwa ni kuuvaa uhusika wa Mamlaka Kuu ya Nchi kwa kuigiza kama Mama (kwa kile kilemba alichovaa) mbona Marais wote nchini huchezwa kimaigizo na wengine huchorwa na sauti zao zinaigwa?

Mbona hii video hapa ilisherekewa.


Kwanini hapo ilikuwa ni sawa na ionekane DC huyu wa Sumbawanga kakosea wakati alikuwa akionesha ukakamavu na utayari wa jeshi la kina mama panapotokea shida.

Sasa maswali mengi tunajiuliza, je, ni watu tu wamejipendekeza ili waonekane au ni fitna tu na husda kwa aliyetumbuliwa?

Bado nachelea kuamini Rais ndio kamtengua huyu DC au la kashauriwa vibaya.
 
Naona alileta taharuki, na kama hapakuwepo na madhara ni jambo la kumshukuru Mungu, vinginevyo pangeweza kutokea hayo madhara halafu mambo yawe mabaya zaidi.

Binafsi naona hajaonewa, siku zote mwenye maamuzi ya mwisho ndio anaamua adhabu ya kutoa, kama ni kusamehe au vinginevyo, mkosaji kazi yako ni kusubiri adhabu tu.
 
Naona alileta taharuki, na kama hapakuwepo na madhara ni jambo la kumshukuru, vinginevyo pangeweza kutokea hayo madhara halafu mambo yawe mabaya zaidi.

Binafsi naona hajaonewa, siku zote mwenye maamuzi ya mwisho ndio anaamua adhabu ya kutoa, kama ni kusamehe au vinginevyo, mkosaji kazi yako ni kusubiri adhabu tu.
Ngoja tuone!

Tunaweza pata jibu hapa toka kwa Dola kuu yenyewe .😅
 
Kuna vitu vya kuigiza, kuna watu wa kuigiza na kuna mahali pa kuigiza. Tatizo sio kuigiza uhusika wa Rais, tatizo ni Kiongozi wa kiserikali kuigiza (kuruhusu igizo) la uhusika wa kiongozi wa nchi akiokolewa kwenye jaribio la kuuwawa kwa risasi mbele ya watu.

Kwa kifupi sana, ukishakuwa kiongozi wa kiserikali, hupaswi kabisa kuijadili au kuizungumzia mifumo rasmi binafsi ya usalama wa rais hadharani. Kufanya hivyo ni kosa kubwa sana. Ni sawa na mke/mume kuja hadharani kuzungumzia namna anavyofanya mapenzi na mkewe/mumewe kitandani.
 
Kuna vitu vya kuigiza, kuna watu wa kuigiza na kuna mahali pa kuigiza. Tatizo sio kuigiza uhusika wa Rais, tatizo ni Kiongozi wa kiserikali kuigiza (kuruhusu igizo) la uhusika wa kiongozi wa nchi akiokolewa kwenye jaribio la kuuwawa kwa risasi mbele ya watu.

Kwa kifupi sana, ukishakuwa kiongozi wa kiserikali, hupaswi kabisa kuijadili au kuizungumzia mifumo rasmi binafsi ya usalama wa rais hadharani. Kufanya hivyo ni kosa kubwa sana. Ni sawa na mke/mume kuja hadharani kuzungumzia namna anavyofanya mapenzi na mkewe kitandani.
Mwambie huyo DC Elimu yake haijamsaidia bado yupo na ujinga Mwingi kichwani aje tu mtaani ajiajiri.
 
Kuna vitu vya kuigiza, kuna watu wa kuigiza na kuna mahali pa kuigiza. Tatizo sio kuigiza uhusika wa Rais, tatizo ni Kiongozi wa kiserikali kuigiza (kuruhusu igizo) la uhusika wa kiongozi wa nchi akiokolewa kwenye jaribio la kuuwawa kwa risasi mbele ya watu.

Kwa kifupi sana, ukishakuwa kiongozi wa kiserikali, hupaswi kabisa kuijadili au kuizungumzia mifumo rasmi binafsi ya usalama wa rais hadharani. Kufanya hivyo ni kosa kubwa sana. Ni sawa na mke/mume kuja hadharani kuzungumzia namna anavyofanya mapenzi na mkewe kitandani.
Kwahiyo pale ametoa au amehatarisha nini au alitoa clue gani au alivujisha nini ktk mambo yanayohusiana na usalama wa Rais!??
 
Kwahiyo pale ametoa au amehatarisha nini au alitoa clue gani au alivujisha nini ktk mambo yanayohusiana na usalama wa Rais!??
Siku ukishaingia kwenye hiyo mifumo ya utendaji wa juu wa kiserikali nadhani utanielewa.

Wewe unaweza kuja hadharani kueleza namna unavyopigana miti na mkeo/mmeo kisa kuwafurahisha watu tu?

Kwa lugha nyepesi sana, fahamu haya;
1. Maigizo yanaweza kubeba taswira ya Ucheshi, mizaha, dhihaka au uhalisia. Kwa namna yoyote ile ambayo yule DC aliikusudia, kwa nafasi yake hakupaswa kufanya hivyo au kuruhusu hilo lifanyike kwenye eneo lake likimuhusu Rais.

2. Agizo lile lilikuwa linahusu mfumo wa kiusalama wa rais, likifanywa na maafisa usalama na likionyesha tukio la jaribio la kuuwawa kwa rais. Kiusalama halifai kufanya hadharani. Zile huwa ni Simulation (Rehersal) zinatumika kuwafunda maafisa usalama wa juu kisiri zikiwahusisha pia viongozi wa juu husika., na kamwe huwa hazisemwi au kutolewa hadharani. Ni kosa kwa afisa usalama au kiongozi kuja hadharani kuzisema au kuzifanya.
 
Siku ukishaingia kwenye hiyo mifumo ya utendaji wa juu wa kiserikali nadhani utanielewa.

Wewe unaweza kuja hadharani kueleza namna unavyopigana miti na mkeo/mmeo kisa kuwafurahisha watu tu?

Kwa lugha nyepesi sana, fahamu haya;
1. Maigizo yanaweza kubeba taswira ya Ucheshi, mizaha, dhihaka au uhalisia. Kwa namna yoyote ile ambayo yule DC aliikusudia, kwa nafasi yake hakupaswa kufanya hivyo au kuruhusu hilo lifanyike kwenye eneo lake likimuhusu Rais.

2. Agizo lile lilikuwa linahusu mfumo wa kiusalama wa rais, likifanywa na maafisa usalama na likionyesha tukio la jaribio la kuuwawa kwa rais. Kiusalama halifai kufanya hadharani. Zile huwa ni Simulation (Rehersal) zinatumika kuwafunda maafisa usalama wa juu kisiri zikiwahusisha pia viongozi wa juu husika., na kamwe huwa hazisemwi au kutolewa hadharani. Ni kosa kwa afisa usalama au kiongozi kuja hadharani kuzisema au kuzifanya.
Wewe upo kwenye System unamuelekeza Dunga embee ambae lengo lake ni kubishaa tuu... Achana naee.. Ila kama zilitumika Risasi za moto kabisaa yule DC alipaswa afukuzwee usiku ule uleee yani mapema tu.
 
Kwanza kabisa naanza kwa kumsalimia Rais wetu kipenzi Dr. Samia Suluhu Hassa. Kwa heshima zote kabisa maana najua atasoma uzi huu..kwani anapita humu na tupo naye.

Ni swali la moja kwa moja tu ...kama ni kweli yule DC wa Sumbawanga katolewa kwa Igizo lile basi hatuna budi kujitafakari upya lakini pia kuwa watu wa kuhimili mihemko yetu.!!?

Shida ilikuwa ni nini!? Kuuvaa uhusika wa kimamlaka kuu au kuleta taharuki!? Je raharuki ilitokea!?
Kama ishu ilikuwa ni kuuvaa uhusika wa Mamlaka kuu ya nchi kwa kuigiza kama Mama (kwa kile kilemba alichovaa) mbona marais wootee nchini huchezwa kinaigizo na wengine huchoorwa na sauti zao zinaigwa.

Mbona hii video hapa ilisherekewa...


Kwanini hapo ilikuwa ni sawa na ionekane DC huyu wa Sumbawanga kakosea wakati alikuwa akionesha ukakamavu na utayari wa jeshi la kina mama panapotokea shida.

Sasa maswali mengi tunajiuliza, Je ni watu tu wamejipendekeza ili waonekane au ni fitna tu na husda kwa aliyetumbuliwa.

Bado nachelea kuamini Rais ndo kamtengua huyu DC. AU LA KASHAURIWA VIBAYA ..

Nchi hii ikae itambue, sumu aliyoipanda Magufuli bado inaishi. Chuki, ubabe, dhuluma na udhalimu wa kila aina
 
Siku ukishaingia kwenye hiyo mifumo ya utendaji wa juu wa kiserikali nadhani utanielewa.

Wewe unaweza kuja hadharani kueleza namna unavyopigana miti na mkeo/mmeo kisa kuwafurahisha watu tu?

Kwa lugha nyepesi sana, fahamu haya;
1. Maigizo yanaweza kubeba taswira ya Ucheshi, mizaha, dhihaka au uhalisia. Kwa namna yoyote ile ambayo yule DC aliikusudia, kwa nafasi yake hakupaswa kufanya hivyo au kuruhusu hilo lifanyike kwenye eneo lake likimuhusu Rais.

2. Agizo lile lilikuwa linahusu mfumo wa kiusalama wa rais, likifanywa na maafisa usalama na likionyesha tukio la jaribio la kuuwawa kwa rais. Kiusalama halifai kufanya hadharani. Zile huwa ni Simulation (Rehersal) zinatumika kuwafunda maafisa usalama wa juu kisiri zikiwahusisha pia viongozi wa juu husika., na kamwe huwa hazisemwi au kutolewa hadharani. Ni kosa kwa afisa usalama au kiongozi kuja hadharani kuzisema au kuzifanya.
Mkuu kazi yeyote inayohusisha utunzi wa kifasihi.. huchukuliwa tofauti vile kila mmoja alivyoelewa..

Lile ni IGIZO tu. OVER.

Acheni siasa. Unnecessary complications.
 
Siku ukishaingia kwenye hiyo mifumo ya utendaji wa juu wa kiserikali nadhani utanielewa.

Wewe unaweza kuja hadharani kueleza namna unavyopigana miti na mkeo/mmeo kisa kuwafurahisha watu tu?

Kwa lugha nyepesi sana, fahamu haya;
1. Maigizo yanaweza kubeba taswira ya Ucheshi, mizaha, dhihaka au uhalisia. Kwa namna yoyote ile ambayo yule DC aliikusudia, kwa nafasi yake hakupaswa kufanya hivyo au kuruhusu hilo lifanyike kwenye eneo lake likimuhusu Rais.

2. Agizo lile lilikuwa linahusu mfumo wa kiusalama wa rais, likifanywa na maafisa usalama na likionyesha tukio la jaribio la kuuwawa kwa rais. Kiusalama halifai kufanya hadharani. Zile huwa ni Simulation (Rehersal) zinatumika kuwafunda maafisa usalama wa juu kisiri zikiwahusisha pia viongozi wa juu husika., na kamwe huwa hazisemwi au kutolewa hadharani. Ni kosa kwa afisa usalama au kiongozi kuja hadharani kuzisema au kuzifanya.
Safi umeeleza vizuri na hata mimi binafsi naelewa maelezo yako. Ila naomba uendelee kunielimisha sehemu moja, natoka nje kidogo, kama utakuwa na uelewa nako; wale waigizaji wa marekani wanaigiza hadi ndani ya ikulu kabisa (White house) na kuhusisha hata hotuba za marais rasmi wa marekani inakuaje? Au kwa vile tuna sera tofauti? Niliangalia series ya 24 season 7, magaidi wameingia ikulu kabisa na kumteka raisi; hii imekaaje tukiliangalia na tukio letu husika?!!!
 
Back
Top Bottom