Ndio Mafuta ni ya Mzeituni au ya Manemane Ila haya ya Manemane ni ngumu kuyapata hata ukienda madukani huyapati, Waislamu wanayaita mafuta ya Maiti sababu hupakwa Maiti baada ya kufa Ila usichokijua Mafuta ya Manemane ndio Mafuta yenye nguvu kuliko hata mafuta ya Mzeituni na Watu hawajui na hio elimu hawapewi, Yesu alipozaliwa Wale Mama Jusi ee Bwana kwa sasa utawaita Wanajimu Wazee wa kubashiri walienda kumpeleka vitu vitatu vyenye nguvu ya kifalme na nguvu ya kimuungu ambavyo ni : Dhahabu, Ubani na Manemane, sio na Mzeituni bali na Manemane, ushaelewa? na Manemane sio na Mzeituni ni -na Manemane hawakupeleka Mzeituni wale
Hivyo vitu vitatu ndio vina nguvu ya kimungu nguvu ya kifalme sasa Mafuta ya Manemane kuyapata kwake ni mtiti hata huyo Mwoposa sijui km anayo nilisikia kuhani mmoja wa kuitwa Musa wa pale Kimara Temboni alikua anawauzia Waumini wake Ila sidhani km kweli yalikua Mafuta ya Manemane yale, ukisikia mfalme Daudi alipakwa Mafuta sio ya Mzeituni ni Mafuta ya Manemane
Mwoposa hata siku hasemi Mafuta yake ni Mafuta gani yaan yanatokana Mmea gani Ila ukicheck pale mbele utaona machupa ya Mafuta ya Mzeituni yamejaa sasa Mafuta ya Mzeituni hayana nguvu kuzidi Mafuta ya Manemane na Mafuta ya Mzeituni yanauzwa Madukani yaan yametapakaa vibaya sana ni mengi Mno supamaketi zote yapo unaweza kuyanywa km unavyokunywa juice au Maji, unaweza kupikia kwenye Mboga, unaweza kuyapakaa mwilini km Mafuta ya kawaida, unaweza kuingiziwa kwenye matundu yote ya Mwili bila shida yoyote hayadhuru Mwili hata kidogo
Na Mafuta ya Mzeituni huna haja ya kuyafuata kwa Mwoposa ni vile tu watu hawana akili hawana maarifa hawana uelewa na alivyo Mwehu yule Jamaa hawapi formula hawapi maelezo hawaambii kwamba haya ni Mafuta gani na yanatokana na Mmea gani na ukienda sehemu gani na sehemu gani unayapata huna haja ya kuja kununua kwangu labda upende mwenyewe ili waendelee kuja na kujaza uwanja na yeye aendelee kuwapiga vizuri
Sababu akiwaambia haya ni mafuta ya Mmea fulani haya mafuta ni ya Mzeituni ukienda supamaketi zote utayakuta yanauzwa bei nafuu kabisa si wataacha kununua wataenda kutafuta madukani kwingine na yeye biashara inakua imekufa na kuishia hapo
Ila Mafuta ya Manemane utazinguka sana madukani kote usiyapate mpaka uagize kutoka nje
Nimekutobolea Siri uliyokua hauijui