Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Kufuzu AFCON-2019: Stars yashindwa kufunga mahesabu mapema! Yakubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Lesotho

Ntakuwa Samaki Samaki M city nikiwa sehemu ya kizazi kilichoshuhudia TANZANIA ikiend AFCON kwa mara ya pili!
 
Tuwatakie kila la kheri tu vijana wetu washinde, lakini tusimhusishe Mungu kabisa katika hili. Mungu hawezi kutubariki wakati nchi inavurugwa kwa makusudi. Nchi hii ina maana jamani na sasa kwa utawala huu wa awamu ya tano ndiyo laana inazidi kuimarika. Sisi ni watu wa ku-loose tu mpaka tupate akili.
 
Hili taifa lina upinzan wa kipuuz huenda hakuna dunia nzima.Mtu anakuambia Mungu ibariki Lesotho, sababu za mcng utasikia oooh taifa stars ikishinda jiwe atapata sifa mara CCM watasema ni mafanikio yao.

-tatizo ni akili mkuu,

-akili ndogo ni nyingi sana nchi hii

-tuwasamehe.
 
Tuwatakie kila la kheri tu vijana wetu washinde, lakini tusimhusishe Mungu kabisa katika hili. Mungu hawezi kutubariki wakati nchi inavurugwa kwa makusudi. Nchi hii ina maana jamani na sasa kwa utawala huu wa awamu ya tano ndiyo laana inazidi kuimarika. Sisi ni watu wa ku-loose tu mpaka tupate akili.
-ni kweli Mungu hawezi kutusamehe maana sasa hivi tunapinga hadi ushoga, tunamkosea sana huyo mungu wako asee.
 
Tuwatakie kila la kheri tu vijana wetu washinde, lakini tusimhusishe Mungu kabisa katika hili. Mungu hawezi kutubariki wakati nchi inavurugwa kwa makusudi. Nchi hii ina maana jamani na sasa kwa utawala huu wa awamu ya tano ndiyo laana inazidi kuimarika. Sisi ni watu wa ku-loose tu mpaka tupate akili.
ukiona unaloose mkuu jua ni wewe na family yako tu mkuu wengine sisi mwendo mdundo aka moto mchibuyu yaana hakuna kuloose wala kufeli, MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI TAIFA STARS,
IMG-20181118-WA0002.jpg
 
Wakuu,

Leo Tanzania inaweza kuingia kwenye historia muhimu sana kwenye ulimwengu wa michezo. Tunatakiwa kuishinda Lesotho kwa namna yeyote ili tuweze kushiriki michuano mikubwa kabisa barani Africa ambayo tulishiriki Zaidi ya miaka 38 iliyopita.

Watanzania wote tusimamishe kila kitu na kuonesha kila namna ya kuiunga mkono timu yetu ya Taifa. Masaa haya machache tuchafue mitandao ya kijamii na mitaani kuonesha mshikamano wetu nyakati muhimu kama hizi.

Hii mechi ya leo si ya kawaida bali ni vita ambayo tukishindwa ni taifa limeshindwa na tukishinda ni taifa limeshinda. Heshima ya ushindi wa leo itaiweka nchi kwenye ramani kubwa Zaidi kimichezo na Zaidi itabadili uelekeo wa michezo na hasa nafasi ya wachezaji wetu kupata fursa Zaidi kwenye Nyanja za kimataifa.

Kila lakheri timu ya taifa ya Tanzania, nendeni mkapiganie nchi kwa nguvu zenu zote. Wanajeshi wetu wengi wamemwaga damu zao kuipigania heshima ya taifa letu na nyie mtambue mnawajibu sawa na huo kwaajili ya Tanzania.

Taifa zima leo limeweka matumaini yote mikononi mwenu, kaipiganieni Tanzania na mlete heshima ambayo vizazi vyote vitawakumbuka kuwa nyie ndio mliorudisha heshima ya nchi baada ya miaka 38 kushindwa kushiriki michuano hii mikubwa.

"We will stand and fight here. If we can't stay here alive, then let us stay here dead." General Sir Bernard Montgomery

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Taifa Stars ….
Wakati JIWE aliishaipiga mkosi! Safari, May bê safari ya sinza Kwa Remy
 
Mkuu hayo leo hayasaidii. Tujifunze kujua tuseme nini wakati gani. Lolote litakalotokea leo huko nje itakuwa ni sura ya Tanzania wala si TFF wala nani. Pamoja na mapungufu yote lakini tukishinda ni ushindi wa Tanzania.
Ukweli hujitenga na uongo. Sitegemei jipya huko Lesotho, walikuja japa TFF wakawapeleka Chamazi tukatoka sare, Leo wako Kwao Maseru unawafungaje? Samatta naye kadi za mano hachezi. Tufungwe tubadirike.
 
Mbona mpaka sasa mshindi anafahamika, ujue unashangaza sana mkuu, mi nakupa ukweli daima,

Najua mtaniita sio mzalendo,
Sisi tut ashiriki hayo mashindano kupitia kwa diamond platnumz.
Naunga mkono hoja yako, ache Madanganyika yajitie mazalendo wakati hao viongozi wenyewe hawako tayari kubadirika.
 
Unawekeza kwa wazee waliobalehe unategemea ushindi

Tengenezeni Timu za watoto, mafanikio yatapatikana tu wewe ukiwa umezeeka

Tatizo mnataka mambo ya haraka muonekane mmefanikiwa kwenye kipindi cha uongozi wenu, Ulaya haipo hiyo

Wanajadili uchumi Wa miaka 100 ijayo hawaogopi atasifiwa nani

Bongo Kila Mtu ataka sifa haraka
na kwa sababu hii hatuta kuja kuendelea.
 
Tuliposhiriki AFCON ya mwisho mwaka 1980 wengi humu tulikuwa tunachezea maringi na kuendesha matairi kwa miti.

Enzi hizo magazeti yanauzwa pale posta mpya na posta ya zamani. Uhuru, Mzalendo, Daily News na Jumapili Sunday News. Katuni maarufu ni zile chakubanga. Mwandishi maarufu ni James Nhende wa gazeti la mfanyakazi lililokuwa likitoka jumamosi.

Hawa kina Diamond, Wema, Rooney Ronaldo, Chris Brown na Jokate walikuwa bado wanatembea viunoni mwa Baba zao.

Na kwa wale wadogo zao pengine hata wazazi wao walikuwa hawajakonyezana.

Mungu ibariki Taifa Stars, Mungu ibariki Tanzania, nchi pekee uliyotujalia.
 
Back
Top Bottom