Kuhani Musa Richard Mwacha ni nani?

Kuna vifungo vingine sizani kama unaweza kujifungua mwenyewe!

Huzuni sana maana watu wengi wanapingana na mambo wasiyoyajua. Wanajiita WaKristo na hapohapo wanapingana na neno la Yesu Kristo


Yohana 8:32
"tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru."

Hosea 4:6
'watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.'

Zaburi 105:15
Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.
 
Sijasema haiwezekani lakini kuna vifungo acha tu, vipi vingine ukiomba vitu vinaachia, na sizani kama mtu utaingia kila pahala , mimi huyo kuhani hata sijui kabisa.

Yesu akutunze Ulweso
 

Unajua maana ya neno Kuhani? Kule seminary ulifundishwa tofauti gani kati ya mitume, manabii; wainjilisti, wachungaji na waalimu? Unajua Kuhani ni nani na padre ni nani?

Mungu wetu hana mipaka. Yeye ndio huchagua nani amtume, amtunze lini na amtume wapi?

Hata Yesu alipingwa na wakuu wa dini tena makuhani wakuu. Jitafute kwenye maelekezo ya Mungu, usikariri ndugu


WAEFESO 4:11-13
"Naye alitoa wengine kuwa 1 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo"

1 WAKORINTO 3: 3:12
"kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?
Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?
Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa.
Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.
Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye.

Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe.
Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.
Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.

Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.
Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri."



MHUBIRI 9:11
"Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba
si wenye mbio washindao katika michezo,
wala si walio hodari washindao vitani,
wala si wenye hekima wapatao chakula,
wala si watu wa ufahamu wapatao mali,
wala wenye ustadi wapatao upendeleo;
lakini wakati na bahati huwapata wote."
 

Unaongea usilolijua
Yesu akusamehe
 
Hivi nyakati hizi bado kunahitajika kuwepo Kwa kuhani?

Je pazia la hekalu lilipovunjwa bado kunahitajika kuhani?

Mbona sasa tumepewa kibali cha kuingia patakatifu moja Kwa moja bila kupitia Kwa kuhani baada ya pazia la hekalu kuvunjwa na Bwana Yesu ?
 

Jitahidi kusoma neno la Mungu kwa wingi zaidi ili uweze kuelewa kwa upana zaidi. Ukisoma kidogo halafu ukakataa kile kikubwa usichokijua ni hatari sana

WAEBRANIA 5:1-4
"Maana kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi;
awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu; na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi.
Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni."

WAEFESO 4:11-13
"Naye Yesu alitoa wengine kuwa 1 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo"
 
Kama sijakosea huyu Kuhani Mussa Richard Mwacha niliwahi kumuona kwa Mzee Mkombo (muonaji) kule Boko - Magengeni.

Nikaja kumuona tena hapo Mwenge - Mpakani.

Kwasasa naona amejenga Kanisa lake hapo Kimara - Temboni (anaita Ngome ya Yesu) fresh spring fellowship!

Na naona anapandisha Ghorofa tatu juu, kafungua na Jehova - Jire TV
 
Tunajenga, Tunajenga ngome, ngome ya YESU...

Nashukuru Mungu kwa kuwa nilipata kibali cha kuona maono ya hilo jengo la madhabahu ya ngome ya YESU likiwa linajengwa na watu wakitoa pesa nyingi...

Katika Ulimwengu wa Roho lishajengwa...

Pia nimepata maono ya shule kubwa imeshajengwa ktk Ulimwengu wa Roho...

Nashukuru sana kwa kuwa mafundisho ya neno la Mungu kupitia Kuhani Musa yamenijenga...

Bwana YESU atukuzwe...
 



Hamna kitu kinajibu hoja yangu katika yote uloandika hapo.
 
Pazia la hekalu lilishapasuka baada ya zile siku 3 za Yesu Kristo.

Sasa hivi hatuhitaji kuhani tena katika kuomba toba kwa Mungu ,

Tumepewa kibali cha kwenda wenyewe kuomba toka kupitia mpatanishi wetu Yesu Kristo.
 
Pazia la hekalu lilishapasuka baada ya zile siku 3 za Yesu Kristo.

Sasa hivi hatuhitaji kuhani tena katika kuomba toba kwa Mungu ,

Tumepewa kibali cha kwenda wenyewe kuomba toka kupitia mpatanishi wetu Yesu Kristo.

Unabishana na maandiko sababu una roho ya kupingana na kazi Yesu Kristo Mungu mkuu

Baada ya zile siku 3 zipi hizo za Yesu Kristo??? Ndio pazia la hekalu lilipasuka???

Roho ya mpinga Kristo 😏🙄



Soma uelewe au Rudi ukajipange kwanza
 

Amina Amina Amina
 

Hujakosea kabisa
Kwani kuna tatizo!?
 
Kazi inaendelea

Kuhani Musa Richard Mwacha katika matukio ya kitaifa

Uzinduzi wa ikulu mpya Dodoma




Mungu ibariki Tanzania

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…