Kuingia na note book Kizimbani haikuwa ishu. Jaji Alikuwa ameishaifunika akaendelea na mambo mengine. Kibatala atabwaga tena

Mpuuzi wewe unaingiaje na simu kizimbani?
 
Hii kesi imejaa; ushetani, aibu, fedheha, ukatili wa kutisha kwa serikali hasa awamu hii.
Mungu wa Mbinguni ambae ndio hakimu wa kweli na ambae huchukizwa na uovu wa aina hii atatenda maajabu kwa kuwapiga kwa upofu waliotunga kesi hii pamoja na mashahidi wao.
 
Masikini mbowe anashindana na serikali ,iliyoshikilia mpinii ...

Kwa namna yeyote namuona mbowe akipigwa mvua ya miaka 30 jela ....

Japo sio gaidi Wala Nini ,hii nchi inaongozwa kimafia ...
 
..Jaji alitakiwa atolee uamuzi pingamizi lililowekwa na wapinzani.

..Haijalishi kama pingamizi lina uzito, au halina.

..kitendo cha Jaji kusahau, au kujaribu "kupotezea" suala hilo, kunamvunjia Jaji na mahakama heshima.
Ivi kumkataa Jaji inabidi afanye Nini. Kitendo Cha kupotezea pingamizi na kufanya maamuzi bila kuzingatia pingamizi walitakiwa wamkatae Jaji tu.
 
..Jaji alitakiwa atolee uamuzi pingamizi lililowekwa na wapinzani.

..Haijalishi kama pingamizi lina uzito, au halina.

..kitendo cha Jaji kusahau, au kujaribu "kupotezea" suala hilo, kunamvunjia Jaji na mahakama heshima.
Jaji ni wa mchongo.....ni wale waliopewa nafasi kimchongo mchongo hajiamini
 
Kwa hiyo kwenye kesi kubwa wanaacha mzigo uwalemee nini
 
Onshulile Agaba,Ninsiima,Mugisha,Hekima,Namala na Amani
 
Kibatala na jopo lake wanaelewa fika maamuzi yatakayotolewa hatua kwa hatua. Ila wanachofanya ni kuikumbusha mahakama mianya na mapungufu yanayojitokeza ili isaidea rejea kwa sie tusiofahamu sheria.
Sisi wengine tunafuatitilia ili kuelewa jinsi ya kutoa vidhibiti, jinsi ya kupinga vitu visivyoshabibiana na shauri husika na pia kuelewa mwenendo wa kesi za kiuhalifu na jinai.
Kama iwapo hii kesi ingerushwa mubashara natumai tungejifunza mengi sana na ingevutia watu wengi sana.
 
Ndugu yangu mtoto wa marehemu William Mushumbusi na Mama Ninsiima unaniangusha yani hujui kuandika hata kiswahili!!!? Una makosa mengi ya kiuandishi mpaka unakera utadhani hukupita darasa la kwanza,pili na tatu
 
Inahitaji kuwa na akili ya kijinga kama hiyo yako ili kuweza kufikia hitimisho hilo. Kwa haraka haraka unataka kutuonyesha kuwa mahakama ipo sahihi, hivyo ikitupilia mbali pingamizi lako, basi ww una uwezo mdogo. Kwa mahakama hizi hizi zinazoagizwa aina ya hukumu na jamuhuri? Nchi yetu imefikia mahali watu wenye uwezo mdogo ndio wenye maamuzi, huku watu wenye uwezo wakiishia kufanyiwa hila.
 

Kwa kinachoendelea unategemea hata wangegoma shahidi kupewa simu wangefanikiwa? Au ulitaka wanyang'anywe simu huyo shahidi wa jamuhuri?
 
..Jaji alitakiwa atolee uamuzi pingamizi lililowekwa na wapinzani.

..Haijalishi kama pingamizi lina uzito, au halina.

..kitendo cha Jaji kusahau, au kujaribu "kupotezea" suala hilo, kunamvunjia Jaji na mahakama heshima.
Utata mtupu,kwanini jaji aliruhusu mahakama ichukue notibook iwe chini ya ulinzi?
Kwanini hakujiridhisha siku ileile kama alikuwa anadokolea?

Ningekuwa Mimi shahidi ningenyosha mkono mahakamani
"Mhesh jaji Mawakili wote siwaamini mbele ya mahakama hii,Sipo tayari kuendelea kutoa ushahidi"
Nimedhalilishwa
 
Kosa la kibatala lipo wapi?. Kama Jaji anakosea au anafanya makusudi utamlaumuje Kibatala. Kibatala anachofanya ni kuweka vitu on record ili apate legal grounds za Rufaa. Maana mahakama ya Rufaa grounds za fact haziruhusiwi Bali grounds za sheria. Yeye anayachukua makosa ya Jaji kwa ajili ya matumizi ya baadae.
 
Akina Kidando hawana uwezo wowote isipokuwa jaji anawabeba.Jaji anaamua mapingamizi bila kujari vifungu vya sheria ili aifurahishe mamlaka ya uteuzi.Shahidi anaingia na diary,kalamu na simu lakini bado anashindwa kuchukua hatua.Kama hilo lingefanywa na shahidi wa utetezi angeondolewa haraka kwenye ushahidi na kupigwa mvua kadhaa.
 
..Jaji alitakiwa atolee uamuzi pingamizi lililowekwa na wapinzani.

..Haijalishi kama pingamizi lina uzito, au halina.

..kitendo cha Jaji kusahau, au kujaribu "kupotezea" suala hilo, kunamvunjia Jaji na mahakama heshima.
Hakika. Hata tusio wanasheria tunaliona wazi kabisa. Yaani kweli Jaji alisahau? Au alitaka kupotezea? Nadhani huyu Jaji ha fit kwenye hii kesi, anayumba sana.
 
Kitu kilichosababisha kuahirisha kesi na kuahidiwa kutolewa maamuzi ndio hicho hicho Jaji kasahau??[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] Tembea uonr mengi
Tanzania maajabu ya Tisa duniani
Hii kesi ni kubwa mno kwake. Kama ataimaliza sijui.
 
Mkuu kuwa navyo tu kizimbani bila idhini ya Mahakama ni kosa. Haijalisha umevitumia/unatumia ama la. Huo ni mtego mkubwa kwenye maamuzi ya Jaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…