Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Hahahaha hahahaaa. Mkuu Kuna Mambo mawili
1.Ama hupendi wengine wawe kile ambacho wewe unacho?
Ama 2. Unaishi kwa ndugu,mama,n.k
Sasa kutokana na mazingira hayo utamshawishi Nani akuelewe?
Na je utawezaje kujimwambafai mkuu!!?????
Simlazimishi mtu anielewe, huu ni msimamo wangu. Kama wewe ulivyo na msimamo wako. Naishi kwa shemeji mkuu, acheni woga.
 
Kuwa na maamuzi sahihi ni kipaji:
Watu A, B, C, D,E, F walikopa bank, kila mmoja sh. 20m kwa marejesho ya jumla ya sh. 36m kwa muda miaka 6, Kila mmoja aliamua kuwekeza fedha yake kama ifuatavyo:-
Mtu A
  • Aliamua kuwekeza fedha yote kwenye ujenzi wa nyumba, na nyumba haikumalizika iliishia kwenye kupaua.
Mtu B
  • Aliamua kuwekeza kwenye ujenzi wa nyumba ndogo,na ilimalizika na hatimaye aliweza kuhamia
Mtu C
  • Aliwekeza milioni 10 kwenye ujenzi na kumi kwenye biashara ya kuuza vilevi
Mtu D
  • Aliwekeza fedha yote kwenye ujenzi wa ofisi ya ushonaji,ofisi imekamilika ila vitendea kazi bado kukamilisha
Mtu E
  • Aliwekeza fedha yote kwenye usafiri wa kutembelea
Mtu F
  • Aliwekeza fedha yote kwenye bashara ya vifaa vya ujenzi

Swali,je baada ya miaka sita (6) hawa watu (A,B,C,D,E,F) ni yupi atakuwa na maisha ya kuridhisha?
Za kuambiwa changanya na zako
 
Hivi mnajua kula kulala huwa hajui thamani ya kitu chochote kwa mfano :- Hawajui thamaani ya kula yao,vaa yao,lala yao, aamka yao n.k kwahiyo msimlaumu saaaaanaaaa mleta mada
 
Duniani tunapita tu, sasa kwa nini nijenge njiani?🙂🙂🙂🙂, Mimi masuala ya kujenga nyumba, mfano ya milioni 70, halafu niipangishe kwa laki 3 au laki 4 nipate hizo kodi.. kwanza inategemea na niliko ijenga (hata nikiishi mwenyewe baado).. hesabu zake ni baada ya miaka 15 au 17 ndo narudisha milioni 70 yangu niliyo jengea, hapo sijaweka hela niliyo nunulia kiwanja, repair, kodi ya ardhi na kodi ya majengo ya serikali na asilimia zingine.

Sasa hela hiyo si bora nika fanyie biashara ndani ya muda huo wa kusubiri kodi izalishe faida na mafaida.. au hela nilio weka irudi mara buku.. Milioni 70 ntakayo wekeza kwenye biashara ni lazima italeta faida kubwa mara idadi itakayo jizungusha.. potelea mbali mawazo ya kupata hasara..(biashara haidanganyi ukiwa serious na una imani) kwan ukijenga likaja tetemeko au bomoa bomoa na hulipwi fidia kama wale wa kimara ile inakuaga ni faida ?
Ingekuwa rahisi hivyo si kila mtu angekuwa tajiri mtaani?
 
Po
Simlazimishi mtu anielewe, huu ni msimamo wangu. Kama wewe ulivyo na msimamo wako. Naishi kwa shemeji mkuu, acheni woga.
Pole Mkuu.NAISHI KWANGU KWENYE TEMBE LENYE SLAB YA UDONGO
 
Kanunue hisa,ingia ubia na wanaojua biashara au jenga fremu za kupangisha.
Mafremu yaliyotapakaa huko mitaani na hayazalishi ndio akili?

Hisa nazo si zina vihela vya mboga tuu hakuna pesa ya maana
 
Kuna swala pia la kutambua nyakati majira na fursa. Kwa mfano, wakati mimi naanza kupata pata pesa angalau, viwanja vilikuwa vinapatikana kuanzia mbezi makonde , mbezi jogoo kuelekea tegeta , kwa bei chini ya tzs 3,000,000.
Wakati huo mimi niliamini katka kufanya biashara na kupata pesa ambayo kwayo jambo la 'ununuzi wa kiwanja na ujenzi wa nyumba lingerahisika. Kwa bahati mbaya, kabla malengo hayajatimia biashara zikayumba na mpaka leo zina survive, na 'sijaweza 'kupata kiwanja maeneo hayo, maana sasa bei haishikiki.
Kwa hiyo maamuzi mengine ni vizuri yakafanyika katika mu da muafaka ili kuepusha majuto ya baa dae , maana mambo na /maisha kwa ujumla yanaweza kubadilika usivyotarajia..
Baishara huwa ni salama kwa mtu mwenye mtaji mkubwa na aliye diversify vyanzo vyake tofauti na hapo mtu utarudi kule kule ulikokuwa .

Ndio maana wanaojiita Wana biashara eti nzuri vimtaji vyao wengi ni 5-10 mln sasa hapo si waganga njaa tuu hao kuna pesa hata ya kwenda vacation mwisho wa mwaka?
 
hata kujenga nyumba ya kupangisha bado sio uchaguzi mzuri kibiashara.

mfano nyumba uliyojenga kwa 80mln tabata,unawezapangisha kwa 250-300 kwa mwezi.
300×12=3.6ml÷ 80mln=biashara kichaa.

wakati eicher la 80ml linaingiza 4.5ml kwa mwezi.
4.5mln×12=54 mln
ndani ya miaka 2 tayari hela imesharudi na hapa ni kama si mkataba,kama ni mkataba unaachia gari ukiwa na hela nyingi zaidi.

nyumba si uwekezaji mzuri kabisaa,labda kwa malengo ya muda mrefu.
Haiwezekani kila mtu akanunua Eicher kwa sababu kila mtu anaangalia uwezo wake wa kukabiliana na changamoto za fursa kadhaa ndio maana lazima tofauti iwepo.

Binafsi ukinambia biashara nazotaka ni hizo za real estates, Ukandarasi,financial na kuuza madawa ya binadamu/ mifugo na kilimo na mwisho kilimo/ufugaji wenyewe.
 
Baishara huwa ni salama kwa mtu mwenye mtaji mkubwa na aliye diversify vyanzo vyake tofauti na hapo mtu utarudi kule kule ulikokuwa .

Ndio maana wanaojiita Wana biashara eti nzuri vimtaji vyao wengi ni 5-10 mln sasa hapo si waganga njaa tuu hao kuna pesa hata ya kwenda vacation mwisho wa mwaka?
Na pia kwenye hyo milioni 5 mpaka 10 unajenga nyumba gan? Maana watumishi wengi hukopesheka kias hcho kutokana na mishahara duni wanayo pata.
 
Na pia kwenye hyo milioni 5 mpaka 10 unajenga nyumba gan? Maana watumishi wengi hukopesheka kias hcho kutokana na mishahara duni wanayo pata.
Unajenga taratibu ndani ya miaka kadhaa nyumba ya 30mln inaisha .

Watumishi Wana salary na Wana uhakika wa mwisho wa mwezi.
 
Watanzania wengi hawana mawazo ya kufanya biashara za maana, wengi wanaofanya biashara hasa ndogo ndogo na umachinga ni baada ya mambo mengine yote kushindikana.

Watanzania wengi ikiwemo pamojavna wewe wanaamini mafanikio yanapatikana kwa kusoma kisha kuajiriwa serikalini, ujenge nyumba.
Exposure na lugha na mfumo wa maisha yenye mentality za kijamaa ndio yamechangia
 
Ni bora hadithi za kilimo cha matikiti kwa eka kuliko kuzika pesa chini.
Inategemeana na tafsiri yako ya kuzika pesa, maana thamani ya pesa ni kwenye vitu vinavyoonekana.

Binafsi nikiwa kwangu ndio nakuwa na utulivu wa kupanga na mipango ikapangika na ikatekelezeka kuliko kubanana kwenye nyumba za watu.
 
Mimi naona kuwa na nyumba ni muhimu sana kama huna kipato cha uhakika. Ila kama una uwekezaji wenye uhakika sidhani kama kuna haja ya kukimbilia kujenga
Asiye na kipato cha uhakika si ndio anatakiwa awekeze kwenye biashara ili apate zaidi sasa akitumia mtaji alionao kujenga anwezaje kuwekeza na kuwa na kipato cha uhakika?
Kwa maana nyingine umesema tajiri aendelee kuwa tajiri na masikini abaki na umasikini wake.

Mimi nadhani hapao ni vice versa
Asiye na kipato cha uhakika aelekeze nguvu na akili zake zote kuwekeza na kujijenga kiuchumi na aliye na uwekezaji wa uhakika hakuna shida akiamua kujenga nyumba ya kuishi.

Kwangu mimi shida si kuwekeza shida ni "Elimu ya uwekezaji"
kundi kubwa la watu hasa wa kipato cha chini na cha kati wanakosa elimu na ujuzi wa uwekezaji hii inapelekea kufeli mara kwa mara kwenye biashara na wengine wanawaangalia hao(waliofeli) kama mifano.

Kwenye kila biashara ambayo mmoja analalamika ilimwangusha na kumpa hasara kuna mwingine biashara hiyo hiyo imemtajirisha na anifanya mpaka leo kwenye hiyo nchi na sera hizo hizo anazolaumu mwingine.
Bado unadhani shida ni sera au sheria nk
Shida ni kutokuwa na taarifa sahihi na za kutosha za biashara/uwekezaji unaotaka kufanya.
Watu wengi wanatanguliza fedha kwenye biashara kabla ya kuwekeza "muda" na kutafuta ujuzi/uzoefu.
 
Unajenga taratibu ndani ya miaka kadhaa nyumba ya 30mln inaisha .

Watumishi Wana salary na Wana uhakika wa mwisho wa mwezi.
Miaka kadhaa mingap? Unajua mwalimu wa shule ya msingi mwenye take home ya 340k akichukua hyo mil 10 kwa makato ya 200k kila mwezi anabaki na 140k kwa miaka 7..
Huyo mtumishi akiwa na familia inayo mtegemea pia ana ndugu wanamtegemea..ataishije kwa kipindi chote hicho na hana posho wala marupurupu yoyote.
Na mbaya zaid nyumba haitaisha kwa pesa hyo..ataishi kwa kuacha kadi mitaani na kuwa omba omba..

Hyo ndo hali halisi.
 
Back
Top Bottom