Kujenga nyumba na kununua magari ni sababu mojawapo ya Umasikini

Kujenga nyumba na kununua magari ni sababu mojawapo ya Umasikini

Kama hauna familia sawa anza kufanyabiashara ila kwa wakina sisi tulioanzaga mchezo mbaya mapema tulijikuta tupo chuo mwaka wa pili tu tayari tuna mke na mtoto.
Hadi unakuja kupata kazi unajikuta familia inakuforce uwe na nyumba ukicheki kupanga nyumba nzima ni gharama sana inakubidi uanze kujenga maana kuishi kwenye chumba na sebule ni udhalili.
Nakumbuka nilijimeki within 6months nikanunua plot, kisha tukafunga mkanda kuanza ujenzi ilikuwa kila mwisho wa mwezi naenda kulipia tofali hardware to make story short.
Ndani ya miaka mitatu mfululizo nilikuwa nishamaliza boma kupaua na fence kusema kweli baada ya kupachika grills plasta na floor nilihamia kwangu mambo ya finishing nilifanya nikiwa humohumo maana nilijiapizaga kuwa sitaki kuanza kusomesha hukunikiwa nyumba ya kupanga.
Ushauri kwa vijana kujenga sio matumizi ya hovyo ya pesa maana nyumba ni pumziko, heshima, utulivu, kituo cha kudumu cha familia yako, kitunza dhiki na shida zako.
Mwenye macho na aone na mwenye masikio asikie[emoji4]
Naona watu wengi humu ni wafanyakazi na ndio wananaounga mkono hoja ya ujenzi wa nyumba ya makazi dhidi ya biashara.
Kwangu mimi mfanyabiashara ni tofauti, huu wimbo wa kujenga nyumba ya makazi hata ukiniimbia kwa miaka 10 sitakuelewa.

Nitajenga pale tu malengo yangu ki biashara yatakapotimia.
Kama ninaishi vyema na familia yangu sioni haja ya kukimbilia kujenga nyumba just for Pride.
 
Familia ya Trump imetajirika kwa kujenga majumba, kujenga nyumba ya kuishi sio chanzo cha umaskini, hata matajiri kama Mo na bakheresa, GSM wote wanaishi, kwenye ma mansion ya kibabe,
Kinacholeta umaskini kwa watu weusi, au bongo ni kutokuwekeza, kutegemea ajira na mshahara kwa kila kitu, unasemaje kununua magari ni chanzo cha umaskini, wakati shabiby anamiriki mabasi zaidi ya 200+! Unaweza, ukawa na gari, ukitoka kqzini unapitia kwenye maduka yako kama 10 ya mpesa,stationary, unapitia kwenye karakana yako ya fanicha, harafu ndio unaenda nyumbani kibaha!
Sasa, hapo bila gari hiyo mizunguko utaifanya kwa boda!?
Wanaojipa umaskini, ni wale ameajiliwa, kajenga nyumba, kanunua gari ya kupigia misele!maintenance ya gari kila kitu kinabebwa na mshahara!! Ajira ikiisha, na umaskini uleeeee
Hizo nyumba alizojenga trump ni za biashara na sio za kuishi yeye na hayo magari ya shabiby ni ya biashara! Watanzania wengi wanadhani kujenga nyumba ya kuishi ndo mafanikio bila kujua kujenga nyumba ya kuishi ni liability kubwa mno maishani!
 
Nimenunua Treasury bond za milioni 104 na Bond fund ya UTT ya vipande vya Milioni 104, huku UTT natumiwa faida kila mwezi ile ya BOT natumiwa kila baada ya miezi 6 katika mwaka. chanzo cha fedha hizo zote niliuza shamba kubwa la miti iringa kwa wazungu walilitaka nimehamia dar ila nimepanga katikati ya mji.. mtoa mada yupo sahihi..
Asee hongera sanaa, Mimi kwa Sasa teali na nimewekeza mfuko wa bond UTT, Sasa naitafutaa hati fungani, treasure Bond ya.miaka 20 au 25, then niache kibarua.. my target UTT ni kupata gawio la 2 mil plus..na treasure bonds mil 90 kwa mwaka. Gawio la UTT litanifanya niishi kama mtumishi wa serikari maana Kila mwisho wa mwezi tutakuwa tunakutana bank na watumishi wa serikari wao wakiwa wanasubiri mshahara Mimi nasubiri gawio.
 
Nimenunua Treasury bond za milioni 104 na Bond fund ya UTT ya vipande vya Milioni 104, huku UTT natumiwa faida kila mwezi ile ya BOT natumiwa kila baada ya miezi 6 katika mwaka. chanzo cha fedha hizo zote niliuza shamba kubwa la miti iringa kwa wazungu walilitaka nimehamia dar ila nimepanga katikati ya mji.. mtoa mada yupo sahihi..
Natamani kujua zaidi hii kitu. Mfano nikiwa na mill. tano nawezaje pata faida kwenye hiyo mifuko.
 
Asee hongera sanaa, Mimi kwa Sasa teali na nimewekeza mfuko wa bond UTT, Sasa naitafutaa hati fungani, treasure Bond ya.miaka 20 au 25, then niache kibarua.. my target UTT ni kupata gawio la 2 mil plus..na treasure bonds mil 90 kwa mwaka. Gawio la UTT litanifanya niishi kama mtumishi wa serikari maana Kila mwisho wa mwezi tutakuwa tunakutana bank na watumishi wa serikari wao wakiwa wanasubiri mshahara Mimi nasubiri gawio.
Hongera sana kaka
 
Natamani kujua zaidi hii kitu. Mfano nikiwa na mill. tano nawezaje pata faida kwenye hiyo mifuko.
Kama una Milioni tano approximately faida ni kama elfu 50 na chenji kwa mwezi.. UTT bond fund faida kwa mwaka ni 14.9%, Treasury Bond ya BOT inategemea unanunua wakati gani but huwa inakuwa 12% mpaka 13% kwa mwaka na mara chache sana inafika mpaka 15% inategemea wakati gani unanunua hati fungani hizo..
 
Kama una Milioni tano approximately faida ni kama elfu 50 na chenji kwa mwezi.. UTT bond fund faida kwa mwaka ni 14.9%, Treasury Bond ya BOT inategemea unanunua wakati gani but huwa inakuwa 12% mpaka 13% kwa mwaka na mara chache sana inafika mpaka 15% inategemea wakati gani unanunua hati fungani hizo..
Na hii una kua unaipata maisha, au kuna muda maalumu. Na je unaweza ukawa unaongeza kila unapopata pesa nyingine ili kukuza faida? Maswali mengi nivumilie hii kitu naiskiaga tu.
 
Habari,

"Tafuta kiwanja, Jenga, Oa/Olewa, nunua mkoko", njia hii na mawazo haya yamekuwa kwa vijana wengi wanaoanza maisha, hususani waliobarikiwa kupata ajira au biashara zao binafsi ambazo zinawapa kipato flani cha kuendesha maisha yao. Kwa uzoefu wangu hii imekuwa kati ya sababu moja kubwa zinazosababisha watu kuwa maskini na kushindwa kufikia uhuru wa kifedha.

Lakini tujiulize swali la msingi, kwanini watu wengi wameamua kuchagua njia hii ya maisha. Nimefanikiwa kuwahoji watu wengi kidogo kuhusu hili na majibu niliyoyapata mengi yalikuwa kama ifuatavyo:

  • Gharama ya kupanga nyumba ziko juu sana, ni bora kujenga ya kwako.
  • Nyumba ni asset.
  • Usafiri ni shida sana eneo niliko jenga ni bora kuvuta gari yangu.
  • Mama/baba mwenye nyumba ana gubu sana.
  • Nikiwa na kwangu nakuwa na uhuru mkubwa sana.
  • Siku nikifukuzwa kazi au biashara ikiyumba nibaki na pakulala na familia yangu.

Sababu hapo juu nyingi ni za maana kabisa ila tatizo ni kwamba njia zilizotumika kutatua hizo changamoto zinaongeza changamoto zaidi, kivipi?. Ngoja tujadili mambo machache kuhusiana na maisha ya watu wengi hususani mijini (e.g. Dar):

- Wengi wananunua viwanja maeneo ya mbali kutoka mahali wanapofanyia shughuli zao zinazowapa kipato.
- Baadhi ya hayo maeneo yana changamoto za miundombinu ya maji, umeme, barabara na hata kiusalama.
  • Wengi wanajenga kwa kuunga unga sana, unaweza jenga nyumba hata miaka sita au zaidi. Kuna msemo wanasema "nyumba haiishi".
  • Nyumba nyingi wanazojenga watu kukaa zinakuwa ni kubwa na za kifahari bila kukumbuka lengo la mwanzo lilikuwa ni makazi tu na sio jengo la maonesho (Hapo utajibiwa kuwa tunajenga mara moja ya kuzeekea)

Kuzingatia hizo hoja hapo juu, yafuatayo yanakuwa ni matokeo ya gharama za maisha baada ya huyu mtu kuhamia kwake:

  • Gharama za usafiri au mafuta zinakuwa juu ukilinganisha na awali.
  • Mazingira yanakuwa sio rafiki kwa familia kuishi, maana nyumba nyingi zinakuwa bado hazijaisha (Wengine wanasema unakuwa unaishi site).
  • Kama una gari, gharama za matengenezo zinakuwa juu kwa sababu ya pengine barabara kuwa mbaya, lakini kwa kuwa unasafiri umbali mrefu kila siku, basi hata service ya gari utafanya mara nyingi zaidi.
  • Pia kama una gari utalazimika kuendesha gari umbali mrefu kila siku, hii si nzuri kwako kiafya.
  • Gharama za umeme na maji pia zinaweza kuongezeka kwa kuwa nyumba ni kubwa sasa na pengine maji hayajafika.
  • Maeneo mengine hata watu hawajahamia wengi hivyo hata usalama unakuwa hatarini.
  • Mara nyingi unaweza ukajikuta mbali na huduma bora za kijamii ikiwemo hospitali, shule, n.k.

***NOTE: Gharama zinaweza kuongezeka ukilinganisha na mwanzo.

Kwanini kuna hofu ya kuwekeza hizo pesa?

Tujiulize swali hili la msingi. Ni kweli baadhi ya watu wanatamani sana kuffanya biashara, lakini wengi wanasema, BIASHARA HAZITABIRIKI. Ni kweli kabisa, lakini ukweli ni kwamba hilo sio tatizo la watu kutokuwekeza.
SHIDA KUBWA NI WATU KUTOKUWA NA ELIMU YA FEDHA. Hili ni jambo la muhimu sana kwa vijana kupata elimu. kwanza kabisa sio kweli kwamba ukitaka kuwekeza ni lazima ukafanye biashara fulani kama kuuza nguo, vinywaji au duka la mangi. Unaweza ukafanya uwekezaji kwa njia nyingi sana ambazo hazitahitaji your active time kuweza kusimamia ila mwisho wa siku ukaja kuwa na uchumi mkubwa kabisa. Uwekezaji huu ni kama mifano ifuatayo:

  • Kununua viwanja na mashamba (Kumba muda unavyokwenda ardhi inapanda thamani lakini nyumba inashuka thamani)
  • Kununua hisa za makampuni
  • Tressury Bonds and Bills
  • Mifuko ya uwekezaji ya pamoja (e.g. UTTAMIS)
  • Fixed deposits accounts
  • Kuwekeza kwenye elimu (Hii sio lazima zile za darasani, inaweza kuwa hata kujiendeleza katika fani flani)
  • N.k.

La muhimu ni kupata elimu sahihi ya mambo ya fedha ili ujue jinsi ya kufanya maamuzi ni vipi utumie pesa yako.


Ngoja nitoe mfano halisi mmoja ulio hai kabisa kwa lengo la kupata uhalisia wa ninacho kisema:

Mwaka 2013 niliajiriwa mahali na tulikuwa kama waajiriwa sita wapya katika hiyo kampuni, mwenzetu mmoja alikuwa na uelewa mkubwa sana wa mambo ya fedha, na mara nyingi alikuwa anatushauri kuhusu haya mambo lakini tulikuwa tunamuona kama kachanganyikiwa: Mimi na wenzangu wengine wa tano tulikwenda mahali tukanunua viwanja na kuanza kujenga kwa kasi sana na badae tukachuku na mikopo kuongeza kasi hiyo. Kwa haraka haraka kwa wastani tuliweza kutenga kama milioni moja kwa mwezi kila mmoja wetu kwa ajiri ya miradi ya ujenzi. Mungu si athumani baada ya miaka mitatu paka minne wote watano tukawa tumehamia kwenye site zetu huku tukiendelea na finishing.

Jamaa alikuwa kila mwezi anaweka milioni moja kwenye mfuko mmoja wa uwekezaji wa pamoja na alikuwa anapata average interest kama ya 11.85% kwa mwaka. Badae akawa ananunua na bond za serikali pamoja na mambo ya kununua mashamba mbali kidogo na mji yakichangamka anakata na kuyauza. Kiufupi jamaa ana zaidi ya milioni 200 kwenye mfuko anaoweka pesa pamoja na kuwa na asset ya viwanja na mashamba na benki ana pesa chafu.

Turudi kwetu tuliojenga na sasa tuna mikoko yetu, umbali wa kwenda na kurudi nyumbani ni 50 Km kila siku. Na pia siwezi pata picha ile hofu ya kwamba nikiachishwa kazi bado ipo maana siwezi nikala nyumba.

Kwa ajili ya muda niishie hapa kwa leo, nipate mawazo ya watu wengine pia. Kiufupi mimi naona kuna mitaji mingi ya biashara na uwekezaji inapotea kwa huu mwamvuli wa kujenga na kununua hii mikoko.

Ahsanteni!!!
Umeongea point mkuu...Ila sikiliza ma experts pia
 
Kujenga sio tatizo /kununua gar tatizo n pale unapojenga wakat ambao hauna stable income,hauna vyanzo vya uhakika vya kipato (specifically passive income)

Ukiwa na kipato cha uhakika,nyumba inasimama kwa miez 2 tu tena n nyumba sio kupanga matofali hizi mtu anajenga miaka 5 haijaisha anahamia huku fundi anapiga plasta [emoji28]

Nashaur hv,watu tuhakikishe tuna vipato endelevu na vya uhakika,ukishafkia uhuru wa kifedha utajenga na kuish popote na muda wowote

Binafsi ukinipa nyumba ya100M na investment inayonipa profit ya 1M monthly consistently nachkua hyo investment


Kujenga nyumba ya kuish kwa mkopo/‘mshahara n seriously mental problem.

Ama mtu unanunua kiwanja alaf ukiumwa au ukiuguliwa unakiuza [emoji28]
 
Kwa ujumla, mawazo ya wananzengo yanafanyakazi kulingana na mahali na hali ya maisha ya familia wanakotokea.

Mawazo yote ni mema na mazuri (Kujenga au kufanya biashara/investment/kuwa na gari kabla ya kujenga n.k) ilimradi yanatupeleka kwenye DHUMUNI/LENGO la MWISHO la mhusika=Maisha bora.

Maisha ni kuchagua na kwa kuwa tumeumbwa kila mmoja kwa madhumuni tofauti hapa duniani, wengine wawe MATAJIRI na wengi sana wawe MASIKINI.

Kila mmoja ashikilie kile anachokiamini na atafika kule atakako.
 
Unaweza ukasema hivyo ndugu lakini kuna watu walinunua mashamba mvuti, msongola na maeneo mengine miaka 5 - 8 iliyopita wakati huo ilikuwa poli, lakini huwezi kuamini leo hii mashamba hayo yalikatwa katwa vipande vidogo vidogo, kila kipande Milioni 2.5, mtu anaheka zake tatu kila heka katowa vipande 8 na kila heka moja aliinunua laki 1, leo hii kapata faida nyingi sana.

Baadhi ya viongozi duniani wanawekeza sana kwenye ardhi, si kwamba wajinga ila wanajuwa kibaruwa kikiota nyasi basi ardhi itakuwa suluhisho la kusonga mbele.

Tunatolea mfano ardhi kwa sababu unaweza kufanyia mambo mengi, unaweza usiize ila ukawa unalima mihogo, karanga, kufugia na n.k, pia ni uwekezaji.
ARIRHI NI FACTOR MOJAWAPO YA UCHUMI ILA KAMA HUNA KITU UNAIFANYIA NI KAZI BURE...unaweza kufanya chochote kikakupa fedha....kuna eneo nilinunua nikaona nijenge fensi... nimepotezxa hela nina niaka kumi ninalo halijawahi nipa hata sent...hopu pekee niliyonayo labda nikiuza nitapata mtonyo wa maana ila hakuna jipya fedha niliyoiwekeza hapo ningejenga guest au nyumba za wapangaji mjini ningekuwa na maokoto kiaina.. kwa hio ardhi sio aset hadi pale utakapoiuza au kukuingizia hedha... kuwekeza kwenye ardhi nisawa na wanaowekeza kwenye mazao kwalengo la kupata faida tunaiita capital gain(sio biashara)mzee wangu kishimba alinifundisha miaka hio kuweka stock ya mchele so biashara....nunua then uza ukipanda unapanda nao ukishuka unashuka nao unaangalia faida tu.....tusijifariji na kumiliki naeneo yasiyokuwa na chochote ukifanyacho fuga hapo au fanya chochote..
 
Kwa ujumla, mawazo ya wananzengo yanafanyakazi kulingana na mahali na hali ya maisha ya familia wanakotokea.

Mawazo yote ni mema na mazuri (Kujenga au kufanya biashara/investment/kuwa na gari kabla ya kujenga n.k) ilimradi yanatupeleka kwenye DHUMUNI/LENGO la MWISHO la mhusika=Maisha bora.

Maisha ni kuchagua na kwa kuwa tumeumbwa kila mmoja kwa madhumuni tofauti hapa duniani, wengine wawe MATAJIRI na wengi sana wawe MASIKINI.

Kila mmoja ashikilie kile anachokiamini na atafika kule atakako.
looser mind set..... chakata hoja...
 
ARIRHI NI FACTOR MOJAWAPO YA UCHUMI ILA KAMA HUNA KITU UNAIFANYIA NI KAZI BURE...unaweza kufanya chochote kikakupa fedha....kuna eneo nilinunua nikaona nijenge fensi... nimepotezxa hela nina niaka kumi ninalo halijawahi nipa hata sent...hopu pekee niliyonayo labda nikiuza nitapata mtonyo wa maana ila hakuna jipya fedha niliyoiwekeza hapo ningejenga guest au nyumba za wapangaji mjini ningekuwa na maokoto kiaina.. kwa hio ardhi sio aset hadi pale utakapoiuza au kukuingizia hedha... kuwekeza kwenye ardhi nisawa na wanaowekeza kwenye mazao kwalengo la kupata faida tunaiita capital gain(sio biashara)mzee wangu kishimba alinifundisha miaka hio kuweka stock ya mchele so biashara....nunua then uza ukipanda unapanda nao ukishuka unashuka nao unaangalia faida tu.....tusijifariji na kumiliki naeneo yasiyokuwa na chochote ukifanyacho fuga hapo au fanya chochote..
..ni kweli mkuu ukiweza plot unayonunua fanyia kitu kinachokuingizia pesa...ila kuwa na plot ni faida zaidi ya kuweka bank..pesa inayokaa bank tu kama akiba inaliwa na inflation na depreciation..pesa unayoiweka kwa plot inapambana na inflation na depreciation hasa maeneo strategic...matumizi ya plot hasa yenye title deed inaweza kuwa mengi ikiwepo kulima mazao kama mboga-mboga kibiashara hasa kwa kutumia greenhouse technology, kukodishia watu kwa busness kama kuosha magari, kufyatua tofali, gulio, etc; pia unaweza kuchukua hati yako ukaenda bank ukakopea mkopo na kufanya mambo mengine!

..kwenye eneo la mkopo kama plot umepata sehemu strategic na plot imekaa muda ikapanda bei unaweza kuchukua mkopo mkubwa na kununua bonds ambayo labda zina rate kubwa kuliko interest rate ya mkopo..then malipo ya bond yakawa yanalipa mkopo hadi muda wa kurudisha deni la bank unaisha na wewe unabaki na pesa&interest ya bond na plot yako...mfano plot ina thamani kuanzia 200m hii ukiichukulia bond ya 25yrs yenye rate ya 12.56% kwa sasa unaweza kabisa kulipa mkopo ambao labda umepata kwa bank au saccos wenye rate chini ya 10%.
 
schools, in economics, taught us that house is an asset, but Robert Kiyosaki, in his book told that a house is a liability, which is which!
Naona watu wengi humu ni wafanyakazi na ndio wananaounga mkono hoja ya ujenzi wa nyumba ya makazi dhidi ya biashara.
Kwangu mimi mfanyabiashara ni tofauti, huu wimbo wa kujenga nyumba ya makazi hata ukiniimbia kwa miaka 10 sitakuelewa.

Nitajenga pale tu malengo yangu ki biashara yatakapotimia.
Kama ninaishi vyema na familia yangu sioni haja ya kukimbilia kujenga nyumba just for Pride.
 
schools, in economics, taugh us that house is an asset, but Robert Kiyosaki told in his book that a house is a liability, which is which!
Naona watu wengi humu ni wafanyakazi na ndio wananaounga mkono hoja ya ujenzi wa nyumba ya makazi dhidi ya biashara.
Kwangu mimi mfanyabiashara ni tofauti, huu wimbo wa kujenga nyumba ya makazi hata ukiniimbia kwa miaka 10 sitakuelewa.

Nitajenga pale tu malengo yangu ki biashara yatakapotimia.
Kama ninaishi vyema na familia yangu sioni haja ya kukimbilia kujenga nyumba just for Pride.
 
Ukijenga nyumba kwa lengo ya kua dhamana au security bank hapo ndo umeferi kabisa bora unge tunza zile pesa ndo zikusaindie kupanua biashara yako Bank za Tz ni wezi ma lengo yao sio kukuinua but kukufilisi nyumba ya 200m itadhamini mkopo wa 30m au 50m ndo watakupa mkopo hiyo njia imefilisi wafanya biashara wengi.......kwahiyo ni vizuri kutunza cash kuliko kuiweka kwenye nyumba liquidity ni muhimu kuliko solid assets kwasbb na benki zinahitaji faida lazima wakufilisi.
Mdau sijui uko kwenye sekta ipi (umeajiriwa/biashara) dhumini kubwa la kujenga ni kuwa makazi au biashara sasa kama upo kwenye biashara dhamana (security) ni muhimu Sana hasa kama unataka kukuza mtaji wa biashara yako. Kwa namna gani unaweza kutunza pesa mfano upate zabuni ya 500m utasave kwa muda gani kiasi hicho zaidi ya kutumia taasisi za fedha kama benki kuhusu malengo ya benki nafikiri hauko sahihi huo ni mtazamo wako hasi juu yao mbona wengi wamefanikiwa kwa kuzitumia taasisi za fedha na kukuza biashara zao​
 
Back
Top Bottom