Kujenga ukiwa tayari una familia si mchezo

Majukumu kibao mkuu huku Kodi, matumizi ya daily , wazazi upige tufu kidg na ada za watoto na matumizi yao ya kila siku shule sio kitoto lazima kichwa kiumee alafu na umri nao ndo unatupa mkono dah
Una umri gani mkuu?
Ili tupate uwiano wa majukumu na umri husika.
 
Ni ndogo au kubwa? mimi wakati naacha kazi hiyo ya utumwa ya kwa jiliwa na wa bongo wenzangu nilikua na lipwa 1.63m take home
Sasa sisi wa tamisemi tunaopata take home ya 800k itakuaje
 
Nyumban kwa wazazi unapigiwa simu unaambiwa hatuna ela ya kula....

Hujakaaa sawa umeungwa kwenye group la michango, afu unaambiwa ahidi...

Hujakaa sawa unaambiwa gesi inaisha, ila ya nondo ipunguze ununue gas....

Nyie wanaume tumeumbwa mateso
Unapita mule mule mkuu
Hujakosea
 
Kujenga Ni hobbies
Ukifanya unachokipenda hutojua pesa imepatikana vipi[emoji16]
 
Majukumu kibao mkuu huku Kodi, matumizi ya daily , wazazi upige tufu kidg na ada za watoto na matumizi yao ya kila siku shule sio kitoto lazima kichwa kiumee alafu na umri nao ndo unatupa mkono dah
Kama ikibidi jaribu punguza matumizi yasiyo ya lazima ikiwemo ada za watoto walio shule za msingi, hamishia shule zetu za St. Kayumba ili upate kusave.

Tunashindwa kufikia malengo makubwa kwa sababu kila kitu tunataka tuvimiliki kwa wakati mmoja ilhali kipato hakitoshi.

Maisha mazuri utayapata kupitia malengo yako.
 
Dah nawashauri vijana kama uneweza kujenga ukiwa bado hujaanza familia itakua bora sana kuliko kusubiri wakati majukumu yamekua mengi dah inasumbua Sana inaweza ata kuchukua miaka 10 kukamisha nyumba kila kitu.
Nina Imani tatizo sio uwepo wa Familia, tatizo ni hela kutotosha mahitaji.
 
Kweli mkuu aisee Wacha kupambanee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…