Wanawake bana nchi tuwape bado ajira iwe 50/50 na bado tuwahudumie nyie na watoto. Hela zenu huwa mnapeleka wapi au ndio kule mnapopanua miguu muoshwe miguu na kupakwa kucha rangi!
Si ndio matumizi ya hela zenu na bado hujaenda kufanyiwa wax ya kipochi manyoya!Kuoshwa miguu na kupakwa rangi mnagharamia nyie pia
Mazingra ninayofanyia kazi hili swala huwa nakutana nalo sana wanawake wengi wanakuja na madai ya kutohudumiwa watoto lakini anapoitwa mwanaume mambo yanakuwa tofauti. Wanaume wengi wanaptia magum mengi kutoka kwa wenza wao lakini wanakaa kimya. Ushauri kwa wanaume wenzangu ukigombana na mke chukua wanao au weka mazingira ya kuwahudumia maana wengne wanatoa huduma kwa ajili ya watoto lakini zile huduma haziwafikii walengwa.
Si kweli kwa sasa ukitoa huo ukanda wote wako hivyosisi kwetu hatuachagi mtoto nyuma lakini kuna ukanda(siutaji) wao kuzaa na kuacha ni kawaida tuu.
Soma vizuri komenti yako kabla sijakucharua ujicharue mwenyewe..Mekunywa juisi ya chungwa tuu KENZY 😅😅😅😅
Kinachowapata hao wanaume unaowasema ni cha kujitakia
Kwani ilikua lazima kupanda mbegu kwenye shamba lenye magugu? Au walibakwa hadi mimba zikatokea[emoji41]
Mnisamehe tuu
unatumia nguvu nyingi kuupinga ukweli ila tambua hamna mwanadam anayeweza kutambua moyo wa mwingne au kujua kle cha ndani. Maana kama uwezekano wa kuona ndani ya mioyo ungekuwepo haya tunayojadili hapa yasingekuwepo.
Nadhani kwa mwanaume Baba kumkimbia mwanao iwe ni last option ukiwepo Duniani.Zamani ilikua ni furaha, heshma na sifa njema mwanaume kupata watoto, kuwalea kwa mahitaji na mafundisho bora lakini siku hizi mambo yamebadilika! Wanaume wengi wamekua na ka desturi kapya kabisaaa. Achana na kale ka kukataa mimba ambazo wanajua kabisa wao ni wahusika; Wanaume wengi wamekua wazito, wazembe na wakatili mno linapokuja swala la kuwahudumia watoto wao.
Kwa taratibu za kiimani na kidesturi mtoto ni wa mwanaume sio kwa ubini tuu; bali hata mfumo mzima wa kupata watoto mwanamke ni kama shamba zuri lenye rutuba na mwanaume ndio mkulima mwenye mbegu zake na yeye ndio anaamua akazipande kwenye shamba gani, azitunze ili apate matunda bora.
Leo nimekutana na kesi ya mwanaume mmoja hospitalini, mtu mzima kama baba kwangu anaumwa vibaya. Watoto zake na mke wake wameshakata tamaa ya kumuuguza sababu wameshatumia pesa nyingi sana na hawana tena uwezo. Ghafla wakaingia watu wawili mwanaume na mwanamke, wakamfuata kwenye kitanda na kuomba faragha waongee nae kwa muda, baada ya muda daktari akaitwa..... kumbe wale ni watoto wake aliwakimbia ila baada ya kupokea taarifa za kuugua kwa baba yao toka kwa mama yao ambaye anaishi hapa wamefanya mipango yote na sasa wamekuja kumchukua kwenda kutibiwa nje ya nchi.
Yule baba amelia jamani, sijui kile kilio kilikua cha aibu? Cha majuto? Au cha uchungu maana kilikua kilio cha nguvu na kwikwi hadi watu wengine machozi yakawa yanawatoka.
Baba zetu, kaka zetu, watoto zetu tunzeni watoto wenu mnaozaa. Haijalishi ulimpata mtoto ukiwa katika hali gani ila kwa kuwa ni mtoto wako wajibika tuu kwa nafasi yako na Mungu atakubariki kwa nafasi yake.
Baba mchungaji Daniel Mugogo anakazia hapa
View attachment 2197930
Mungu awabariki wanaume wote mnaotunza watoto zenu bila shurti
Kuna huyu alikuwa girlfriend wangu, alipopata ujauzito, tulijikuta tupo watatu wote kila mmoja anadai mimba ya kwake [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mwisho wa siku mtoto nalea mimi, natamani niishi nae tulee mtoto, sina amani naye. Baadhi ya wanawake mnahatari sana [emoji23][emoji23][emoji23]
Nadhani kwa mwanaume Baba kumkimbia mwanao iwe ni last option ukiwepo Duniani.
Ila kwenye familia yanatokea mengi saana asikuambie mtu.....mengi Saana
Ni kweli....Pamoja mengi tuendelee kupambania hili
"Nadhani kwa mwanaume Baba kumkimbia mwanao iwe ni last option ukiwepo Duniani."
Na unapo opt kukimbia ukimbilie mautini, usimtelekeze mtoto wako ukiwa una uhai
Tunachoongelea hapa ni mtoto
Huwezi telekeza mtoto ati sababu mama uliyezaa nae ulikua huujui moyo wake. Leo mtoto hayo mambo ya moyo wa mamake hayahusiki
Asante kwa maombi mwali.Baba mjengo wewe hujawahi kuniangusha
Yesu aendelee kukubariki kwa baraka za moyoni na za mwilini
Unatulaumu as if ushawahi tufundisha au Jamii ya sasa inafundisha Nini maana ya uanaume , Wanaume kamili hawaibuki tuu wanatengenezwa.
Poor parenting strategies ndo matokeo ya yote hayo.
Jamii inahusika kwa kiasi kikubwa
aise mungu si athumaniZamani ilikua ni furaha, heshma na sifa njema mwanaume kupata watoto, kuwalea kwa mahitaji na mafundisho bora lakini siku hizi mambo yamebadilika! Wanaume wengi wamekua na ka desturi kapya kabisaaa. Achana na kale ka kukataa mimba ambazo wanajua kabisa wao ni wahusika; Wanaume wengi wamekua wazito, wazembe na wakatili mno linapokuja swala la kuwahudumia watoto wao.
Kwa taratibu za kiimani na kidesturi mtoto ni wa mwanaume sio kwa ubini tuu; bali hata mfumo mzima wa kupata watoto mwanamke ni kama shamba zuri lenye rutuba na mwanaume ndio mkulima mwenye mbegu zake na yeye ndio anaamua akazipande kwenye shamba gani, azitunze ili apate matunda bora.
Leo nimekutana na kesi ya mwanaume mmoja hospitalini, mtu mzima kama baba kwangu anaumwa vibaya. Watoto zake na mke wake wameshakata tamaa ya kumuuguza sababu wameshatumia pesa nyingi sana na hawana tena uwezo. Ghafla wakaingia watu wawili mwanaume na mwanamke, wakamfuata kwenye kitanda na kuomba faragha waongee nae kwa muda, baada ya muda daktari akaitwa..... kumbe wale ni watoto wake aliwakimbia ila baada ya kupokea taarifa za kuugua kwa baba yao toka kwa mama yao ambaye anaishi hapa wamefanya mipango yote na sasa wamekuja kumchukua kwenda kutibiwa nje ya nchi.
Yule baba amelia jamani, sijui kile kilio kilikua cha aibu? Cha majuto? Au cha uchungu maana kilikua kilio cha nguvu na kwikwi hadi watu wengine machozi yakawa yanawatoka.
Baba zetu, kaka zetu, watoto zetu tunzeni watoto wenu mnaozaa. Haijalishi ulimpata mtoto ukiwa katika hali gani ila kwa kuwa ni mtoto wako wajibika tuu kwa nafasi yako na Mungu atakubariki kwa nafasi yake.
Baba mchungaji Daniel Mugogo anakazia hapa
View attachment 2197930
Mungu awabariki wanaume wote mnaotunza watoto zenu bila shurti