Kukataliwa Goli la Simba dhidi ya Coastal, Azam TV Hamtutendei Haki Wateja Wenu

Kukataliwa Goli la Simba dhidi ya Coastal, Azam TV Hamtutendei Haki Wateja Wenu

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Kwema Wakuu,

Najua hili litawafikia sababu JF ni Platform kubwa. Nyinyi Azam TV ndio mmepewa haki ya kuonyesha Mpira wa Ligi yetu pendwa ya NBC Premier League. Sisi Subscribers wenu tuna haki ya kupata Matangazo hayo katika ubora wa hali ya juu bila ukakasi. Yaani Sisi kwa kununua ving'amuzi vyenu automatically tunakua tumeingia makubaliano (implied contract ) kua mtatuonyesha mpira katika ubora wake.

Goli lililofungwa baada ya Kona ya Shomari Kapombe lilikataliwa kwa madai kua Mpira huo ulizungukia kwanza nje (curve) kabla kisha ukarudi ndani. Mpaka mpira unaisha Azam wameshindwa kuonyesha hiyo "Curve". Hata Watangazaji wenyewe wamebaki na kigugumizi maana hakuna Video kuthibitisha mpira uli curve nje ya mstari.

Solution hapa ilikua ni kuwepo kamera kwenye kila kona (kibendera) lakini kwa ubahili wa Azam wameshindwa kuweka. Ina maana Simba jana wangeweza kusema Refa aliwahujumu kumbe maamuzi ya Refa yalikua sahihi.

Au tuseme ingekua ndio Coastal Union wamefunga lile goli likakataliwa ingeweza kudhaniwa Simba anabebwa. Hii yote ni sababu Azam wameshindwa kuweka Kamera za kutosha Uwanjani.

Nawaza ni kiasi gani tunalipia ving'amuzi ambavyo kila kukicha vinapanda bei, na Kamera ni kiasi gani kwa kampuni kama Azam kushindwa kuweka kila pembe ya uwanja. Hii si sawa, na ni unyonyaji mkubwa tunafanyiwa.
 
Azam wekeni Mambo sawa bana Yani replay hazionekani "clear" kabisa sasa sijui hamlioni...
 
Azam kwenye kamera bado sana,hili suala ni mda mrefu wadau wa soka wamekuwa wakiliongelea hapa lakin wamefeli kufanya maboresho
 
Simba wameacha kulalamika wao wanacheza mpira tu siku hizi.
 
Ukitaka uone azam wana matatzo angalia mechi za timu kama Mbeya kwanza vs Ruvu,kamera itayotumika hapo ni moja tu,yan unaangalia mpira huoni hata jinsi mchezaji anavyokimbia ni blurry na kutetemeka kwa camera,
Hutaweza kuona replay hata moja,
 
TFF sijui kama walizingatia katika mkataba kuhusu ubora wa picha, pamoja na idadi za kamera za kuwepo uwanjani.

Kama kwa mkapa tu, bado wanapata shida, sijui huko mikoani inakuwaje.
 
Jama eeh, Nyie Jueni tu Wale Marefa Walishapokea Kitu Kidogo...! Sasa Ni Kama Walishindwa Kukataa hata Lile Lingine La Kagere La tatu...! Lakini kama amri ingekuwa Yao Bao La Kagere Wangesema faulo ..Penati iende Simba..!
Chezea 'furusi' wewe tena Kutoka Jiesieee..........
 
Hivi ukipiga ngumi refa kama huyu unashitakiwa?
Hiyo video haithibitishi kwa 100% kuwa kuwa mpira haukuenda nje na kurudi. Mchukuaji alitakiwa awe amekatwa na mstari katikati kama alivyo mshika kibendera. Camera iko kulia kwa goal line. Video haijamaliza utata
 
Hiyo video haithibitishi kwa 100% kuwa kuwa mpira haukuenda nje na kurudi. Mchukuaji alitakiwa awe amekatwa na mstari katikati kama alivyo mshika kibendera. Camera iko kulia kwa goal line. Video haijamaliza utata
una shida ya macho? hilo goli lilishadhibitishwa ni halali,Kipyanga cha mwisho kilishatoa ufafanuzi
 
Back
Top Bottom