Kukataliwa Goli la Simba dhidi ya Coastal, Azam TV Hamtutendei Haki Wateja Wenu

Kukataliwa Goli la Simba dhidi ya Coastal, Azam TV Hamtutendei Haki Wateja Wenu

Mkuu, nami naungana na wewe! Hata kingekuwepo kipande cha clip kionyeshacho huo mpira, kama ulitoka au lah, bado isingemsaidia refarii, kwani asingetumia kujiridhisha, kama wenzetu watumiao VAR!
Ingesaidia kuweka ukweli hadharani
 
Kwema Wakuu,

Najua hili litawafikia sababu JF ni Platform kubwa. Nyinyi Azam TV ndio mmepewa haki ya kuonyesha Mpira wa Ligi yetu pendwa ya NBC Premier League. Sisi Subscribers wenu tuna haki ya kupata Matangazo hayo katika ubora wa hali ya juu bila ukakasi. Yaani Sisi kwa kununua ving'amuzi vyenu automatically tunakua tumeingia makubaliano (implied contract ) kua mtatuonyesha mpira katika ubora wake.

Goli lililofungwa baada ya Kona ya Shomari Kapombe lilikataliwa kwa madai kua Mpira huo ulizungukia kwanza nje (curve) kabla kisha ukarudi ndani. Mpaka mpira unaisha Azam wameshindwa kuonyesha hiyo "Curve". Hata Watangazaji wenyewe wamebaki na kigugumizi maana hakuna Video kuthibitisha mpira uli curve nje ya mstari.

Solution hapa ilikua ni kuwepo kamera kwenye kila kona (kibendera) lakini kwa ubahili wa Azam wameshindwa kuweka. Ina maana Simba jana wangeweza kusema Refa aliwahujumu kumbe maamuzi ya Refa yalikua sahihi.

Au tuseme ingekua ndio Coastal Union wamefunga lile goli likakataliwa ingeweza kudhaniwa Simba anabebwa. Hii yote ni sababu Azam wameshindwa kuweka Kamera za kutosha Uwanjani.

Nawaza ni kiasi gani tunalipia ving'amuzi ambavyo kila kukicha vinapanda bei, na Kamera ni kiasi gani kwa kampuni kama Azam kushindwa kuweka kila pembe ya uwanja. Hii si sawa, na ni unyonyaji mkubwa tunafanyiwa.
Dah...!!! Hivi goli lile lingekubaliwa ungedai kamera!? Shida umeweka upenzi wako wa Simba mbele badala ya uhalisia.
 
Dah...!!! Hivi goli lile lingekubaliwa ungedai kamera!? Shida umeweka upenzi wako wa Simba mbele badala ya uhalisia.
Dah,
Nimeandika mahali kule juu kua nimeandika uzi huu kama Subscriber wa Azam TV, sio kama Mshabiki wa Simba. Yaani kama mlipiaji wa King'amuzi nilistahili kuona lile tukio Kwa undani wake.
 
Dah...!!! Hivi goli lile lingekubaliwa ungedai kamera!? Shida umeweka upenzi wako wa Simba mbele badala ya uhalisia.
Sema wewe ndiyo umekuja kiyanga ndiyo maana huelewi maana matukio yenye utata ni mengi na kamera zinababaisha
 
Hapa hatuzungumzi goli kukubaliwa bali uchache wa kamera huelewi nini sasa?
Sawa, mechi ngapi kamera zilikuwa kwa idadi hiyo na hakukuwa na madai hayo..!? Why specifically mechi ya Simba!? I thought reference ingekuwa michezo yote iliyokwishachezwa na AZAM kuonyesha mechi hizo. Inapokuwa reffered mechi ya Simba pekee, that means upenzi ndo umetamalaki
 
Sema wewe ndiyo umekuja kiyanga ndiyo maana huelewi maana matukio yenye utata ni mengi na kamera zinababaisha
Matukio yenye utata hayawezi kupungua kwa kyongeza idadi ya kamera.. NI UMAKINI WA MAREFA NDO UTAPUNGUZA UTATA...
 
Sawa, mechi ngapi kamera zilikuwa kwa idadi hiyo na hakukuwa na madai hayo..!? Why specifically mechi ya Simba!? I thought reference ingekuwa michezo yote iliyokwishachezwa na AZAM kuonyesha mechi hizo. Inapokuwa reffered mechi ya Simba pekee, that means upenzi ndo umetamalaki
Haya madai hayajaanza leo yapo kila leo
 
Matukio yenye utata hayawezi kupungua kwa kyongeza idadi ya kamera.. NI UMAKINI WA MAREFA NDO UTAPUNGUZA UTATA...
Hata sisi hatujasema yapungue au yaongezeke watujua wenyewe siye kama watazamaji tunataka kuona matukio yote uwanjani basi siyo mpira unapigwa ,mara unaona goli mara huelewi limepatikanaje
 
Sawa, mechi ngapi kamera zilikuwa kwa idadi hiyo na hakukuwa na madai hayo..!? Why specifically mechi ya Simba!? I thought reference ingekuwa michezo yote iliyokwishachezwa na AZAM kuonyesha mechi hizo. Inapokuwa reffered mechi ya Simba pekee, that means upenzi ndo umetamalaki
Matukio yenye utata yanayolalamikiwa ni mengi. Lakini je nalazimishwa kuangalia kila mechi ili nilete hapa matukio yenye utata? Yaani Biashara akicheza na Geita Gold jumanne labda niko kazini nalazimikaje kuleta hilo tukio hapa ?
 
Hata sisi hatujasema yapungue au yaongezeke watujua wenyewe siye kama watazamaji tunataka kuona matukio yote uwanjani basi siyo mpira unapigwa ,mara unaona goli mara huelewi limepatikanaje
Sahihi kabisa mkuu, Sisi kama Subscibers wa Azam ni haki yetu, maana vifurushi tunalipia vile.
 
Sahihi kabisa mkuu, Sisi kama Subscibera wa Azam ni haki yetu, maana vifurushi tunalipia vile.
Tatizo humu watu wanapenda sana ushabiki yanga wanaona simba ndiyo wanalalamika badala ya kuungana wote kumpush ili aweze kuboresha uchukuaji wa matukio ya mechi uwanjani
 
Tatizo humu watu wanapenda sana ushabiki yanga wanaona simba ndiyo wanalalamika badala ya kuungana wote kumpush ili aweze kuboresha uchukuaji wa matukio ya mechi uwanjani
Simba ni mara ya pili wanafunga goli la hivi likakataliwa. Kuna member mmoja kaweka video ya mechi ingine yenye tukio kama hili. Marefa au vibendera hawakomi sababu wanajua hakuna pa kuweza kupata ushahidi.
 
Kwani ile gemu Simba si alikuwa kwenye uzi mweupe, hii sio
Ndio kuonyesha kua Simba amekua akionewa Kwa hili kosa zaidi ya mara moja na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
 
Vice versa,kapombe ndo aliyesukumwa na goli likafungwa.Baadaye mchezaji wa Geita gold akakiri alimsukuma.
Malizia pia na alienda kumuomba msamaha Kapombe mara tu baada ya Refa kuliza Kipyenga kua Kapombe amechezewa faulo.
 
Hiyo ni gemu nyingine ambayo Chama (sio Kapombe) ndiye aliyepiga kona na baada (sio kabla) ya goli kuingia, utaona ndio kibendera kinainuliwa juu kwa madai hayo hayo ya mpira kutoka nje. Nadhani aliyeweka post ametoa tu tukio linalofanana na hili la juzi
Sahihi kabisa,
Haya ni matukio mawili tofauti yenye kufanana ambapo Simba wanakataliwa magoli Kwa madai kua mpira ulipita kwanza nje ukarudi ndani.

Tukio la Kwanza lingetosha kabisa kuwafanya Azam waongeze kamera uwanjani lakini imeshindikana mpaka la pili la aina hiyo hiyo limetokea tena.
 
Back
Top Bottom