Kuku kibudu aliyekufa akachinjwa ana shida gani?

Kuku kibudu aliyekufa akachinjwa ana shida gani?

Wale kinamama wanaodamka na ndoo zao kwenda vingunguti wanaenda kuuziwa nyama za ngombe ,,,wale walofia njiani ama wale waliokuwa wajawazito,,,vile vitoto hukatwa katwa na kuuzwa ! Wewe hushangai hapa mjini kuna mama ntilie wanauza mpaka supu za jero ? Nyama unawekewa kubwa kubwa mbili,,,, ! Supu ya buku unashiba kabisa ,,! Unadhani hizo nyama ndo wananunua Buchani 10k-12k per kg ? Sio kweli wananunua zile za bei rahisi!
Chanzo cha nyama inayouzwa bei rahisi au bei poa a.k.a kwa mafungu:-
1. Nyama zilizokataliwa i.e. condemned carcasses kutokana na nyama hiyo kuwa tepetevu mno imejaa maji mengi na mautelezi-malenda, imekonda kupitiliza i.e. on Borderline(cadavar). Nyama aina hii huzuiliwa ili walau inyauke.
2. Nyama zinazoamriwa kuchemshwa kwanza kabla ya kuuzwa e.g. nyama inayopatikana na kiasi kidogo cha CB (cystcercus bovis)
3. Sehemu au badhi ya Nyama/viungo zinazopatilizwa kutokana na kitu kinaitwa for aethetic reasons. e.g. utumbo wenye pimply guts nyingi, figo zenye congenital cysts nyingi au hydronephrosis n.k.
4. Nyama zilizochafuliwa (soiled meat)na uchafu au mavi ya mnyama, mchanga/udongo wakati wa uchunaji, ukataji n.k. ikiwemo milopoo
5. Nyama wanazoiba (wanachomoa au wenyewe wanaita Kusokoza) wachunaji
Hizo zote 1-5 ndo za bei poa/maelewano.
 
TUSHAKUBALIANA KATKA UKRISTO HAKUNA MAKATAZO KWENYE KULA, KIMUINGIACHO MTU SI NAJISI BALI KMTOKACHO TU
Haya ni maneno ya mafumbo usiyachukulie jumla jumla, wayahudi wana sheria ngumu sana hususan kwenye vyakula, na Yesu hakuja kuitengua Torati bali kuitimiliza, na huu mfano si kwa ajili ya vyakula bali ni matendo yetu tunayotenda ndiyo yanayotufanya kuwa najisi. Hebu pitia Marko 7:20
Akaendelea kusema, “Kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia unajisi. Maana kutoka ndani, moyoni mwa mtu, hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, uchoyo, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi na upumbavu. Maovu hayo yote yatoka ndani ya mtu, nayo humtia mtu unajisi.”
 
Siafu wameingia kwenye banda la kuku, wameua kuku kadha wa kadha...

Siruhusiwi kuwala? maana sababu ya vifo vyao inajulikana!
Kabla ya siafu ajaingia bandani uwenda kuku ana maambukizi fulani ukimchinja ile damu inapotoka kwa kasi inaondoka na vimelea vya magonjwa na ndio maana mnyama akiwa mgonjwa hata urukaji wa damu ni tofauti na mnyama mwenye Afya yake.
 
Ni sawa na kupiga risasi maiti
Utasema umemuua?
Kuku kafa sasa kuna maana gani kupitisha tena kisu shingoni?

Ili utuonyeshe waalikwa kuwa umechinja eti 😄 🤣
 
Eti wakuu kwa mfano kuku kafa na na ndani ya nusu saa akachinjwa ana shido gani kuliwa?mimi sielewi mantiki ya kuku kutoliwa baada ya kufa nachojua ili mfugo aliwe lazima AFE kwanza..
Sasa kama amekufa unachinja nini?
 
Sasa kama amekufa unachinja nini?
Yeah. Inaonekana Huyo ndg. anashindwa au hawezi kutofautisha kati ya Kuchinja na Kuchakata (Process) au kutayarisha ili aweze kuliwa kama chakula. Hapo changamoto ni Lugha ya Kiswahili.
 
Kabla ya siafu ajaingia bandani uwenda kuku ana maambukizi fulani ukimchinja ile damu inapotoka kwa kasi inaondoka na vimelea vya magonjwa na ndio maana mnyama akiwa mgonjwa hata urukaji wa damu ni tofauti na mnyama mwenye Afya yake.
Mmmmh. Ukienda kwa mtizamo huo; basi hutokaa ule chochote kwani hakuna kitu chochote (sio vyakula tuu bali hata hewa unayovuta wamejaa tele) kisichokuwa na vimelea (microbes) i.e. Fungi, Protozoa, Bacteria na Viruses.
Hoja mtambuka ni Je, ni wenye kuleta madhara kwa mtumiaji??? Kumbuka wengine ni muhimu sana wawepo ili maisha yako na yangu yaendelee i.e. wanafaida/manufaa makubwa katika mustakabali wa Uhai wetu wanadamu na viumbe vingine hapa duniani. Mungu muumbaji ni fundi sana. Tunamshangaa na hatumwelewi na hatutakaa tumwelewe.
 
kufa na kuchinjwa ni vitu viwili tofauti.kuchinjwa ni kitendo cha mnyama/ndege kufa kwa njia halali Ila kufa kibudi ni kitendo cha mnyama/ndege kufa pasipo halali kuliwa na binadamu(hasa kwenye Imani za dini)
 
Sina utaalamu lkn naona kuna haja ya mnyama kumwaga damu yake kabla kumuandaa kwa mapishi.
Sina uhakika lkn nawaza tu, bila kumwagika damu mnyama jee huwa hana madhara? Nahisi kuna umuhimu kwa mwili wa mnyama kuupunguza damu kabla ya kumuandaa kwa mapishi
 
Back
Top Bottom