Huyo mheshimiwa ametafsiri kuchinja kuwa ni ile kazi ya kumnyonyoa huyo kuku mfu, kumpasua, kuondoa utumbo na kumkatakata vipande ili aweze kupikwa au kuandaliwa kama chakula. Hatua hizo ni mchakato yan anamchakata (Process) kuku mfu.Ni sawa na kupiga risasi maiti
Utasema umemuua?
Kuku kafa sasa kuna maana gani kupitisha tena kisu shingoni?
Ili utuonyeshe waalikwa kuwa umechinja eti 😄 🤣
sawa na wataalamu wa afya wanasema mnyama/ndege kuchinjwa kunasaidia kuondoa bacteria mbalimbali ambao wanaweza kusababisha madhara kwa binadamu.Fikiria mnyama/amekufa kwa kula sumu akifa kibudu bila ya kunjinjwa maana yake ni kwamba sumu isalia mwilini mwa mnyama na kumletea madhara mlajiSina utaalamu lkn naona kuna haja ya mnyama kumwaga damu yake kabla kumuandaa kwa mapishi.
Sina uhakika lkn nawaza tu, bila kumwagika damu mnyama jee huwa hana madhara? Nahisi kuna umuhimu kwa mwili wa mnyama kuupunguza damu kabla ya kumuandaa kwa mapishi
Hakuna madhara yoyote kiafya kumla mnyama ambaye damu yake haijamwagika kama chakula. Wale Jamaa wengine hula "kisusio".Sina utaalamu lkn naona kuna haja ya mnyama kumwaga damu yake kabla kumuandaa kwa mapishi.
Sina uhakika lkn nawaza tu, bila kumwagika damu mnyama jee huwa hana madhara? Nahisi kuna umuhimu kwa mwili wa mnyama kuupunguza damu kabla ya kumuandaa kwa mapishi
Ni sahihi kabisa na wapo watu waliowahi kuathirika (hata kufa) kwa ulaji huo.sawa na wataalamu wa afya wanasema mnyama/ndege kuchinjwa kunasaidia kuondoa bacteria mbalimbali ambao wanaweza kusababisha madhara kwa binadamu.Fikiria mnyama/amekufa kwa kula sumu akifa kibudu bila ya kunjinjwa maana yake ni kwamba sumu isalia mwilini mwa mnyama na kumletea madhara mlaji
Kama amekufa kwa maradhi hatari ukimla unamsindikiza chapEti wakuu kwa mfano kuku kafa na na ndani ya nusu saa akachinjwa ana shido gani kuliwa?mimi sielewi mantiki ya kuku kutoliwa baada ya kufa nachojua ili mfugo aliwe lazima AFE kwanza..
sio kweli kula nyama ambayo haijachinjwa kuna madhara makubwa kiafya, Nimetoa mfano mnyama ambaye amekula sumu Kama asiponjinjwq ile sumu itaenea mwili mzima wa mnyama na hii itapelekea mlaji kupata madhara makubwaHakuna madhara yoyote kiafya kumla mnyama ambaye damu yake haijamwagika kama chakula. Wale Jamaa wengine hula "kisusio".
Ni kweli inafaa kuupunguza mwili wa mnyama damu kama atatumika kama chakula kwa sababu damu ikivia ndani ya mwili; mwili huo(Nyama) huharibika mapema sana, muonekano wa nyama hauvutii walaji inakuwa nyekundu mno na ladha yaweza kubadilika kwa kiasi fulani kwani virutubisho(Nutrients) na takamwili (metabolic Waste products)vilivyokwenye mzunguko wa damu hubaki kwenye nyama. Ila usiogope we twanga/kula kama huna kinyaa.
Waaaaapi. Nani kakudanganya mkuu? Huku Umasaini ndani-ndani huku 98% ya nyama tunazokula ni vibudu kwa mujibu wa mtizamo wa nyie Waswahili.Sio tu kidini.hata kiubinadamu HAIFAI.
Kwa mtizamo wako huo; basi elewa fika kwamba kuchinja sio kigezo cha kuondoa sumu mwilini. Kwa mfano mnyama aliyekufa kutokana na kula sumu ya panya (zinc sulphide) hata ukimchinja halafu ukajichanganya eti umemchinja na ukala hiyo nyama; basi na wewe ni bye bye. Ndo mana wadau hapo juu walisema kama ukijua kisababishi cha kifo na ukaridhika hakuna madhara, waweza kula. Mnyama aliyekufa kwa kugongwa na nyoka ukila hata bila kumchinja huyo mnyama hakuna madhara. Umeona hizo tofauti? Pote kisababishi cha kifo ni sumu na pote mnyama hakuchinjwa i.e. damu haikumwagwa.sio kweli kula nyama ambayo haijachinjwa kuna madhara makubwa kiafya, Nimetoa mfano mnyama ambaye amekula sumu Kama asiponjinjwq ile sumu itaenea mwili mzima wa mnyama na hii itapelekea mlaji kupata madhara makubwa
The hidden truthWafugaji hatuchinji mnyama alie na afya njema, tunawala wale choka mbaya, katibiwa kwa tiba zote zimegonga mwamba basi huyo anachonjwa tu, hata akifa mwenyew bado anakua hajakwepa kuliwa ataliwa tu.
Hii kwa anaejari afyake, wala aihitaji watu wa imani fulani kujibu.Kina bwashee wanakuja
Na ndio maana kuna namna ya kuandaa nyama na sisi waislam tumeelekezwa kabla ya kula tuseme Bismillah.Mmmmh. Ukienda kwa mtizamo huo; basi hutokaa ule chochote kwani hakuna kitu chochote (sio vyakula tuu bali hata hewa unayovuta wamejaa tele) kisichokuwa na vimelea (microbes) i.e. Fungi, Protozoa, Bacteria na Viruses.
Hoja mtambuka ni Je, ni wenye kuleta madhara kwa mtumiaji??? Kumbuka wengine ni muhimu sana wawepo ili maisha yako na yangu yaendelee i.e. wanafaida/manufaa makubwa katika mustakabali wa Uhai wetu wanadamu na viumbe vingine hapa duniani. Mungu muumbaji ni fundi sana. Tunamshangaa na hatumwelewi na hatutakaa tumwelewe.
Nyie kuleni tu.ila ina madhara hyo nyamaWaaaaapi. Nani kakudanganya mkuu? Huku Umasaini ndani-ndani huku 98% ya nyama tunazokula ni vibudu kwa mujibu wa mtizamo wa nyie Waswahili.
Upo porin unawinda na mishaleKuchinjwa ni Kabla ya kufa,. Sio afe ndo achinjwe. Ni vile ninavyoamini Mimi. Kama kashakufa ni haramu na mwenyezimungu anajua zaidi.
Jamaa anatafuta namna ya kujihalalishia kula vibudu!Mfu hafi tena.. Au hauliwi tena.. Kitendo cha kuchinja tafsiri yake ni kuua.. Ni kutoa uhai.. Kibudu kimeshakufa sasa unakichinja tena ili iweje😂