Kulikoni Kanisa Katoliki kukosa uwakilishi Mkutano wa Rais Samia na Viongozi wa dini?

Hata sisi wabaniani tumekosa mwakilishi, nasikia hata zumaridi hakuwa na mwakilishi
 
Hili hasa ndiyo jibu. Na nyongeza yake ni kwamba katika Kanisa Katoliki Askofu ana uwezo wa kukasimu mamlaka na madaraka yake kwa Padri yoyote na inakuwa kwamba ni Askofu amefanya au ni Kanisa limefanya. Kwa mfano, kwa kanuni ya kanisa ile sakramenti ya kipaimara hutolewa na Askofu, lakini pia Askofu anaweza kutoa idhini kwa Padri mwingine ku-administer sakramenti hiyo. Hali kadhalika kwa mambo mengine ya utawala, likiwemo hilo lililotajwa kwenye huu uzi.
 
Askofu ni Padre pia.

Padre Ni Mwakilishi Wa Yesu Kristo.

Padre Ni Zaidi ya Mufti na hao viongozi wengine.
 
Pumba hizo.

Kanisa katoliki syo taasisi inayojipendekeza, hata enzi za mwendazake hawakuwahi kuhudhuria ktk vikao viwe kuapisha au makanikia
Umezunguma kinyume,tangu dikteta wa Italia awahonge Vatican na maruzuku na misamaha ya Kodi,katoliki imekua ikipenda kujikurubisha na siasa
 
Rais aliyeko madarakani sio wa dhehebu lao
 
Tusitumie maneno ya kuchochea chuki, pengine zipo sababu za msingi Kanisa mama kukosekana hapo na Mh Rais anajua.

Majuzi tu ametoka kwenye jubilee ya miaka 25 ya uaskofu huko Ngara tena kwa Askofu mtata mtata.
 
Labda hawakualikwa
 
Nafikiri Mkutano ulikuwa umepangwa siku mbaya - Jumatano ya Majivu, siku muhimu sana kwa Wakatoliki. Je mpangaji hakujua au alipitiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…