Kulikoni? Msafara wa Rais Samia kuwa na magari yote haya, pia ulinzi wake umeongezeka maradufu

Kulikoni? Msafara wa Rais Samia kuwa na magari yote haya, pia ulinzi wake umeongezeka maradufu

View attachment 1977510Wale walioko Arusha na viunga vyake leo tumeshuhudia/kuona Mh. Raisi mama Samia Suluhu Hassan kaongezewa ulinzi mara dufu, tofouti na tulivyozoea na msafara wake umekuwa na ulinzi mkali na idadi kubwa ya askari na usalama wa taifa kitengo cha ulinzi.

Pia msafara wake una magari zaidi ya 70 kutoka 20 ya awali kama tulivyokwisha zoea, msafara huu umeambatana na helikopta mbili kama tulivyokuwa tukiona enzi za Hayati John Pombe Magufuli.

Cha kushangaza amekuwa akisisitiza kauli kama ile ya Hayati John Pombe Magufuli ya kwamba “aombewe”, kulikoni?

Je, hii misafara mikubwa sio janja janja ya baadhi ya watumishi wakubwa kujilipa posho kubwa kubwa ilihali, wananchi wanalia maisha magumu katika awamu hii ya sita?

Tujadili.
Safi sana Rais wetu analindwa aisee, ngoja na mimi nijitafutie ulinzi wa Mungu wanitosha
 
Back
Top Bottom