Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

Naaam, eti hata rais wa nchi anavunja sheria live! Kwanini sheria hii walishindwa kubadili kwa hati ya dharula?

Hii inatokana na mtawala kutokuwa na weledi sababu ya kuamini kutawala kwa kupiga ramli na matunguli!!
 
Umenena sawia kabisa.Ila ningeshauri swala hili pia lifikishwe ICC.Vita ya kuisaka ikulu ni kali kwa hiyo ni lazima kusimama ikulu.
ndio raha ya kua na viongozi watetezi na majasiri..
LAKINI
tatizo liko palepale
kesi ya ngedere kumpelekea nyani !!
 
Umenena sawia kabisa.Ila ningeshauri swala hili pia lifikishwe ICC.Vita ya kuisaka ikulu ni kali kwa hiyo ni lazima kusimama ikulu.
Hivi mnataka yatokee MAUAJI ya kina nani ili CCM Wapelekwe ICC??Je, na watoto wa kina Freeman Mbowe,Philemon Ndessapessa,Reginard Mengi,Edward Lowassa,Rostam Aziz na James Mbatia Watakuwepo?????!!Duniani hakuna HAKI DUNIANI.Unauawa na wanapelekwa ICC Wanashinda KESI unawaacha kina MBOWE Wanakula BATA huku wazazi wako wakiteseka.Uhuru Kenyata yupo HURU.
 
NEC na Kikwete sijui wanabanwa na nini sisi kukaa mita200. Hivi mtangaza matokeo atamtangazia nani sote tukiondoka?

Hiyo nguvu anayoisema JK ya kuwashughulikia wakaidi wa amri batili kwa nini asitumie kuwalinda wasilete fujo?
 
Tayari wakili jembe na nguli Peter Kibatala akiambatana na wanasheria nguli wa Ukawa Prof Safari, Mallya na Tundu Lissu asubuhi ya leo amefungua kesi mahakama kuu kuishitaki NEC kwa ukiukwaji wa sheria juu ya wananchi kukaa mita mia mbili na kulinda kura.

Kesi imefunguliwa under certificate of urgency nadhani kama sijakosea kwa kiswahili ni 'hati ya dharura' ili isikilizwe na tafsiri itoke kabla ya uchaguzi.Tayari jalada lishapelekwa kwa pilato na wanasheria nguli wa Ukawa wamejipanga kwa hoja za nguvu na ushahidi wa kutosha.

Pia jopo la wanasheria nguli wa UKAWA wameiomba mahakama kuu ya Tanzania kutoa tafsiri ya kisheria juu ya matamshi ya rais wa nchi kuwa alitumia mamlaka gani kuvaa kazi za tume.

Atatangazwa rais aliyeshindwa.
 
Je kama mahali hapo ni puplic road inakuwaje. .

Ukae kwenye public road??? Ukikaa kwenye public road ina maana umefunga bara bara wakati inatakiwa kuwa wazi ili kuwezesha FFU na defender zao wapite kwa uhuru na watumiaji wengine wa barabara waitumie kwa uhuru.

Kukaa kwenye public road ni kujitangazia kiyama wewe mwenyewe mkaaji sababu polisi watakuja na mabomu na virungu kuvurumisha waliofunga baraba kwa kukaa ili kuhakikisha wanaifungua ili watumiaji wengine wa bara bara waendelee kuitumia.
 
Usichokijua ni kuwa sheria ya Uchaguzi inasema siku ya kupiga kura hakutakuwa na mikusanyiko ya kisiasa.Mikusanyiko yote ya kisiasa mwisho wake ni siku ya mwisho wa kampeni ambayo ni tarehe 24 octoba 2015.Ukikusanya watu wako siku hiyo ya uchaguzi wawe wana UKAWA au CCM wakajikusanya mahali ni kosa kisheria.

Pili kwa mujibu wa sheria zinazohusu mikusanyiko ni lazima kutoa taarifa polisi kuwa kutakuwa na mkusanyiko mahali fulani na kwa lengo gani. Hivyo kama kurtakuwa na watu wenye lengo la kukusanyika popote inabidi wawasilishe maombi yao polisi wakijieleza wao ni akina nani ili wapewe ulinzi wa polisi

Tatu kuna sheria ya ardhi.Unaposema utakusanyika hapo kwenye mita 200 hilo eneo ni mali ya baba yako au mama yako? Huyo mwenye miliki ya hiyo ardhi karidhia? Hivyo kama kuna watu watakaotaka kukusanyika ni lazima wapeleke kibali cha mwenye eneo kuwa karidhia eneo lake litumike kwa mikusanyiko.Na kwamba mikusanyiko hiyo haitakuwa kero wala bugudha kwa wakazi wa eneo husika,majirani n.k Maana kama watu watajiamulia kukusanyika hiyo mita mia 200 bila mwenye eneo lake kuridhia ina maana ni uvamizi wa ardhi ya mtu bila ridhaa yake.Na huo ni uvunjifu wa amani kwenye eneo la watu.Hivyo Mahakama lazima iangalie maslahi ya wenye maeneo maeneo yao yasije vamiwa SIKU YA KUPIGA KURA NA KUKALIWA KWA MABAVU na hao wanaojiita walinda kura.

Polisi kwa kuliona hilo kuwa kutakuwa na uvunjaji sheria kwa watu kuvamia maeneo ya watu na kujikusanya wakasema kila mtu aende kwake asubirie kwake.Sababu vituo vya kupigia kura haviko mbali na makazi ya watu.Kwa nini watu wakae kwenye viwanja vya watu? Mahakama iliangalie hilo

Kwangu sikubali mtu akusanyike WALA KUWEKA MAKALIO YAKE KWENYE ENEO LANGU NITAITA DEFENDER NA GARTI LA WASHA WASHA HARAKA WAJE NA MABOMU NA VIRUNGU WAONDOE WAVAMIZI KWENYE ENEO LANGU.

Hawa akina KIBATALA wanataka kuleta vurugu na ugomvi kati ya wenye maeneo na hao watu anaotaka wakusanyike hizo mita mia mbili sababu sio kwao ni kwa watu.

Eti bila haya lowasa na mbowe wanatoa amri mkimaliza kura kaeni mita 200.Hilo eneo wanaloamrisha watu wakae ni la baba yake au mama yake lowasa au mbowe.Sheria ya ardhi iheshimiwe majaji msimamie hilo kwa maslahi ya wenye maeneo yao.Mkiwakubalia mnawaweka wenye maeneo matatizoni.

Sheria haitenguliwi kwa amri.
Waliotunga sheria hawakujua kuwa hizi mita ziko ardhini?
 
Sheria haitenguliwi kwa amri.
Waliotunga sheria hawakujua kuwa hizi mita ziko ardhini?

Sheria ukiisoma lazima usome na sheria zingine.Sheria nyingi hazisimami peke yake.Kwa mfano kama kuna sheria ina sema mtanzania yuko huru kwenda popote.Usije ukasema inasema naweza kwenda popote ikiwemo msikitini mfano wewe ni mkristo ukaenda msikitini na viatu sababu kuna sheria inasema ruksa kwenda popote.Inabidi ujue na sheria zingine KUWA SALAMA.
 
Hivi ndo inavyotakiwa kuwa hata kwa mambo ya chama.. Kuna Prof.mmoja kule Zimbabwe anawaendesha sana wanasiasa wakanyaga sheria. Kila kitu kinapofanywa kinyume hata kama ni cha kichama yeye anafungua kesi mahakamani na mara zote hushinda.

Mathalani issue ya EL kwa ccm ilikuwa ni kufungua shauri mahakamani , kwanza unazui uchaguzi kuendelea pia unaombwa kusikilizwa na mahakama kutengua maamuzi yote. wakigoma kuwa hayo ni mambo yao na sisi tuwanyime ruzuku kwani zinatoka kwa walipa kodi wengine hawana vyama
 
Huu Uchaguzi mpaka kujakumalizika Wapo Watakao kufa kwa Mshtuko wa Moyo
 
Friday, October 16, 2015

Leo tarehe 16 October 2015, Ukawa kupitia wakili wa CHADEMA,Peter Kibatala na mawakili wengine, wamefungua chini ya hati ya haraka sana (certificate of extreme urgency) shauri nambari 37 la mwaka 2015 katika Mahakama Kuu ya Tanzania (Main Registry) wakiomba Mahakama Kuu itoe tafsiri sahihi ya kifungu cha 104 (1) cha Sheria ya Uchaguzi Tanzania na itamke iwapo wapiga kura na watu wengine wenye shauku wanaruhusiwa au la kukaa KWA UTULIVU umbali unaozidi meter 200 kutoka kituo cha kupigia kura/kufanya majumuisho ya kura.

Pia wameiomba Mahakama Kuu itamke iwapo ni halali kwa Rais wa nchi kutoa matamko aliyoyatoa kwa namna ya katazo kwa wapiga kura/raia wenye shauku kukaa KWA UTULIVU umbali unaozidi mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura/kufanya majumuisho.

Pia wameiomba Mahakama Kuu itamke iwapo Rais ana mamlaka hayo kisheria kwa kuzingatia Sheria ya Uchaguzi Tanzania.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa Wakili Peter Kibatala ambaye ameshare nasi kwenye ukurasa wake wa facebook
 
MACCM mwaka wa kufa nyani hakuna namna nyingine ni lazima wapigwa tu,maana hakuna namna nyingine kama watu hawasikii watafanyanywe?ndio hakuna namna nyingine lazima wapigwe tu
 
Good idea UKAWA inatwanga kotekote bao la mkono mwisho chooni/bafuni kwa FISIEMU
 
Back
Top Bottom