Kumbe BongoFleva inalipa!! Diamond Platnumz anaingiza Milioni 200 kwa mwezi kwa matangazo tu

Kumbe BongoFleva inalipa!! Diamond Platnumz anaingiza Milioni 200 kwa mwezi kwa matangazo tu

Juzi kasema ukipata view one million YouTube bas unapata around 900K up to 1000K , video ya waah ina view 37Mil , IT wao karopoka imeingiza 90 Mil mpak sasa , jamaa wamekaa kiongo ongo sana
Propaganda zingine hata kwenye siasa huzikuti ila WCB zimejaa tele
 
We una amini hajajenga? Vii kuhusu madale? Hotel aliyonunua? Nk
Imani huwa ni kazi bure, kama amejenga ukaamini hajajenga, imani yako haimfanyi kuwa hajajenga. Kama hajajenga ukaamini amejenga, imani yako haimfanyi kuwa na nyumba 5.

Diamond haingizi iyo hela kwa mwezi kama endorsement za matangazo tu. Tusidanganyane,hukujifunza kitu kwenye diamond karanga?
 
Msanii wa Bongofleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz amesema kila mwezi huingiza Sh200 milioni kutokana na kuingia mikataba na kampuni mbalimbali kuwa balozi wa bidhaa zao.

Akizungumza katika kipindi cha TheSwitch kinachorushwa na redio ya Wasafi leo Alhamisi Januari 28, 2021, Diamond amesema fedha hizo ni mbali na zile anazoingiza kupitia muziki.

Amebainisha kuwa anaingia mikataba na kampuni na amekuwa akifanya hivyo kwa kila kampuni inayohitaji huduma yake.

“Endosment zangu mimi mshahara wangu kwa mwezi si chini ya milioni 200, na tunasaini mikataba kila siku. Ninaingiza kwa wiki Sh55 milioni kwa siku Sh7 milioni kwa saa moja Sh300,000 na kwa sekunde Sh6,000.”

Amesema mwaka 2021 fedha anazozipata katika eneo hilo huenda zikaongezeka kwa kuwa anatarajia kuwa balozi wa vitu vingi zaidi kwa kuwa ameamua kufanya muziki kuwa kazi na biashara.

View attachment 1689019
=====

Ina maana hii ni kwa endorsement za matangazo tu
Yupo wapi Mr Nice na Q-Chief
 
Mkwe wangu alistaafu mwaka jana na alikua senior officer serikalini akaramba mafao ya mil 500
Hii ni sawa na miezi miwili tu ya huyu chizi
Kweli maisha hayajawahi kuwa fair
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Wote tunaishi lakini vitu vingine sio mpaka muweke ligi, rizika na unachopata
 
Mzik bongo unalipa ukiufanya biashara
Ukiufanya ki local local sahau huoni kingkiba anakua kama amestuck, Diamond anavuka boda sana mtu anafanya corabo hadi na Alicia keys, juzi juzi tu hapa nasikia kuna nyimbo yake inataka kuingizwa kwenye come into america part2 sio mchezo diamond ni kiboko
 
Akili za kimasikini hizi,kwahiyo mnabishana na ukweli,Mnashangaa mil200 kwa mwezi?wakati kuna watu wanaingiza mil500 kwa wiki tuu.
 
Hapo sawa, hawakawiii kufungua kesi ya uhujumu uchumi
Huyo ni kada mtiifu hawezi kushtakiwa kizembe we subiri uone sakata la tv ya wasafi kufungiwa litakavyoyeyuka kiaina soon utawaona hewani
 
Huyu huyu ambaye nyumba anayoishi / amepanga, mwenyewe kaamua kuiweka sokoni huku mpangaji akiwa ndani?
Jamani.. ile nyumba unayotangazwa kuUzwa zaidi ya mwaka siyo anayoishi Daimond.

Kingine Hiyo nyumba Daimond halipi Kodi kwa hela yake. Moja ya kampuni anayofanya nayo matangazo kwenye mkataba walikuwa na makubaliano hayo.

Ikumbukwe kuwa na thamani za ndani waliweka GSM.
 
Mkuu kweli wewe haujui kitu ,una uhakika magari ni yake? Hivi unawajua wasaniii kweli wewe? Achana na tantalila za wasanii.
Yale Magari ni ya kwake. Kuna kampuni anakatia Insurance naijua kadi za gari zina umiliki wa kwake.

Dai kuna wakati huwa ananikasirisha ila kwenye hili nimtetee tu.
 
Hahaa atimize ahadi ya rozi rozi naona tangia 2016 ipo kwenye maji,kisha ajenge mansion lake aache kupanga!!
Nyumba ile hajapanga.. Na inayotangazwa kuuzwa siyo anayokaa Dai..

Nyumba anayoishi analipiwa kila kitu na Moja ya Kampuni anayoifanyia matangazo..ilikuwa moja ya offer aliyopewa.

Yule hadi mafuta ya gari zake analipiwa.
 
Mwenye pesa hana tantalila au longo longo ,Mwenye pesa unaona tu actions zake! Tunachosema hapa ni kuwa huyo bwana mdogo kutufanya sie mapoyoyo na uongo uongo wake,kama pesa anazo atulie ni zake sio kupayuka payuka tu anaingiza sijui mili 220 kwa mwezi,hivi anajua mili 200 kwa mwezi?
Sasa wewe maskini ndio maana unaona ajabu, hizo hela hujawahi ht ziota then mwenzio anakunja kwa mwezi basi povu linakutoka hatari
 
Zari, babutale, yule msomali salah na esma, jumachoko, mamaake na basha wake wanachukua ngapi hapo kabla ya kodi.
Huku kuna romio sijui alafu na huyu kakaake wa juzi sijui Nyange takataka gani sijui
 
Back
Top Bottom