baba-mwajuma
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 4,178
- 7,591
Nilishauri kitu hiki hiki Mkataba uwe kwa Target, wakiongeza mapato unaendelea, wakishindwa kufikia target unavunjika.Jamani kuna hakika gani mapato yataongezeka hawa jamaa wakapokuja? Sasa hawa jamaa wanawekeza alafu inakuwaje tunagawana faida au tunawalipa kama waajiriwa? Kama kweli wataongeza faida maradufu ya sasa mkataba wetu uweke malengo na yasipofikiwa basi hao ndugu wasilipwe. Hata hivyo huu mkataba mara nasikia ni uwekezaji mara ununuzi mara uendeshaji sasa ni lipi? Kuna mikataba ya aina nyingi duniani inayolenga kuleta ufanisi na kuongeza mapato; kuna management contract, Franchise, share holding, joint venture, Outsourcing, sub contracting, rent option au co Branding. Wataalamu wetu waseme bila kificho mkataba wetu ni wa aina gani? Mimi nashauri kwamba kama shida yetu ni vifaa vya kazi basi tununue hivyo vifaa alafu tuwaajiri hao waarabu wataalamu tuwalipe mshahara, bandari na vitendea kazi vibaki kuwa mali yetu.
Mapato wanaendelea kukusanya Tra na wenzake wao wanakua upande wa Bandari, kama umewahi kutoa Container Kuna Gharama za Tra kama Vat na Duty na Kuna Harama za Bandari kama Handling fees, storage etc. Hizo Gharama za Bandari ndo wao wanapata hapo, sijajua ubia wataingia vipi na watagawana vipi.