KUMBUKIZI: Mada maalum ya kumuenzi Munga Tehnan na kazi zake

KUMBUKIZI: Mada maalum ya kumuenzi Munga Tehnan na kazi zake

Katika mtanadao wa Wikidepia Free Encyclopedia neno Falsafa (Kigiriki φιλοσοφία filosofía = upendo wa hekima) ni jaribio la kuelewa na kueleza ulimwengu kwa kutumia akili inayofuata njia ya mantiki.
Falsafa huchunguza mambo kama kuweko na kutokuweko, ukweli, ujuzi, uzuri, mema na mabaya, lugha, haki na mengine yoyote.
Tofauti na dini, imani au itikadi njia ya falsafa ni mantiki inayoeleza hatua zake ikiwa tayari kuchungulia upya kila hatua iliyochukua. Kwa hiyo falsafa ni njia ya maswali.
Katika lugha ya kila siku neno "falsafa" mara nyingi linachukuliwa kutaja jumla ya mafundisho au imani ya mtu au kundi la watu kwa mfano "falsafa ya chama fulani", "falsafa ya maisha yangu" na kadhalika. Lakini kwa jumla fikra hizo hazistahili kuitwa "falsafa". Ila tu kuna makundi ya wanafalsafa wanaopendelea mielekeo tofauti na kuhusu haya inawezekana kutumia neno "falsafa ya fulani" kwa kutaja matokeo ya kazi yao.
Vipi katika kupatia na kukosea katika misingi ya Falsafa ? Namaanisha Falsafs na Mantiki nayo unaipimaje kama imepatia au kukosea, sababu inaonekana msingi wao mkuu Elimu hizi ni AKILI.
 
Ahsante kwa kunirekebisha.Ila waislam ninachowapendea kwenye kuzika hawana mbwembwe na complications nyingi mfano kusakafia kwa marumaru,matarumbeta,maua,kuzikwa na pesa na magari kaburini.mtu anazikwa anagusa udogo moja kwa moja japo anazikwa na sanda.Hata kuiweka maiti muda mrefu hata mwezi na kuiangalia angalia muda wote hii kitu hakuna.
Raisi Sani Abacha wa Nigeria alifariki hakutangazwa ila walitangaza redioni tayari akiwa ameshazikwa i like this kwa kweli
Jurjani unasemaje hapo nirekebishe kama nimekosea kitu au ongezea
Ulichosema ni sahihi kabisa, katika vitu vinavyotakiwa kuwahishwa ni kuzika. Wapo watu walikufa saa kumi na mbili jioni akazikwa saa mbili usiku. Alimuhimu hakuna haja ya kuchelewesha maiti zaidi ya kujipa gharama na kupoteza muda.

Tuko pamoja.
 
Kuna kipindi lilikuwa na mgogoro sijui ni mipaka au ninini..likapigwa X..kama bado lipo tunaweza kujipanga upya[emoji848][emoji848]
Kuna Bro mmoja kitaa alikuwa analipenda sana gazeti la JITAMBUE nikawa na muona mtu wa ajabu sana. Mada zake nilikuwa sizielewi kabisa.
 
Uzi maalumu kwa watu maalamu,hasa sisi wa kipindi kile ambapo kusoma makala haikuwa shida.
 
Vipi katika kupatia na kukosea katika misingi ya Falsafa ? Namaanisha Falsafs na Mantiki nayo unaipimaje kama imepatia au kukosea, sababu inaonekana msingi wao mkuu Elimu hizi ni AKILI.
Falsafa ni wazo, halafu mantiki ndio inazaa dhana....sasa dhana inaweza kuwa dhanifu ama halisi
Shule na elimu zetu vina ukomo, na ukomo wake unaishia kwenye mantiki ya dhana halisi , hivyo huwa vigumu kumtoa mtu kutoka dhana halisi kumpeleka dhanifu..na hapa ndio tatizo la kimantiki linapoanzia
Wenzetu wamewekeza kwenye falsafa kama msingi wa mfumo mzima wa dhana dhanifu ama dhana maizi na kutoka hapo ndio hutohoa michakato yote na kuihuisha na dhana halisi
Na kwenye hilo la kuhuisha wameipa falsafa makundi mbalimbali..kwa maana ya kwamba.. Msingi wake ni mmoja lakini wenye matawi mengi
 
Kuna Bro mmoja kitaa alikuwa analipenda sana gazeti la JITAMBUE nikawa na muona mtu wa ajabu sana. Mada zake nilikuwa sizielewi kabisa.
Hii ndio elimu ya utambuzi...kuongea ama kuandika vitu beyond normal thinking ya binadamu wengine
 
Kweli dunia ni jumba. Natamani wengi tungelijua na kulithamini hili, labda maisha yetu na watu wetu yangekuwa yamepiga hatua.
 
Hii ndio elimu ya utambuzi...kuongea ama kuandika vitu beyond normal thinking ya binadamu wengine
Shida katika Falsafa na Mantiki ni kuufikia ukweli kama ulivyo. Kama elimu haikusaidii kuufikia Ukweli ujue ina shida.

Kufikiri kuliko tukuka kunataka msaada wa njia madhubuti zaidi ya akili(Falsafa na Mantiki) pekee.
 
Late 90's to early 2000
moja ya mtu mahiri munga tehnanan mungu kutokea kwa sisi tuliobahatika kupata nakala zake na kuhudhuri kongamano zake hakika tunamkumbuka kila siku hadi sasa hakuna aliyeweza kuandika nakala za munga!
rest in peace munga.....
 
nashukuru sana kaka watu kama nyinyi mnatambua uwepo wa gwiji huyu wa elimu ya utambuzi....
moja ya mtu mahiri munga tehnanan mungu kutokea kwa sisi tuliobahatika kupata nakala zake na kuhudhuri kongamano zake hakika tunamkumbuka kila siku hadi sasa hakuna aliyeweza kuandika nakala za munga!
rest in peace munga.....
 
Ukiweka ahadi lazima uitimize..Ukiweka nadhiri ni lazima uitangue la sivyo itakutesa kifikra na kudai utanguzi.

Mwaka wa jana kwenye post moja, tukiwa na mjadala, tulimjadili gwiji wa falsafa maizi Hayati Munga Tehnan na nikaahidi kuna na mada maalum kwa ajili yake kumuenzi. Naomba sasa nitangue nadhiri na ahadi yangu hii kupitia mada hii.

Kwa wengi wasiomfahamu ndio alikuwa Mmiliki wa gazeti la utambuzi liitwalo JITAMBUE na MSHAURI. Humo ndani kulijaa madini tupu ya falsafa kindakindaki, saikolijia, mambo ya kiroho kijamii hata utani na simulizi za kufurahisha sana.

Mimi ni mmoja wa shabiki na mwanafunzi wake mkubwa... Wengine ninaoweza kuwakumbuka kwa haraka ni pasco na Mtambuzi ..Natambua list ni ndefu na kila mmoja atakuja na mchango wake

Uzi utakuwa updated kutokana na kadiri maudhui yatakavyokuwa yanapatikana ili hatimaye tuwe na mada iliyoshiba kumhusu Munga Tehnan.

Naamini kati yetu kuna wanaojua historia yake, maana mtandaoni haupatikani.

Ombi kwa Moderator Kama kuna uwezekano wa kuziweka mada zake pamoja kwenye mada moja kuu, zile zenye maudhui ya kufanana.

Ombi kwa wana JF kama kuna mwenye hard copy ya kazi zake kupitia JITAMBUE pls share.
Binafsi kazi zake zimenisaidia sana kujitambua japo sikumfahamu mapema , sikuwahi kosa gazeti la Jitambue au mshauri nikipata muda nitaangalia nilikoficha baadhi, wengine niliwapa wakasome kwa kutojua thamani ya kilicho ndani waliyateketeza na nilipoyahitaji viswahili vikawa vingi. leo hii kila nikishauri lazima nizungumzie umuhumu wa KUJITAMBUA.
 
Dah! Munga Tehnan alikuwa mwalimu/ mentor wangu. Mshana Jr inawezekana tulikuwa darasa moja na tunafahamiana kupitia mtu huyu maana kuna wakati unatoa mada ambazo nahisi kama ulikuwa akilini mwangu.

Huwezi kuamini lile gazeti la Jitambue alikuwa anaandika peke yake (kwa majina tofauti na angle tofauti) kuanzia page 1 hadi page ya mwisho...
 
Ukiweka ahadi lazima uitimize..Ukiweka nadhiri ni lazima uitangue la sivyo itakutesa kifikra na kudai utanguzi.

Mwaka wa jana kwenye post moja, tukiwa na mjadala, tulimjadili gwiji wa falsafa maizi Hayati Munga Tehnan na nikaahidi kuna na mada maalum kwa ajili yake kumuenzi. Naomba sasa nitangue nadhiri na ahadi yangu hii kupitia mada hii.

Kwa wengi wasiomfahamu ndio alikuwa Mmiliki wa gazeti la utambuzi liitwalo JITAMBUE na MSHAURI. Humo ndani kulijaa madini tupu ya falsafa kindakindaki, saikolijia, mambo ya kiroho kijamii hata utani na simulizi za kufurahisha sana.

Mimi ni mmoja wa shabiki na mwanafunzi wake mkubwa... Wengine ninaoweza kuwakumbuka kwa haraka ni pasco na Mtambuzi ..Natambua list ni ndefu na kila mmoja atakuja na mchango wake

Uzi utakuwa updated kutokana na kadiri maudhui yatakavyokuwa yanapatikana ili hatimaye tuwe na mada iliyoshiba kumhusu Munga Tehnan.

Naamini kati yetu kuna wanaojua historia yake, maana mtandaoni haupatikani.

Ombi kwa Moderator Kama kuna uwezekano wa kuziweka mada zake pamoja kwenye mada moja kuu, zile zenye maudhui ya kufanana.

Ombi kwa wana JF kama kuna mwenye hard copy ya kazi zake kupitia JITAMBUE pls share.
Kipindi hiko nilikuwa na msichana nikiwa chuo yeye alikuwa secondary kila tukionana alikuwa ananikuta na gazeti la jitambue hakuwa akinielewa aliona nina mambo ya kizee na hata magazeti ninayoyapenda ni ya kizee alikuwa halielewi hata akiamua kulisoma the same applied to me nilikuwa simwelewi na magazeti yake ya KIU, RiSASI, UWAZI just to mention a few.
 
Back
Top Bottom