DR HAYA LAND
JF-Expert Member
- Dec 26, 2017
- 23,928
- 63,499
Acha ujinga wewe. Ulisikia wapi urusi msanii ajiite vladimir lenin kwa kua tu anaigiza sauti yake.Ujinga tu , nchi zilizoendelea hayo majina ya watu yanatumika sana na akuna tatizo tz sijui uwa Kuna nn
Kweli ni kosa kisheria kutumia jina la mtu pasipo na izini
Familia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere imewataka wasanii wanaoigiza sauti za viongozi akiwemo Baba wa Taifa kuanza kutumia majina yao halisi badala ya kujitambulisha kwa majina ya viongozi wanaoigiza sauti zao na kuleta mkanganyiko.
Msemaji wa familia hiyo ambaye ni mtoto wa sita wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage, Madaraka Nyerere ameyasema hayo wakati akipokea tuzo ya Mwalimu iliyotolewa na Umoja wa Wanafunzi waliosoma Shule ya Sekondari Milambo, (Amsha) kijijini Mwitongo wilayani Butiama mkoani Mara.
Madaraka amemtolea mfano Steve Mengele maarufu kama "Steve Nyerere" na kumtaka msanii huyo na waandishi wa habari kuanza kutumia jina lake halisi ili kuondoa mkanganyiko unaojitokeza kwa baadhi ya watu pamoja na familia kwa ujumla kwani na wao wana mwanafamilia aitwae Steven.
Familia hiyo pia imewataka viongozi na watu mbalimbali wanaofika nyumbani kwa Mwalimu Kijijini Butiama kwa ajili ya masuala mbalimbali ikiwemo kumuenzi Baba wa Taifa kutoa ushirikiano kwa familia hiyo hata baada ya kilichowapeleka kutamatika.
Familia hiyo imesema baadhi ya viongozi na watu mbalimbali hufika nyumbani hapo kufanya walichokusudia na baada ya hapo hupotea na kukata mawasiliano.
Madaraka Nyerere amesema kabla ya watu hao kufika nyumbani hapo huwa na mawasiliano mazuri lakini wakishakamilisha jambo lao hupotea kabisa.
Akizungumza kwa niaba ya familia, Madaraka amesema italeta maana zaidi kwa wanaokwenda Butiama na kuhusisha familia kuacha kukata mawasiliano kama kweli wanamuenzi Baba wa Taifa.
Amesema wanapopiga simu kwa viongozi hao kwa kuwa kunaweza kuwa na jambo la muhimu kujadiliana au ni taarifa muhimu mara nyingi watu hao hawapokei simu utadhani si wale waliokuwa 'wanawasumbua' wakitaka ushirikiano wao katika kumuenzi Mwalimu Nyerere.
USSR
Ni aibu kufikia wenye jina wanakuambia uache kulitumia.Kila ukoo ujitahidi kutoka kimaisha ili ujivunie ubini wao
Ubini wa Huyo Steve wa Mengele ni maskini wa kutupwa ndio maana kaamua akimbie huo ubini atumie ubini wa watu ubini wa Nyerere
Ukoo wa Mengele mkae chini mjitathimini kumaliza tatizo la ulofa kwenye ukoo wa Mengele ili watoto na wajukuu na vitukuu wajisikie fanatic kutumia jins la ubini ls Mengele badala ya kulikimbia na kwenda kuokota majina ya ubini ya watu sababu anaona jina la ubini la baba yake halina maana yoyote zaidi ya ulofa
Kaeni kikao mjadiliane hilo
Wameona jamaa anawazingua tuNi aibu kufikia wenye jina wanakuambia uache kulitumia.
Ukiona amekosea kulilinda jina la babake kutumika kiholela na kuwa hana haki hiyo basi nawe badili jina la babako kisha itangazie jamii kuwa wewe hutotumia jina la babako mzazi uuone mtoto wa wanaukoo!Nyerere alikosea sana kuto wasomesha watoto.
Mtu kuchagua jina si ni jambo la hiyari yake ?
Kwani Nyerere wa kwanza ni huyo baba yao?
Kwani kila Nyerere ni Kambarage ?
Hakuna hatia miliki ya Jina, watu wanaojiita Yesu sembuse Nyerere.
Maendeleo hayana Chama.
Kwasababu wamevumilia wamechoka. Pia wameona wanaotumomia jina la baba yao hawana akili wanaropoka pumba muda wote, inawaumuza. Hata wewe usingefurahia .Kwann leo hii
Ujumbe wako umefika kesho simu haipatikani kuanzia Asubuhi mpaka jioni mpaka waje na land rover za Arusha 😁Eti watu wangine wanakuja hapa ila wakishaondoka hawapokei simu Tena na wanapotea..... Kwenye haya maisha usijipe umuhumu kwenye maisha ya watu Wala usitake kupendwa... Hapa huyu Madaraka alitaka tu kutoa hisia zake kwamba hawathaminiki na hawapewi kipaumbele familia yao especially yeye, ningekua yeye ikifika Nyerere day nazima simu na sipatikani ili wasinizoee tena.
Kutumia jina Nyerere ni jina kama majina mengine Kila mtu ana haki ya kuitwa au kujiita... Mohammed, Mwakyambiki, Yesu, Mkapa, Obote, Kassim yote hayo ni majina unajichagulia unalotaka,, Hata huyo Nyerere baba ake kuna watu waliitwa Nyerere kabla yake...
Hivi unajua hata hiyo Elsa Marie ni jina la mtu huko liliko tokaKwasababu wamevumilia wamechoka. Pia wameona wanaotumomia jina la baba yao hawana akili wanaropoka pumba muda wote, inawaumuza. Hata wewe usingefurahia .
Inawezekana.Hivi unajua hata hiyo Elsa Marie ni jina la mtu huko liliko toka
Hujawahi kuona watu wenye ukoo tofauti lakn wana majina yanafanana kama Massawe Mushi etcInawezekana.
Lakini huyu steve mangere sijui steve nani alianza kutumia jina la nyerere wakati anafanya usanii wa kuigiza sauti ya nyerere. Hata sasa akiongea anajifanya anaongea kama mwalimu nyerere.
Pia kawarithisha watoto wake nao pia wanatumia ubini wa nyerere kwenye mitandao ya kijamii.