Kumbukumbu ya kuundwa kwa chama cha AA mwaka 1927 chini ya Sesilia Matola

Kumbukumbu ya kuundwa kwa chama cha AA mwaka 1927 chini ya Sesilia Matola

Ungelitambua hilo usingetembea dunia nzima ukiwatukana... Hivi Kleist Sykes asingebadili dini yake ya ukristu kisa mwanamke akawa muislamu leo ungemlilia kila kona ya ulimwengu? Mbona Cecil Matola humsemi wala kumuenzi zaidi ya kumfifisha ilihali yeye ndie mwasisi wa vyama Tanganyika?
Wewe Yericko Nyerere ni mpumbavu sana! Yaani nilikuwa nakuona kama mmoja ya vijana hazina ya taifa hili tukufu hapa jukwaani. Ila kupitia uzi huu umejivua nguo kabisa !

Umeshindwa kihoja na mzee mohame said naona umekimbilia kwenye dini yake! Mtu mstarabu alitakiwa achukue yakujifunza nakuyafanyia kazi..! Ila wewe unayejifanya mjuvi wa mambo bado unaleta ubishani wa kitoto!

Pathetic!

Sent by Ubavu
 
Ilikuwa mwaka 1927 ndipo chama cha AA kiliundwa kwa msaada wa Gavana wa Kiingereza nchini Tanganyika Sir Roland Davidl Cameron na Dr Agrey raia wa Ghana mwenye mtaa Kariakoo ya leo, huyu Mghana alikuwa mshauri wa kisheria na kimuundo tu, kikawa kinafanyia shughuli zake nyumbani kwa Rais wa kwanza wa AA bwana Cecil Matola kutoka kabila la wayao, na miaka mitatu baadae, yaani 1930 ndipo wakapata jengo toka kwa Gavana Donald Cameron, hapo ndipo picha hii ilipigwa,

Mwaka 1933 Cecil Matola alifariki dunia, na nafasi yake ikakaimiwa na katibu mkuu wa AA Bwana Kleist Sykies (ambae baba yake mzee Platanta alikuwa ni muhamiaji haramu toka Afrika Kusini aliyefika Tanga na kuanzisha makazi huko baada ya kuwa mateka wa wajerumani vita ya kwanza ya dunia), mpaka mwaka 1948 chama kilipobadilishwa jina nakuwa TAA chini ya Rais wake Daktari Vedasto Kyaruzi (Mhaya),

Hapo Rais wake wa kwanza wa TAA akawa Daktari Vedasto Kyaruzi, na katibu akawa Abdulwahid Klest Sykies, miaka miwili baadae, Dr Kyaruzi alihamishiwa Kingolwila hivyo nafasi ya urais wa AA ikakaimiwa na Abdulwahid Kleist Sykies hadi ilipofika uchaguzi wa 1953 ambao Julius Nyerere alimshinda Abdulwahid Kleist Sykies kwakishindo na kuwa Rais wa TAA, Mwaka mmoja baadae Julius Nyerere alibadilisha jina na mrengo wa TAA nakuwa TANU ya kupigania uhuru kutoka chama cha kuratibu shughuli za starehe za weusi (chama cha walevi)

................................................................ Yote kwa urefu yamo katika kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi,

View attachment 544629

View attachment 544695

Ndugu zangu,
Mambo hayo hapo juu katika kitabu.
Nisaidieni kusahihisha.
 
Wewe Yericko Nyerere ni mpumbavu sana! Yaani nilikuwa nakuona kama mmoja ya vijana hazina ya taifa hili tukufu hapa jukwaani. Ila kupitia uzi huu umejivua nguo kabisa !

Umeshindwa kihoja na mzee mohame said naona umekimbilia kwenye dini yake! Mtu mstarabu alitakiwa achukue yakujifunza nakuyafanyia kazi..! Ila wewe unayejifanya mjuvi wa mambo bado unaleta ubishani wa kitoto!

Pathetic!

Sent by Ubavu
Kama hujui mjadala huu kaa kimya na sihitaji heshima yako kwangu...
 
Mtanganyika ikiwa unaona napotosha njoo na historia unayoiamini tutaisoma.


Sent using Jamii Forums mobile app

UTANGULIZI

Naam. Ili mtu awe Afisa wa Idara ya Ujasusi yampasa awe mwenye akili zilizotulizana. Yaani, razini. Ndipo basi, pasi na kutafuna maneno, kitabu hiki ni mahususi hususan kwa wasomaji weledi. Kitabu hiki ni motifu, kinachoangazia masuala umuhimu ya ujasusi na jinsi yalivyo ya kipekee, kikitilia uzito umuhimu wake katika maisha ya wanadamu. Kutokana na upekee huo, taaluma ya ujasusi itumike kuleta ustawi katika jamii badala ya kudhuru kama ambavyo mashirkika mbalimbali ya ujasusi yamekuwa yakifanya kwa njia moja au nyingine, hii au ile. Ama kitabu hiki kinakusudiwa kutoa mwanga wa jinsi taaluma hiyo inavyopasa kuendeshwa pamoja na kuonesha uhalisia wa utendaji wake, kinyume na ilivyo kwa baadhi ya mashirika ambapo sasa imefikia hatua jasusi, kachero au afisa usalama kutangaza hadharani, “Unanijua mimi nani? Mimi ndimi, afisa usalama. Sichezewi!” Kwa lengo duni, ili kuwatisha watu kwa sifa za Mfalme Juha.

Mintarafu, kitabu hiki ni bashraf kwa baadhi ya mataifa yanayoendelea kuhusiana na suala zima la ujasusi, mathalani ujasusi wa kidola wa Idara ya Usalama wa Taifa la Tanzania (TISS) na Ujasusi wa Kimataifa unaofanywa na mashirika kama MOSSAD la Israel katika harakati zake za kutimiza dhamira ya kutawala eneo zima la Mashariki ya Kati na dunia kwa ujumla. Zaidi ya hayo, kitabu hiki kinatoa maarifa pevu ya kijasusi ili kuelewa misingi ya ujasusi na umuhimu wake pamoja na kukamilisha shughuli zake mbali mbali. Mathalani kuna Ujasusi wa Kiushindani (Competitive Intelligence) ambao zaidi hutumika katika ulimwengu wa biashara na harakati waweza kuainishwa kama utaratibu wa kiufundi wa kupata habari nyeti za biashara na harakati za malengo, wateja, washindani, maadui, teknolojia na mazingira ya jumla ya harakati na biashara. Habari hizi zaweza kutoka kwa mtu yeyote au vyanzo vyovyote katika eneo husika.

Ujasusi unatajwa kama ni taaluma ya pili kongwe duniani. Yaani, ulikuwapo tangu utanguni, ulimwengu ulipopata maarifa. Mashujaa katika vita vya kale wanasema kuwa ujasusi ni sehemu muhimu ya kimkakati, wakati wa vita. Kinachomuwezesha kamanda hodari kushambulia, kuteka na kufanya mambo yasiyo ya kawaida, yaliyo nje ya uwezo wa kawaida, ni ule ujuzi anaokuwa nao kabla ya pambano lenyewe. Na, ujuzi huo anaokuwa nao kabla, hautokani na uzoevu ama uhodari wa kufanya mahesabu, bali unatokana na taarifu za siri za adui ambazo hupatikana kutoka kwa watu wengine.

Aidha, ujasusi umekuwa sehemu muhimu ya taasisi za kijeshi na kibiashara. Na pia, ujasusi ulikuwa na hadi leo umekuwa ni chachu ya harakati za Kanisa Katoliki. Punde taarifu zinapopatikana, husambazwa kwa usahihi na kwa wakati kwa watoaji maamuzi wa ngazi zote. Ujasusi wa Kiushindani (Competeteve Intelligence) ni ujasusi unaoshughulika zaidi na harakati za kibiashara ambao unatofautiana kidogo na ule wa serikali. Hata hivyo, serikali pia huuwa na idara ya ujasusi wa kibiashara. Ujasusi wa Kiushindani unafuata taratibu na maadili ya biashara ambayo hayafuatwi na taasisi za ujasusi unaohami serikali. Ujasusi wa Kiushindani haufanywi chini ya mwavuli wa kidiplomasia bali, una lengo zaidi la kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kuimarisha huduma na kukabili mikikimikiki ya ulimwengu kwa ajili ya kujipatia faida na ufanisi wa shughuli husika. Kadhalika, Ujasusi wa Kiushindani unatofautiana na ukachero mwingine wa kiserikali ambao huweza kukiuka au kupuuza sheria na taratibu za wengine.

Nyuma ya pazia, mara nyingi, ujasusi hautazamwi kwa wema. Badala yake, ujasusi umeonekana kama shughuli isiyo na uhalali wa kimaadili au utu. Kwa ajili hiyo, kitabu hiki kinatoa changamoto kwa wajuzi na wajuvi wa taaluma hiyo, washiriki na watu wa kawaida kuonesha iwapo fani ya ujasusi itafanywa kitaalamu, inaweza kuwa ya muhimu kwa kurejea mifano ya wakongwe hasa MOSSAD (Israeli), CIA (Marekani), KGB (Urusi), M16 (Uingrereza) na wengineo, wameweza kutawala nyanja hio na kuweza kudhibiti kila sehemu kwa minajili ya kulinda na kuendeleza maslahi yao sehemu mbali mbali duniani.
Wataalamu wa ujasusi wa baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1939-1945), wametoa tafsiri nyingi kuhusiana na neno ujasusi. Licha ya tafsiri hizo, tafsiri ambayo pengine yaweza kukubalika na wote ni inayoafanua ujasusi kama shughuli za uchunguzi wa mambo mbalimbali kwa njia za kificho, mienendo na harakati za siri za usakaji wa habari au nyaraka muhimu na za uhakika kuhusu watu na matendo yao, yaliyo ya dhahiri na ya uficho, yanayoyafanywa dhidi ya watu wengine, serikali, jumuiya, taasisi, nchi, taifa, kabila, biashara au maslahi ya wengine. Kwa upande mwingine, kitaaluma, ujasusi ni ufundi wa kunasa taarifu au uwezo wa kupata taarifu nyingi kutoka vyanzo tofauti zenye kulenga kuhami, kushambulia kwa ufanisi zaidi, na kuangamiza adui ni shughuli za kimyakimya zenye malengo mazuri au mabaya kwa maslahi ya mtu, kundi, jumuiya, taasisi au Serikali.

Kwa tafsiri ya kiutendaji, ujasusi ni ukusanyaji na uchambuzi wa data na taarifu zinazotoka katika chanzo chochote kile (iwe kwa mtu au chombo). Taarifu hizo huwa zenye mitazamo ya mbali na zinazotoa taswira ya dhamira, nguvu, harakati na athari au matokeo yanayoelekea kutokea. Shughuli za kijasusi ni muhimu katika maisha ya kila siku ya ulimwengu huu wenye matukio mengi.

Tanbihi: Upelelezi/Ushushu/Ukachero ama Ujasusi kamili, usiishie ndani ya vyombo vya Ulinzi na Usalama tu mathalani Jeshi la JWTZ, Usalama wa Taifa, Polisi, Magereza na Uhamiaji tu, bali uende mbali zaidi kama Vyuoni au kwenye kampuni mbalimbali kunatakiwa kuwe na wapelelezi; mashirika ya umma yanatakiwa kuwa na wapelelezi, viwanda vya ndani vinatakiwa kuwa na wapelelezi na wote hawa wanatakiwa kufanya kazi pamoja ili kuleta maendeleo kwa jamii ya watu wao hasa Watanzania. Nchi zenye maendeleo yaliyotia fora, zinaendelea na kuendeleza ushindani mkubwa kwenye nyanja hii. Mathalani, Taifa la Jamhuri ya Watu wa China, lilianzisha utaratibu wa kupeleka wapelelezi nchi nyingi duniani ili wakadukue na kuiba teknolojia/tunduizi na maarifa kuzileta kwao. Hivi sasa, China wana mafanikio makubwa sana si tu kwenye teknolojia bali na kwenye vitivo vingine. Mfano mwingine unaturejesha wakati wa Vita Kuu Pili ya Dunia ambapo Marekani waliiba wanasayansi wengi wa Ujerumani ambao walikuja kusaidia kujenga uwezo mkubwa wa jeshi lao na taasisi nyingine. Kwa ujanja huo, Marekani limekuwa taifa lenye nguvu duniani kwa kipindi kirefu.

Tunapaswa kukumbuka kazi za ujasusi ni ngumu na zenye siri nyingi na kubwa sana. Majasusi wengi pia wana mafunzo ya kujilinda, kupambana, kushambulia na kufisha maisha. Tendo la kufisha katika medani za kijasusi ni tendo la hitimisho katika misheni au zoezi lolote lile ikiwa kutakuwa na ulazima huo na halina kinga ya kisheria wala msingi wa huruma ya kiutu. Muhimu ni kuwa kufisha huwa ni kwa maslahi ya Taifa.

Kwa kuhitimisha, ujasusi hautumiki kutafuta taarifu mbaya tu. La hasha. La mara elfu la. Kuna taarifu nyingi nzuri zinazoweza kutumika Vyuoni au Ndakini, Wizarani, jeshini na sehemu nyingine kwa minajili ya kuimarisha au kujenga zana na vifaa vya kisasa katika utandawazi wa dunia mpya........

Kitabu kinapatikana Dar kwa 80,000/= tu

Piga simu 0715865544
0755865544

IMG_20170729_090615_184.jpg
 
D
Chige,
Yericko hana kitabu wala nini...
Kkuandika hajui ataweza kuandika kitabu?

Hebu soma hili darsa nililomzawadia huko FB:
''Bado niko na wewe Yericko. Nimekuwekea darsa zima kuhusu uandishi wa vitabu. Meza kibri chako na soma na zingatia. Umesema uko Amzon lakini ukweli ni kuwa hawakujui huko. Mimi nimeingia Amazon toka mwaka wa 1998 kwa hiyo nawajua vyema. Kuna kitu lazima ukijue pia. Amazon hujipeleki. Amazon unapelekwa na ''publishers,'' na ''booksellers'' yaani wauza vitabu. Kuna kitu kinaitwa ''blarb'' katika kitabu. Haya ni maelezo nyuma ya ''cover,'' ya kitabu. ''Blarb,'' inaandikwa na ''publisher,'' si wewe Yericko. Huu ni ushauri wa bure wenzako wanalipia fedha. Mimi nakupa bure ili ujitoe katika ujinga.''

5bDT5yK4WfHz0QFpqYKBzUNiSToufTEZZ5p4HUil4VnNM7AoRI2DPidbJp3SvJjB4tC74NS1Me9u6h_WzKik7hLuj6eQM6uKlb7jjgn-2OeZxEV7ZWVUt2N1lXfLGR3n-cjnsiif0fZH3_TyeEzV80edxUgStfIJs7gZrzdi4EFjDMRwjOYK2OnpI2ub0FdB9e1Q7-uC1uVcXDSohM3Orp2aQMp73JB023taZeWCz-M9WtJEVuxq_C7qjt68ahXqSlkX68knlzkxEapRn4dllWkiZaXT-9COMnzIqGI6jD8VWF-AY374i0m8NnAP8TU6mVRgMBc2jBLvDQypndbIEuDNrzBHId43uU07S35PFVz-iFP1h6ZTFGyA7dnVUAtPdGV_m94rgn3QyRJ8rWHWDpVF2ywH1qBSHGQH0e0vV7h2EtTUERqlkuvBxab22AHizpLrSFtxPgxBF_G57kU_4Uj35VLjlI7MPPGS0GnKsMVT1kDG0BOBNPDrvn_IFCKqi2k7SlcNVRfmO5CiOMQpAZpcHt7u9_KPzCdVMxtwkVYUvD1v2bYtDHeWGOs6J7Iu8rohqMAhLLgNhzySaThe6Yu0Z5dY_XoOBNVnqq_zNA_mf9F5au2JpQ=w335-h188-no


''Daisy baada ya kufariki baba yake mwaka wa 1968 alitaka kuandika kitabu cha maisha yake lakini mwalimu wake John Iliffe alimwambia somo hilo linataka muda haitakuwa vyema kwa yeye kufanya haraka. Daisy hakuandika kitabu kile na ikaja kuwa mimi ndiye Allah akanijaalia kukiandika kwa msaada mkubwa sana wa nyaraka za ukoo wake. Picha hiyo tumepiga April 2017 na Daisy ni huyo kashika kitabu cha maisha ya baba yake. Unaweza kumsoma Daisy katika hii, ''paper,'' yake: A.D. Sykes ‘’The Life of Kleist Sykes,’’ University of Dar es Salaam Ref. No. JAN/HIST/143/15). Inapatikana Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana.''

''Marafiki wa Mwalimu Nyerere na baadhi ya wasomi wameona ni bora baada ya mimi kuandika kitabu cha Abdul Sykes ambacho kwa namna moja au nyingine kimegusa maisha ya siasa ya Baba wa Taifa, na wao wafanye utafiti na iandikwe ''biography,'' ya Mwalimu Nyerere. Nimefanya mahojiano na wao nyumbani kwangu Magomeni Mapipa mara tatu na nimewapa nyaraka na picha nyingi sana kutoka kumbukumbu za akina Sykes. Mradi huu nadhani sasa uko mwaka wa nne. Wanaofanya utafiti huu ni Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Othman Yahya na Dr. Kamata.''

Chige,
Haya ndiyo yangu katika historia hii.
Darsa ni kiswahili cha wapi? Hata kama neno lina asili ya kiarabu lakini baada ya kulikopa na kuliingiza kwenye matumizi lahaja yake imebadilika kuendana na lugha mpya ya kiswahili, hivyo tusione ni ufahari saaana kulitamka au kuandika kama waarabu walitamkavyo bali ni vyema tukalitumia kama watanzania wote tunavyolitumia neno hilo DARASA na sio DARSA
 
Okaoni mimi nimezaliwa Dar es Salaam na kukulia Dar es Salaam sijapatapo kuzungumza lugha nyingine yeyote ila Kiswahili na nakisema kwa lafidh ya Pwani. Darsa ni mfano wa "lecture," hii ni tofauti na "darasa," yaani "class room."
Mohamed kwani wewe unaweza kuzungumza lugha ngapi?
 
Nguruvi,
Nazungumza lugha mbili Kiswahili na Kiingereza.
Sawa, kauli ya kwamba 'hujapato kuzungumza lugha nyingine zaidi ya kiswahili ilinishtua, kuna vitabu umeandika kwa kiingereza na huko unakokwenda sikuwahi kusikia una mkalimani

Uliwahi pia kusema kama sitakosea kuwa asili yako ni Umanyema!
Kama ndivyo, wamanyema hawana lugha!

Pili, unafahamu kidogo wa lugha ya kiarabu?
 
Sawa, kauli ya kwamba 'hujapato kuzungumza lugha nyingine zaidi ya kiswahili ilinishtua, kuna vitabu umeandika kwa kiingereza na huko unakokwenda sikuwahi kusikia una mkalimani

Uliwahi pia kusema kama sitakosea kuwa asili yako ni Umanyema!
Kama ndivyo, wamanyema hawana lugha!

Pili, unafahamu kidogo wa lugha ya kiarabu?
Nguruvi,
Nilikusudia kusema lugha nyingine hapa nyumbani kama ''dialect.''
Wamanyema wa Tanzania hawana lugha yao.

Sifahamu Kiarabu.
 
Nguruvi waliingia Tanganyika wakizungumza, "Kilungwana," yaani Kiswahili.

Kuongea lugha kwa matamshi tofauti kunategemea asili zetu kuna watu hawawezi kutofautisha kati ya "r," na "l."
Kwahiyo unataka kutuambia kuwa Wamanyema hawana lugha isipokuwa kilungwana? I mean hakuna lugha ya Kimanyema?
 
Nguruvi3,
Wamanyema wanasema Kiswahili ndiyo lugha yao. Hicho Kilungwana ni Kiswahili na hilo neno lilitumika zaidi ya karne mbili sasa wakati wanaingia Tanganyika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nguruvi3,
Wamanyema wanasema Kiswahili ndiyo lugha yao. Hicho Kilungwana ni Kiswahili na hilo neno lilitumika zaidi ya karne mbili sasa wakati wanaingia Tanganyika
Historia inaonyesha asili ya kiswahili ni Pwani. Wamanyema wametoka Kongo kama sijakosea

Hili ningeomba mwenye ufahamu atueleweshe, hivi ni kweli hakuna lugha ya Kimanyema?
Na je ni kweli kuwa lugha ya kimanyema ni kiswahili!

Nikirudi kwa Mohamed, uwepo wa Kilungwana tu unatosha kuonyesha kitu tofauti na kiswahili
 
Back
Top Bottom