Kumbukumbu ya kuundwa kwa chama cha AA mwaka 1927 chini ya Sesilia Matola

Kumbukumbu ya kuundwa kwa chama cha AA mwaka 1927 chini ya Sesilia Matola

Nguruvi mimi nazungumzia historia ya karibuni ya kuingia Wamanyema Tanganyika wakija huku wakiwa kwanza Waislamu na lugha yao Kiswahili. Hiki Kiswahili wamekipata katika kuingiliana na Waarabu. Wamanyema wakakichukua Kiswahili kama lugha yao na huo Ulungwana maana yake ni Uungwana yaani yeye kastaarabika ni Muislam.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nguruvi mimi nazungumzia historia ya karibuni ya kuingia Wamanyema Tanganyika wakija huku wakiwa kwanza Waislamu na lugha yao Kiswahili. Hiki Kiswahili wamekipata katika kuingiliana na Waarabu. Wamanyema wakakichukua Kiswahili kama lugha yao na huo Ulungwana maana yake ni Uungwana yaani yeye kastaarabika ni Muislam.
Kabla ya kuingiliana na Waarabu, hao Wamanyema walikuwa wanazungumza lugha gani?
 
Mohamed pia niukumbushe kuhusu msaada niliomba wa kuelewa tofauti ya Quran na Arabic

Halafu hili la Wamanyema, kabla ya kuingliana na Waarabu wao walikuwa wanazungumza lugha gani.
 
Mohamed, natoka kidogo kwa udhru, nitarudi tuendelee na mnakasha
 
Hili la Arabic na Qur'an sijui tofauti yake.
Kabla sijatoka umenijibu. Mohamed ni kweli hujui tofauti ya vitu hivyo?

Kama ni hivyo na kwa mantiki yako, je, nitakuwa nimekosea nikisema kuwa wewe unaongea kiarabu? Kumbuka ni wewe uliyetuletea tafasiri ya maneno ya Dr Dau akifungua daraja la Kigamboni. Je tafasiri ile ilitokana na nini Quran au Arabic na ilikuwaje ukaelewa tafasiri ikiwa hukujua ni ya lugha gani

Nitarudi tuendelee maana hapa naona kuna mnakasha mzuri sana
 
Tafsiri ya Qur'an nimesoma na ikisomwa nami nasikiliza nafahamu maana yake lakini siwezi kuzungumza lugha. Swali hilo lako aliniuliza mwalimu wangu mmoja Arab Maratime Transport Academy Alexandria, Egypt baada ya sala ya Ijumaa, akaniuliza kama nimeelewa khutba. Nikamjibu ndiyo. Akashangaa vipi nitaelewa khutba ilhali sijui Kiarabu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafsiri ya Qur'an nimesoma na ikisomwa nami nasikiliza nafahamu maana yake lakini siwezi kuzungumza lugha. Swali hilo lako aliniuliza mwalimu wangu mmoja Arab Maratime Transport Academy Alexandria, Egypt baada ya sala ya Ijumaa, akaniuliza kama nimeelewa khutba. Nikamjibu ndiyo. Akashangaa vipi nitaelewa khutba ilhali sijui Kiarabu?
Dah habar kubwa sheikh. Ina maana hakuna mahusiano yoyote kati ya Quran na Arabic?
 
Mimi ni kizazi cha tatu Mmanyema kuzaliwa Tanganyika hata bibi yangu mkuu nimemuwahi hakuwa anazungumza Kimanyema. Yeye alikuja kutoka Kongo
Hakuna kosa wewe kutojua kimanyema. Swali la msingi ni kuwa kabla ya Wamanyema hawajaingiliana na Waarabu na kupata lugha ya kilungwana, walikuwa wanazungumza lugha gani.
Umesema hapo juu walizungumza Kimanyema

Kwa kauli hiyo ina maana kuna lugha ya kimanyema ambayo si lazima uijue kutokana na mazingira
Hata hivyo ukweli wa lugha hiyo hauwezi kufichwa au kufunikwa

Ninapochanganyikiwa kuelewa, sijui wewe umebeba utamaduni upi, wa Kimanyema au kiswahili
 
Ngruvi3,
Mimi utamaduni wangu ni mila ya Nabii Ibrahim.

Inaanzalna Qur'an Arabiyya...Qur'an imeshushwa katika lugha ya Kiarabu.
Ah Mohamed, kama utamaduni wako ni ule wa Nabii Ibrahimu hakuna shaka

Tatizo linajitokeza kwa ukweli kuwa LUGHA hubeba utamaduni wa jamii husika.
Ni ukweli usiopingika popote pale duniani

Sasa Arabic umesema huwezi kuzungumza, na hiyo ndiyo imebeba utamaduni. Huoni tatizo hapo?
 
Ah Mohamed, kama utamaduni wako ni ule wa Nabii Ibrahimu hakuna shaka

Tatizo linajitokeza kwa ukweli kuwa LUGHA hubeba utamaduni wa jamii husika.
Ni ukweli usiopingika popote pale duniani

Sasa Arabic umesema huwezi kuzungumza, na hiyo ndiyo imebeba utamaduni. Huoni tatizo hapo?
Nguruvi3,
Hapana sijaliona tatizo.

Hakika lugha hubeba utamaduni nami ninalo tatizo hili nina mjukuu
hasemi Kiswahili na nawaambia wazazi wake kuwa Uislam unakwenda
na utamaduni wake kwenye lugha yetu nayo ni Kiswahili.

Wakifanya maskhara, nawaambia mtoto atasoma Qur'an na lafidhi ya
London.

Mimi lugha yangu ni Kiswahili na Uislam umejikita vizuri katika Kiswahili.
Nikisema, ''shahada,'' najua ni nini halikadhalika nikisema, ''sala.''

Hiki ni Kiarabu na kipo ndani ya Kiswahili.

Nikisoma Aya hii, ''Akimi salat liduluki shamsi ila ghasaki layli wa Qur'an
Fajr...''

Angalia hapo unayaona maneno mangapi ya Kiswahili katika Aya hiyo?
Wewe utatambua, ''sala,'' ''Qur'an,'' na ''Fajr.''

Aliyesoma Qur'an atajua maana ya maneno yote hayo ila labda machache.
Nadhani umeelewa.

Sasa turudi kwa yule mwalimu wangu wa Arab Maratime Transport Acedemy
Alexandria, Egypt.

Tuko katika msikiti wa Muntaza Palace, Alexandria.

Muntaza ilikuwa moja ya makasri ya Mfalme Faruq wa Misri na kuna msikiti
mzuri sana.

Tumemaliza kusali Ijumaa akaniuliza kama nimeelewa khutba nani nikamjibu
kuwa nimeielewa.

Akashangaa vipi nimeielewa khutba ya Kiarabu ilhali mimi Kiarabu sikijui?
Nadhani sasa nimekuelewesha na umefahamu.

Hii ni nyongeza.

Iko siku huyu mwalimu wangu akaniuliza kama namjua Um Kulthum.
Nikamwambia kuwa mama yangu akiimba nyimbo zake tena kwa Kiarabu.

Alichoka.
 
Inaanzalna Qur'an Arabiyya...Qur'an imeshushwa katika lugha ya Kiarabu
Kwa mantiki hiyo ukielewa Quran kwa kuisoma na kuieleza moja kwa moja unaongea Kiarabu.
Kiarabu ni lugha imetumiwa kama 'vehicle' ya contents ndani ya Quran.

Huwezi kuzielewa contents kama huelewi zimebebwa kwa 'vehicle' gani

Unachojaribu kukwepa ni kusema 'unaongea kiarabu' kama lugha kukwepa fedheha ya Kimanyema kama lugha mama

Pili, unaposema Kiswahili ni lugha ya Quran kuna walakini.
Waliopokea Uislam ni watu wa Pwani kwasababu za usafiri zilizoleta wageni kwa bahari

Kiswahili kilikuwepo bali ujio wa dini uliimarisha na kutumika kama lugha ya mawasiliano iliyosambaza dini. Soma vitabu vya watunzi wa kale utaelewa kwanini kiswahili kilikuwepo

Hoja ya kwamba Kiswahili kimebeba Uislam ni kweli na ina mantiki kwasababu nilizoeleza

Hata hivyo Kiswahili si Uislam bali kuna mahusiano ya Kiswahili na Uislam kutokana na mazingira ya wakati. Ni mahusiano hayo kama yalivyo ya Ukristo na Kiingereza

Tukirudi katika Umanyema, ningekuomba usidharau lugha hiyo.
Umanyema ndio mother tongue yako hizi zingine ni za kufikia.

Na wala kuwa mmanyema hakuondoi mantiki ya utamaduni wa Ibrahimu.

Unaweza kuwa na tamaduni nyingi, muhimu ni namna gani una practice tamaduni hizo.

Kiingereza unachosema kimebeba utamaduni, hakijaondoa utamaduni wako wa Ibrahimu

Muhimu utambue kuwa dini yoyote ni imani iliyojengwa kiroho.

Hili ni tatizo kwa wananchi wetu wengi. Wanashindwa kuelewa mipaka ya dini na tamaduni
 
Kwa mantiki hiyo ukielewa Quran kwa kuisoma na kuieleza moja kwa moja unaongea Kiarabu.
Kiarabu ni lugha imetumiwa kama 'vehicle' ya contents ndani ya Quran.

Huwezi kuzielewa contents kama huelewi zimebebwa kwa 'vehicle' gani

Unachojaribu kukwepa ni kusema 'unaongea kiarabu' kama lugha kukwepa fedheha ya Kimanyema kama lugha mama

Pili, unaposema Kiswahili ni lugha ya Quran kuna walakini.
Waliopokea Uislam ni watu wa Pwani kwasababu za usafiri zilizoleta wageni kwa bahari

Kiswahili kilikuwepo bali ujio wa dini uliimarisha na kutumika kama lugha ya mawasiliano iliyosambaza dini. Soma vitabu vya watunzi wa kale utaelewa kwanini kiswahili kilikuwepo

Hoja ya kwamba Kiswahili kimebeba Uislam ni kweli na ina mantiki kwasababu nilizoeleza

Hata hivyo Kiswahili si Uislam bali kuna mahusiano ya Kiswahili na Uislam kutokana na mazingira ya wakati. Ni mahusiano hayo kama yalivyo ya Ukristo na Kiingereza

Tukirudi katika Umanyema, ningekuomba usidharau lugha hiyo.
Umanyema ndio mother tongue yako hizi zingine ni za kufikia.

Na wala kuwa mmanyema hakuondoi mantiki ya utamaduni wa Ibrahimu.

Unaweza kuwa na tamaduni nyingi, muhimu ni namna gani una practice tamaduni hizo.

Kiingereza unachosema kimebeba utamaduni, hakijaondoa utamaduni wako wa Ibrahimu

Muhimu utambue kuwa dini yoyote ni imani iliyojengwa kiroho.

Hili ni tatizo kwa wananchi wetu wengi. Wanashindwa kuelewa mipaka ya dini na tamaduni
Nguruvi3,
Kwanza napenda nikufahamishe kuwa mimi sina sababu yoyote ya kuwa na ''complex,''
kwa hiyo siwezi kuwa na sababu ya kudharau lugha ya Kimanyema.

Lakini ningependa kukueleza kuwa Kimanyema hakijapatapo kusemwa katika ardhi ya
Tanganyika.

Kuhusu lugha ya Kiarabu.
Ningekuwa najua lugha hii kwangu ingekuwa faraja kubwa.

Dr. Abbas Abu Abbat aliyekuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Markaz, Sudan alinifanyia
darasa langu binafsi Khartoum niende nikasome Kiarabu.

Huyu Msaudia nilikutananae Nairobi 1989 katika mkutano ambao lugha ilikuwa Kiarabu.
Katika wote waliohudhuria mkutano ule ni mimi peke yangu ndiye niliyekuwa na mkalimani.

Mwisho wa mkutano Dr. Abu Abbat alinipa, ''offer,'' ya ''Special Course,'' ya Kiarabu na
alinambia miezi 9 ingetosha mimi kusema Kiarabu.

Sikuweza kuchukua, ''offer, ile.

Nilipokutananae Khartoum 1990 Dr. Abu Abbat alinitania kwa kuniambia kuwa lile darasa
langu bado lipo linamsubiri mwanafunzi wake.

Hayo mengine ni fikra zako sina haki ya kuziingilia.
 
Back
Top Bottom