Kumekucha: Baraza la Mawaziri kivuli - Mbatia out

Kumekucha: Baraza la Mawaziri kivuli - Mbatia out

Mbowe ni kiongozi makini sana. Big up Mwamba.
Bila Mbowe, siasa za upinzani Tanzania zisinge kuwa zimefikia hapa - kwanza Credit kubwa mno kwake kwa kufanikisha kupatikana kwa wanachama wapya takribanii 6m nchi nzima na kufanikisha uchaguzi mkuu ndani ya chama..... hasa ukizingatia hali ya ufanyaji wa shughuli za kisiasa ulivyo sasa.

CDM inazidi kukua pamoja na hila zote hizo hazitii dafu......

Vijana wasomi wanajiunga katika chama huku wazee walioishiwa hoja wakitoka nduki.......
 
Yanayotokea kwa CHADEMA sasa ni mambo ya kupitia machungu na kujifunza.

Safari bado ni ndefu lakini la muhimu safari haiwezi kuisha.

Mshika dola ataendelea tu kutumia rasilimali na uwezo aliojipa kuzuia kila chama kitakachoibuka kuwa tishio.

Hakuna namna ataruhusu vyama vipate ushindi rahisi.

Ni jukumu la vyama vya upinzani halisi na wanaowaunga mkono kulitambua hilo, kubadili mbinu kadiri ya aina ya mchezo na kupambania ushindi kila sehemu.

Siyo jambo la afya kabisa kuwa na bunge asilimia 90 ni chama tawala.

Bila shaka hata wananchi wengi hawapendi iwe hivyo, lakini miundo mbinu ya kuwapata wawakilishi inaondoa fursa hiyo ya kupata uwiano wenye faida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii nayo italeta impact gani kwa Chadema inayoenda kufa? Bado miezi kama mitatu bunge livunjwe?
hivi unamkumbuka lile lizee la bunda lililoangushwa na binti mdogo wa chadema? hili zee lilisemaga haya maneno uliyosema wewe ZWAZWAmbugila wa LUMUMBA kuwa CDM haifiki 2014 inakufa. leo ni lini na nani kati ya hili lizee na CDM aliyekufa?
CHUNGA MAKALIO YAKO UTATAFUNWA KWEUPE HADHARANI
 
Hapa hata magufuli kawapiga bao. Maana kwenye nafasi za uongozi anao hadi waliokuwa upinzani na kugombea uraus kama kina anna mghwira.
Mbowe ye ukitofautiana nae tu ujue out. Hana uvumilivu wa kisiasa. Acha Magufuli awanyooshe tu maana wao wangeshika dola wangenyanyasa sana watesi wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Anaaga maana KUB hatapata tena nafasi hiyo.
 
Hapa hata magufuli kawapiga bao. Maana kwenye nafasi za uongozi anao hadi waliokuwa upinzani na kugombea uraus kama kina anna mghwira.
Mbowe ye ukitofautiana nae tu ujue out. Hana uvumilivu wa kisiasa. Acha Magufuli awanyooshe tu maana wao wangeshika dola wangenyanyasa sana watesi wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Magu kashajichokea sasahivi anatapatapa tu baada ya kuona mfuko wa manunuzi alokabidhiwa slowslow umeanzakukata na chadema halifi tu liko ngangari
 
hivi unamkumbuka lile lizee la bunda lililoangushwa na binti mdogo wa chadema? hili zee lilisemaga haya maneno uliyosema wewe ZWAZWAmbugila wa LUMUMBA kuwa CDM haifiki 2014 inakufa. leo ni lini na nani kati ya hili lizee na CDM aliyekufa?
CHUNGA MAKALIO YAKO UTATAFUNWA KWEUPE HADHARANI
Mh...
 
Naunga mkono hoja, Chadema pekee yao hawawezi na haitakuja kutokea wakaweza!. Sisi Tanzania tuna tatizo kubwa la kitu kinachoitwa "Managing The Political Diversity" from both parties, CCM na Wapinzani, hadi ndani ya mihimili Bunge, Serikali na Mahakama.

Kwa muda uliobakia, hata kama Chadema inajua NCCR imenunuliwa na CCM, hivyo itajitenga nao, na Wabunge wote wa CUF wanasubiria tuu Bunge livunjwe watur rasmi ACT Wazalendo, Chadema walipaswa wawavumilie tuu, sometimes its good kumvumilia adui yako ili usiwaudhi wale waliokuja kwako kwasababu ya huyo adui yako. Kura milioni 6 za Lowassa ile 2015 sio za wana Chadema pekee.

Kosa kubwa la Chadema kuelekea 2020 ni kujidhania kwenye kambi ya upinzani, Chadema bado ni determinant, it's not!. Kuendelea 2020, Chadema is a dying horse, hivyo kitendo kama hiki cha kuihodhi kambi rasmi ya upinzani Bungeni, it's like a final kick of a dying horse.

Ili upinzani uweze kuvuna mavuno yoyote ya maana 2020 kwanza lazima Chadema wakubali kugawana himaya yake kwa kukubali ku share na vyama vingine vya upinzani.

Kabla ya Bunge kuvunjwa, Chadema ambacho kwa sasa ndio chama kikuu cha upinzani, kifanye SWOT na PEST analysis kwa Wabunge wake wote, matokeo ya analysis hiyo yakionyesha Mbunge huyu anachaguliwa kama mtu na sio chama, then Chadema ikubali matokeo, wabunge wote wa Chadema watakaojiunga CCM, Chadema ijihesabu hayo majimbo yamepotea unless wana CCM wenyewe ndio waipigie Chadema kura za chuki kutokubali wapinzani waja leo na kusimamishwa kugombea CCM.

Pili wabunge wote wa Chadema watakao hamia vyama vingine, Chadema ikubali to share them na wapinzani wengine kwa kutosimamisha wagombea wengine ili kila jimbo na kila kata mgombea wa CCM apambane na mpinzani mmoja tuu. Ikitokea jimbo lilikuwa Chadema kama Moshi Vijijini na Rombo, wabunge wake wwkahamia NCCR Mageuzi, Chadema ikubali matokeo. Ikisimamisha wagombea wapya, hii itakuwa ni vita vya panzi, furaha ya kunguru, wapinzani wata split kura zao, CCM atayatwaa majimbo ya upinzani kama ameokota dodo chini ya muembe.

Upinzani pamoja na tofauti zao za ndani, lazima wavumiliane by managing diversity kwa kushirikiana hivyo hivyo pamoja na tofauti zao, wasimame united and stand as one against a common enemy, vinginevyo kwa huku bara, tunarudi kuwa nchi ya chama kimoja CCM only and only CCM!.
P
Unadhani kwa sasa CUF na NCCR kwao na Chadema wanapambana na one common enemy ambaye ni CCM? Anaye amini hivyo ni bonge la mnafiki na nadhani Mbowe na Chadema hawajapenda kuwekwa kundi hilo.
Nadhani unaukumbuka msimamo wa George Bush wakati wa vita vya ghuba (Desert Storm), kwamba eitha uko nasi kama rafiki au uko na adui yetu kama adui na sio vinginevyo.
 
Duh...!. Kama kuna binaadam anayeamini ataishi milele, then huyo sio binadamu ni mungu!. Na kama kuna binaadam yoyote anayeshabikia mabaya yakimkuta binadamu mwingine huyu naye sio binaadam, huyu ni shetani!. Kufurahia mateso yoyote ya binaadamu yoyote ni ushetani.
Ila pia kumsingizia uongo binaadam mwingine kuwa nyuzi zake zinashabikia shambulio la Lissu, kama sii kweli zinashabikia, then huu pia ni ushetani!.
Tuna mashetani wengi miongoni mwetu kuliko tunavyojidhania!.
P.

Bila kujiingiza moja kwa moja kwenye majibizano yako na huyo member, vyote ulivyoandika kuhusu Lisu tuliviona na kuvisoma. Tuna uwezo wa kusoma na kuelewa, na kisha kupima msimamo wako kwenye shambulio la Lisu
 
Unafiki hautakiwi kaka,kama ambavyo Magufuli aliwapiga chini washindani wake akina January na Nappe ndivyo hivyo hata mbowe amefanya.Unafika wakati watanzania wanaona kama Mbowe na CDM wanafanywa ndondocha na watu kama akina mbatia na Antony Komu hivyo baadhi ya Wananchi nikiwemo mimi niliona kama Mbowe hana makucha hivyo hata kiuongozi inakupunguzia point.
Hii ni ishara kwamba hatua zinachukuliwa kwa yeyote yule bila kujali ni nani na amefanya nini kama amekosea anaadhibiwa.
Siasa za Tanzania kichekesho sana.
Si upinzani wala CCM ni vituko tupu.

Sasa bunge lenyewe ni la mwisho kabla ya serikali mpya, hao mawaziri vivuli wapya watakao ziba nafasi hizi watafanya nini?
Na wa zamani waliotemwa wangekuwa na athari gani?

Kuna wakati unatakiwa kuwaacha watu kama hao na kutumia nafsi hiyo kujiimarisha kisiasa kwa kujisifu majukwaani hawa walitutendea ubaya huu lakini kwa vile sisi wakomavu wa kisiasa na sio watu wa visasi tumewaacha kwenye nafasi hizi ingiwa sababu na uwezo wa kuwatosa kama kisasi tulikuwa nao.

Mambo madogo kama haya ya uvumilivu ndiyo yana kuwezesha kuvuna pointi muhimu kwenye siasa, hasa kwenye masanduku ya kura.
You can act like you live what you preach.

Wapiga kura ni watu wa ajabu sana, wanaweza kukupa kura sababu umewataja kwa majina angalau watu wawili tu wa kawaida wa eneo lao, au umewapa msamaha watu waliokutendea ubaya.

Huenda sipo sahihi kabisa katika hili, ngoja niamini KUB yupo sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Mzee alikuwa sahihi sna Sema ndugu zetu wazito sna kusikia au kusoma ushauri wake...
IMG-20200403-WA0065.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom