Walnut Creek
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 5,830
- 6,315
Mambo kama haya yanatokea tunapokuwa na Rais Kilaza na MVIVU.Mamlaka ya maji safi na maji taka Dar es Salaam imetangaza mgao wa maji jiji la Dar es Salaam kanda ya Kinondoni ili kupunguza kero kwenye maeneo yanayotajwa kuwa na msukumo mdogo. Katika ratiba hiyo wakaazi wa Masaki na Obey wameula, watapata maji saa 24 siku saba za wiki. Baadhi ya maeneo sijayaona kabisa pia tangazo halina mwanzo wala ukomo wa mgao.
Anyways tunawasubiri Tanesco nao watoe ratiba badala ya kwenda kimya kimya pia wasisahau majenereta ya IPTL, tuko tayari kuchangia akaunti ya Tegeta Escrow..
View attachment 2013747
Heri dhalimu yule kuliko hawa wachamungu wa sasa watatuua hawa malaika wa shetani hawa.Eeh nchi inafunguliwa bwana toka kwa dhalimu jiwe 😅!!!
Dhalimu ambaye hajawahi kuwalaza gizani zaidi ya masaa 24 katika siku zote ambazo alikuwa madarakani! Maji hayakuwahi kukatika katika namna yeyote isioeleweka😅
“Sote tu watu wazima haina haja ya kufatiliana na kutumbuana kila mtu afanye majukumu yake kwa moyo”~Amiri jeshi
Ha ha ha ha ha ha! Wacha nifike mlimani nikajipooze na AC za umma kwanza😅 hii joto ya huku uswahilini haifai!
Wangapi wana uwezo wa kujenga system ya kuvuna maji, nyumba zenyewe vyumba vina ungwaungwa kama mabewa, chumba cha kulala unajenga leo, sebule baada ya miaka mitano, mitano mengine unaongeza chumba kingine, baada ya mitatu stoo......... Kuna wengine hawajui lini watamaliza kujenga nyumba zao.Mkiwa mnajenga nyumba msisahau kuweka system ya kuvuna maji ya mvua.
Inategemea nyumba iko wapiMkiwa mnajenga nyumba msisahau kuweka system ya kuvuna maji ya mvua.
Kwani huyo fala alikuaa Mungu?JPM alisema mtamkumbuka, mtamkumbuka tu... sio ombi! Pale samaki wenu watakapoanza kuoza kwa kukosa umeme wa mafriji, pale mtakapoanza kukosa maji ya kufanyia shughuli za kila siku...
Sasa hapo obei na masaki wanatumia mfumo tofauti??
Wewe si ndio ulikuwa mtabiri wa vifo wewe mkuu!!Mkiwa mnajenga nyumba msisahau kuweka system ya kuvuna maji ya mvua.
Mimi nafurahi sababu walikuwa wanasema huyu Magufuli ni mpigaji ngoja sasa wale ambao sio wapigaji wamerudi sasa ndio mtajua kuwa mlikuwa hamjui kitu.JPM alisema mtamkumbuka, mtamkumbuka tu... sio ombi! Pale samaki wenu watakapoanza kuoza kwa kukosa umeme wa mafriji, pale mtakapoanza kukosa maji ya kufanyia shughuli za kila siku...
Sasa hapo obei na masaki wanatumia mfumo tofauti??
Una afadhali. Hapa nilipo ni wiki ya pili maji hakuna kutoka hata mara moja.Mbona tunaopata huduma kutoka mtambo wa Ruvu juu hatuoni ratiba maana eneo nilipo leo ni siku ya nne mfululizo maji hayajatoka.
Kwa kweli hakua mungu ila huu ufala wa Dawasa ulimuogopa kama ukoma.Kwani huyo fala alikuaa Mungu?
Vipi mwenzetu ulishawahi kutekwa au kutekewa ndugu, jamaa, rafiki au mtuwako wa karibu yoyote?!Bora kukosa Maji na umeme kuliko kutekana kidwanzi na mtu mmoja kujifanya ndio mungu mtu nchi nzima.
Niliwahi kukuteka awamu ya 5 Mara 3, Nataka nikuteke awamu hii ya 6 japo kiduchu tu.Vipi mwenzetu ulishawahi kutekwa au kutekewa ndugu , jamaa, rafiki au mtuwako wa karibu yoyote?!
Otherwise sema ukweli umetoa wapi hii idea ya kutekana?!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kuna kipindi walitaka kuwafuata na story za kuwatoza kwa lita wanazotumia za maji ya ardhini.Kuna wilaya haziguswi na DAWASA kabisa wilaya ya kigamboni Ubungo,Temeke na Ukonga wao wamejizoelea kunywa maji ya madimbwi wanayojichimbia na Maji ya mvua
Ukiwaangalia hata muonekano wa sura wanaotoka maeneo hayo yasiyo na ratiba wako tofauti na huko kwenye ratiba ya Dawasa sura zao zimekakamaa hasa
Ratiba haiwahusu
Manina... [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Eeh nchi inafunguliwa bwana toka kwa dhalimu jiwe [emoji28]!!!
Dhalimu ambaye hajawahi kuwalaza gizani zaidi ya masaa 24 katika siku zote ambazo alikuwa madarakani! Maji hayakuwahi kukatika katika namna yeyote isioeleweka[emoji28]
“Sote tu watu wazima haina haja ya kufatiliana na kutumbuana kila mtu afanye majukumu yake kwa moyo”~Amiri jeshi
Ha ha ha ha ha ha! Wacha nifike mlimani nikajipooze na AC za umma kwanza[emoji28] hii joto ya huku uswahilini haifai!
Haya neno kwa ambao hawapigi hizo trilioni 1.5 mkajenge nchi sasa kwa kudhurumu wananchi.Tutamkumbuka kwa wizi wa 1.5 trillion na mauaji ya watanzania
Kuna jamaa kaoga maji ya mrefejini kapauka then ananukia kama churaNimeshindwa kwenda chuo kwa sababu sina maji siku ya nne, sijaoga, maji ghetto yameisha, foleni ya maji yanayopatikana sijui inaanza lini na kuisha lini kila nikienda watu wanachota haijalishi ni saa 5 usiku au saa 11 alfajiri. Mtu anakuja na dumu 30 anapanga mstari na hawa ni wengi, sisi tumehamia hosteli kufua, vyoo na kuongea uko. Alafu nako ni foleni.
Nimepika jana mchana nikaja cheki maji ya kuoshea vyombo hakuna nikaviacha. Jioni nimeenda kula chips at least ndio vyakula vya kukaanga havina madhara sana maji yasipokuwepo ila nikakuta maji yanayooshea viazi ni machafu kuliko ambayo ningeoshea viatu.
Nikatoka zangu kuja kwa family relative mmoja mitaa ya Tabata ana visima nikaambiwa gari zinasomba maji kupeleka Masaki.
Miaka 60 ya uhuru, waliozaliwa tunapata uhuru ndio wanastaafu ila hatuna vyanzo vya uhakika vya maji kwenye jiji kuu la biashara na mji mkuu
Sasa utavuna maji ya mvua halafu uyatumie kufanyia nini kuoga au kuflush?!Wangapi wana uwezo wa kujenga system ya kuvuna maji, nyumba zenyewe vyumba vina ungwaungwa kama mabewa,Chumba cha kulala unajenga leo,sebule baada ya miaka mitano, mitano mengine unaongeza chumba kingine, baada ya mitatu stoo......... kuna wengine hawajui lini wata maliza kujenga nyumba zao.
JPM angekuwa hai angefanya nini na maji yapatikane na hiki kiangazi kilichopo nchi nzima?JPM alisema mtamkumbuka, mtamkumbuka tu... sio ombi! Pale samaki wenu watakapoanza kuoza kwa kukosa umeme wa mafriji, pale mtakapoanza kukosa maji ya kufanyia shughuli za kila siku...
Sasa hapo obei na masaki wanatumia mfumo tofauti??