Kumekucha Madawa ya Kulevya: Kina 'Masogange' wawataja waliowatuma!

Kumekucha Madawa ya Kulevya: Kina 'Masogange' wawataja waliowatuma!

.......Mimi hadi sasa hivi nazeeka kila siku nasikia sikia kuhusu mtoto wa raisi, hivi nae hajatajwa au katika mzigo huo hausiki yake anapeleka China tu?
unazeeka??? basi wewe ni mtoto wa <5 yrs. manake huyu katajwa zaid ndani ya hii miaka 5 na kuhusu china katajwa this yr.
 
japo siamini habar iliyopo hapo juu kwasababu ya chanzo na jinsi ilivyoandkwa lakin watanzania haya madawa tuyaangalie zaid, tushrkiane kwa pamoja bila kujali tofauti zetu za aina yoyote..Tanzania yetu itapotea, haya maziwa na asali tunayojivunia yatapotea, hii nguv kazi tunayoijenga itapotea na mwsho Tanzania itapotea. Hakutakuwa na viongoz na wananch bali watawala na watawaliwa...
 
Mmmmh kweli watu balaa wamegundua mbinu mpya ya kwamba ukitaka kuzima moto ni kupambana na moshi.kamwe hiyo kazi haitofanikiwa hata siku moja.wawaachie wakina masogange warudi kwenye chanzo kwa kina kinje na wengineo kazi itafanikiwa.
 
masogange waachiwe huru. Hawana hatia katika hili. Watakuwa wamewaonea kama wakiwahukumu. Hii nchi kila kitu ruksa. Wakubwa huwa hawaguswi kamwe! Pambafuuu!

hakuna kuachiwa sindo hao wanajifanya kuigiza tu mamilionea ------- zao funga miaka mia, si tunaangaika wao wanalala lkn wanaela
 
Na Mwandishi Wetu
IMEVUJA! Staa muuza nyago kwenye video za wasanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu za Kibongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ na shosti wake, Mellisa Edward kabla ya
kupandishwa kizimbani kwa msala wa dawa za kulevya ‘unga’ Afrika Kusini waliingizwa kwenye chumba cha mateso kwa saa 24 ili kutaja waliowatuma.

Habari kutoka kwa chanzo chetu kilichopo jijini Johannesburg nchini humo zilidai kuwa baada ya kukamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, walipelekwa polisi ambapo walichukuliwa maelezo.

Ilielezwa kuwa mwanzoni waligoma kueleza mzigo huo wa kilo 150 wa unga ulikuwa wa nani hivyo ikabidi polisi wa upelelezi watafute njia nyingine ya kuwalainisha kwa kuwabembeleza kuwa wakieleza ukweli wataachiwa.


MATESO SAA 24
Chanzo hicho kilisema kuwa baada ya mbinu hiyo kushindikana ndipo wawili hao wakaingizwa kwenye chumba maalum cha mateso ikiaminika kuwa watasema aliyewatuma.

USHUHUDA
“Unajua Sauzi (Afrika Kusini) huwa hawana utani na ishu za madawa ya kulevya. Jamaa (polisi) wana kila aina ya mbinu ya kumfanya mtu aeleze ukweli.

“Katika kutesa unaweza kuingizwa kwenye chumba maalum cha mateso ambayo nayo huwa yana steji zake.

“Kwanza utaanzia kwenye chumba kilichojazwa siafu wakubwa na huko unaweza usijue kuwa kuna siafu zaidi ya kuona kitu kama red carpet (zuria jekundu) kuanzia sakafuni, ukutani hadi kwenye dari, kumbe wale wote ni siafu.

“Wakishakuingiza mle ndipo utashangaa wale siafu wanacharuka na kuanza kukung’ata mwili mzima, zoezi hilo hufanyika kwa saa 24. Lazima useme ukweli.

“Kama bado ukijifanya mbishi au nunda ndipo unapelekwa hatua nyingine ya kulazimishwa kujisaidia haja ndogo kwenye waya wa umeme.

“Si unajua tena waya wenye umeme na maji vikikutana nini kinatokea? Lazima itatokea shoti ya kutisha kwani ule waya hufuata sehemu yale maji yanapotokea.

“Kinachofuata ni mtu kupigwa shoti kali ya umeme ambapo lazima utasema tu.

“Hicho ndicho kilichowapata akina Masogange kama wanavyofanyiwa Wabongo wengine wanaokamatwa Mitaa ya Rissik hapa Johannesburg.

WALIOWATUMA
“Baada ya mateso hayo, waliwataja waliowatuma mzigo huo wa unga aina ya crystal methamphetamine wenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8,” kilisema chanzo hicho ambacho ni Mbongo ambaye kwa sasa ni mkazi wa Mtaa wa Rissik, Johannesburg, wanapoishi Wabongo kwa kuungaunga aliyewahi kukumbwa na mkasa kama huo.

MTOTO WA KIGOGO ATAJWA
Habari za ndani zilidai kuwa baada ya kupitia mateso hayo, mabinti hao waliwataja watu wawili waliowatuma kusafirisha mzigo huo, mmoja akiwa ni mtoto wa kigogo ambaye ni mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania (jina lipo).

Ilidaiwa kuwa mtoto huyo wa mkubwa ni mjanja wa mjini ambaye alihusika kushughulikia kusafirisha mwili wa msanii Albert Mangweha ‘Ngwea’ aliyefia Johannesburg Juni, mwaka huu.

Ilivuja kuwa mwingine aliyetajwa na akina Masogange ni mfanyabiashara maarufu Bongo anayesafiri nje mara kwa mara huku jina la ‘mtoto wa mjini’ Mangunga likitajwa zaidi hata na Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison George Mwakyembe.

Gazeti hili lilipozungumza na Kamanda wa Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya, Godfrey Nzowa, alikiri kupewa majina hayo lakini akaliomba gazeti hili kutoyachapisha kwa sasa kuepuka kuvuruga ushahidi.

ULINZI KAMA SHEHE PONDA
Baada ya polisi wa upelelezi na wale wa kimataifa (Interpol) kujiridhisha na maelezo ya mabinti hao, walipandishwa kizimbani kwa mara ya pili Agosti 19, mwaka huu chini ya ulinzi mkali kama ule ‘anaowekewaga’ Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Shehe Ponda Issa Ponda anapofikishwa kwenye mahakama mbalimbali nchini kwa kesi zake za madai ya uchochezi.

WAPANDISHWA TENA KORTINI
Habari kutoka Sauzi zilieleza kuwa akina Masogange walipandishwa tena kizimbani hivi karibuni ambapo tayari kesi yao imeanza kuunguruma ikielezwa kuwa endapo watakutwa na hatia watakula mvua ya kifungo si chini ya miaka 10 kwa sheria za nchi hiyo.

Masogange na Mellisa walinaswa nchini humo Julai 5, mwaka huu wakiwa na mabegi sita yaliyokuwa na mzigo huo wa unga.
mtu wa kuulizwa hapo ni mkuu wa kaya je? waliotajwa ni sawasawa? maana yeye anawajua
 
Mi sioni kipya hp yote yasemwayo yanajulikana,Police,Tiss wote wanajua wauza unga wakubwa.Hawawezi kuwafanya lolote,wamo miongoni.
 
Yaani hapa inabidi wenye ma boutique wote wachunguzwe na wale wenye kampuni za clearing and forwarding wachunguzwe pia kwani wengi wao asilimia 98.9 ni wazungu wa sembe.
 
Biashara ya sembe imeshika kasi ya hatari,punda wamekuwa wengi balaa.
 
Mimi ninachoona hapo hata wakipewa adhabu ya kufa hao sio kwamba tatizo litakuwa limeisha, hivyo ni viji tawi tu, matawi makubwa na mashina yake hayaguswi sasa basi tutafute shina na si kwamba hayajulikani lahasha yanajulikana lakini nani wa kumvisha paka kengele, Tanzania hakuna shamba la unga lakini ndio wasambazaji wakubwa waunga je unatoka wap? Juzi juzi kakamata mchina mchana kweupe na mbeg mzima, jana tena yule Dada hapo hapo hamuoni km kuna chanzo? Na kwa nini wanakamatwa lakini bado wanapita? Inamaana wanaopita ni wengi kuliko wanaokamatwa!
Wito wangu kwa serikali isifanye masihala na swala hiki na wala wasidhani watakuwa kwenye hizo nafasi milele, km unachekelea kudhulika au kunyanyasika kwa mwenzako kesho itakuwa kwako.
Naamini km serikali ikiamua haishindwi. Ila kwa sasa imeamua kutishindana na wauza unga.

Sio mbaya sana kwan wakishugulikiwa ipasavyo wengine wanaosafirisha wataogopa. Hivyo biashara itadorora vigogo hawawezi kusafirisha mzigo. Na hakuna dogo mwingine atakayekuwa tayari kubeba hiyo cargo.
 
Mi sioni kipya hp yote yasemwayo yanajulikana,Police,Tiss wote wanajua wauza unga wakubwa.Hawawezi kuwafanya lolote,wamo miongoni.

Mkuu kuna wakati tunalaumu sana bila kuangalia. Hata hapa anatajwa Kinje, huenda yeye ni msimamizi tu wa biashara lakini kuna mfanyabiashara mwenyewe, angekuwa Kinje bila shaka angekamatwa. Polisi TISS na wengine wanajua kuliko tunayojua sisi, ni hadi wakubwa watakapoamua ndipo watu wa chini watatekeleza wanachoambiwa. vinginevyo tutaendelea kulalama tu kila kukicha.

As usual hakuna atakayekamtwa, sana sana wabebaji ndio watasumbuliwa kidogo, wataachiwa.
 
Hawa wanaosafirisha wanyongwe kabisa. Hii itasaidia hawa vigogo kukosa watu wa kuwabebea cargo zao....
 
kama serikali inataka kukomesha biashara hii haramu ya madawa ya kulevya, basi ismuonee aibu mtu kwa sababu ya umaarufu wake au nafasi yake katika serikali. Lazima itangulize usalama wa nchi kwanza na ihakikishe wahusika wote wanachukuliwa hatua stahiki.
 
Hivi huyo kinje pesa zote za Parking System za Dar city hazimtoshi hadi awafanye raia wengine Punda wa kubeba dawa za Kulevya? Mijitu iliyozaliwa kwa kula vya dezo ndio hadi ikikua inakuwa hivyo hivyo kupenda Dezo.....
 
mtu wa kuulizwa hapo ni mkuu wa kaya je? waliotajwa ni sawasawa? maana yeye anawajua

yaaan daaamie naichikia sana serikali yetu kwa kufumbia macho kwann wasiwajibishwe mapema hao wote wanotajwa mara moja sasa utashangaa eti tuunde tume iwachunguze wakat wametajwa daaa
PONGEZ ZANGU ZA DHAT ZIMWENDEE NDUGU MWAKYEMBE KWA HARAKAT NZITO ANAYOIFANYA BG UP JEMBEEE
 
Chini ya utawala wa hawa ma CCM,tutaendelea kucheza huu music wa watoto wa vigogo mpaka mwisho,hakuna yeyote atakayechukuliwa hatua kwa sababu ndo wafadhili wakubwa kwao;JK ana list ya wauza unga mda mrefu,lakini hakuna hatua yeyote ya kisheria iliyochukuliwa,tutakwisha,bora hata wameanza kudakwa na ukweli umeanza kujulikana taratibu,kuliko majina waliyoya'hold' kwenye meza zao
 
Back
Top Bottom