Kumfunga Maria jela miaka 22 kisa nyama ya swala ni matokeo ya kuwa na wanasheria waliokosa hekima na busara

Miaka 22 kwa nyama yenye thaman ya laki tisa?
Yaani unasema kweli, huyo mwana dada kakaa jela miaka 22?

Na, kosa lake ni hiyo nyama ya swala?

Na katika miaka yote hiyo, 22, hapakuwepo hata na KUDURUVU (Review); wala ile tume ya msamaha aliyokuwa akiiongoza Marehemu Mrema, haikuweza hata kumfikiria?

Mkuu 'Carlos', nimejikuta nashindwa kabisa hata kukupa 'like' tu ya taarifa ya namna hii, kwa sababu hakuna kitu cha 'ku-'like' kwenye dhuruma ya namna hii.

Nchi hii imechelewa sana kupata mapinduzi za kuondoa utawala wa namna hii!
 
Kuiondoa CCM madarakani. Na kwa bahati mbaya mpaka muda huu hakuna njia sahihi wala mpango wowote ule wa kueleweka, wa kuitoa.
Kuna njama CHADEMA zimefanyika kuzima matumaini ya waTanzania.
Viongozi wa chama hicho wanao kizima chama hiki hawatakuwa tofauti na wahaini wengine wote.
 
Ni hukumu ya kisheitwaaaani.
Mdogo wake rostam yuko uraiani anapeta na ameua maelfu ya tembo wetu, kinana kasafirisha twiga na sasa n mutu mukubwa huko lichama la kijani.
 
No way huyu mama anaweza winda swala,
 
Mahakimu hawako huru miyoyoni mwao,you cant be free if you judge people
 

Maelezo mrefu umeandika pumba, kumbe hata Tembo haujawahi waona. Nenda sehemu zenye changamoto hiyo waulize wakueleze.
 

Mahakama inazidi kuwakosanisha wananchi na Serikali.

Tunazo reference nyingi za matajiri na wanasiasa hasa CCM kukutwa nyara za thamani kubwa hasa meno ya tembo na mwisho wa siku waliachiwa huru, wapo watu walituhumiwa kwa ufisadi wa kutisha wakapewa kifungo cha nje na kufagia na wengine wapo nje tu.

Nchi ni hii hii tunaona kwahiyo chocheeni moto tu
 
Mdogo wake Rostam aliyekuwa mratibu wa ujangili wote hapa Tanzania alipigwa faini ambayo kwa utajiri wa familia yake unaotokana biashara haramu ni kama pipi tu.
 
Huyo hakimu ningekula sahani naye moja tuende wote kuzimu kama ningekua mtoto wa huyo mama pona yake ingekua tu bi mkubwa kushinda rufaa.
 
Yaani kila kilo 1 Mwaka 1 jela total 22kg/per 22 yrs sentence dah this is disgusting Ila dah nahisi kuchoka mama anahitaji huruma Jamani kwani swala wapo kwenye list ya extinction Jamani [emoji24][emoji24][emoji24]
sheria haina huruma
 
Hakimu achunguzwe, unaweza ukakuta amegushi vyeti.
 
Huku majizi na majambazi yakiendelea kula mema ya nchi. Its so sad Kwa kweli. Mkurungezi wa ATCL ameiba 71 bil anahukumiwa miaka 2 au fine ya Tsh 12 mil tu.

Hii nchi Kwa kweli Kuna mambo yanauimza Sana. Itafika sehemu watu wataanza kujitoa mhanga Kwa upumbavu huu aisee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…