Kumfunga Maria jela miaka 22 kisa nyama ya swala ni matokeo ya kuwa na wanasheria waliokosa hekima na busara

Kumfunga Maria jela miaka 22 kisa nyama ya swala ni matokeo ya kuwa na wanasheria waliokosa hekima na busara

Mbunge
nenda jela wewe kwa niaba yake km umemwonea huruma, mnafki mkubwa sheria ni msumemo haiangalii hali ya mtu. Sheria haijatungwa kwa maskini wala tajiri. Km we unajijua ni maskini tii sheria. Ufanye uhalifu halafu ndio uachwe kisa maskini? We kweli ni kenge tena mnafki tu unatafuta umaarufu wa kilofa.
Mbunge wa Kishapu alifungwa miaka mingapi vile nikumbushe?
 
Kuna kitu tunakosea sana kuhusu wanyama pori. Raia hawana elimu ya kuishi nao pale wanapoingia mazingira yao au wanyama wanapokuja mazingira yao.

Nadhani tunahitaji wataalamu wanaowafahamu hawa wanyama vema ili raia waweze kuelekezwa namna ya kuishi nao na kuweza ku:co exist.


Mnyama kama tembo akija eneo la makazi ya watu basi amepata harufu ya chakula kama mahindi, viazi, mihogo na kadhalika. So raia wanatakiwa kujua yule ni mnyama kitendo xha kumletea shari au kutaka kumfukuza itamlazimu kujitetea na ndipo hapo madhara hutokea.

Nimeshaona video ya tembo wanaokwenda kwenye hoteli ya kitalii na wapishi huwa wanaandaa mazaga wanawawekea hapo pembeni maana unawalifumua paa la jiko na ndipo hapo chakula wanaweka so wakija wanakula wakiwa wamesimama kwa nje na kupenyeza mikonge yao kwa ndani ya chumba cha jiko.

Imeshakuwa mazoea na hao tembo huwa wanakuja hapo mara kwa mara. Aiseee ukiwa muoga huwezi kukaa hilo eneo maana unakuta bonge la tembo linachungulia juu ya paa linaingiza mkonga wake kupapasa msosi. Halafu wanakuja kimya kimya.

Tembo anaweza pita nyuma ya jengo na usijue kama wapo nyuma ya nyumba hapo sasa tokea huko nyuma bila mahesabu utashangaa umempiga kikumbo. Me wakisema sehemu fulani tembo huwa wanapita au kuja sana huwa sishauri mtu aende hayo maeneo kama ana umakini mdogo maana ukizingua wanapita na wewe na kukudedisha ni dakika chache tu.
Hivi umekijua nilichoandika au umevurugwa na mvua?

Mtu analima shambani kwake unfortunately tembo anatokea anamuua, je , hapo inahitajika elimu ya kuishi na tembo?

Tembo wamekuwa wengi sasa wamewafuata wanadamu wanakula mazao ya watu huku waathirika wakilipwa fidia kiduchu tena kwa kuchelewa na wakati mwingine hulipwi.

Mjomba wangu kauwawa na tembo mchana kipindi yuko shamba analima. Tembo wavunwe au wauzwe ili kutuamini uhai wa watu.

Watu wanakufa serikali inatoa million 1 huku wewe ukiua tembo miaka 50 jela na faini sh. 50 ml.
 
Hii sio haki nilipoisoma hii habari Kwa Millard Ayo machozi yalinilenga walahi. Umasikini ni kitu kibaya Sana jamani hivi kweli wale waliokua wanaiba wanayamapori kwenda nje ya nchi wamefanywa nini?
Huyu hakimu aliyetoa hii hukumu ana vina Sana na shetani siamini kama ana Moto wa kibidamu
 
Hatafungwa kifungo hicho. Ila lazima umma utangaziwe maamuzi ya mahakama. Huyu atakwenda kukaa mahabusu kama wiki tu kisha atatoka ili next time awe makini na wanyama pori

Sheria ni lazima ziwe kali ili kuwalinda wanyana pori sababu tukicheka na hawa raia wadogo wanaozunguka mbunga miaka 10 ijayo wakiwekeza maisha yao kwa hao wanyama hamtaamini namna namna watawatokomeza pia usisahau swala la magonjwa ya mlipuko kutokana na kula nyama ambazo hazijathibishwa ubora wake.

Kwa kifupi tusiwe wepesi sana wa kuleta hisia katika maswala ya kisheria. Huu mchezo wa kuleta hisia ndio chanzo cha rushwa na utendaji mbovu wa mamlaka za serikali sababu wanainchi ndio mstari wa mbele kuwatetea wakosaji sababu wanatia huruma wakitiwa mbaroni.
Naamini huyo mama angekua ndugu yako usingeandika hizi pumba. Kama ni Sheria iwabane na wale wanaosafirisha wanyama kwenda ughaibuni sio mama masikini asiye na nguvu hata ya kuua sungura
 
umlinde binadamu mwenye akili zake, funga hata miaka 100, pumbavu kabisa. Na ujue wanyama ktk himaya yao ni bora kuliko we kenge mtu
Kaeni karibu na majority ya watanzania muone Wana upeo dini kiasi gani,elimu mmewanyima,elimu ya sheria hamuwapi,mmeshindwa kuwaondolea umasikini,mmeshindwa hata kuwapa huduma za wanasheria Bure,mnawafunga tu!!..watanzania wengi wajinga,hawajui kitu
 
Mahakama
Polisi
Vyombo hivi vimewekwa kuwanyoosha masikini havihusiki na watu wa daraja la 2 na 1
 
mnafki tu wewe
Wewe mbona unabwabwaja sana kwani wew ndiye hakimu uliemuhukumu mubibi wa watu!? Hoja siyo msumeno au mukisu wa sheria, hoja ni kwa nin vyombo vya dola vinashughulika wa watu wenye makosa madogo kama hayo ya mubibi wa watu na kilo tisa(9) za nyama ya swala ambayo hata haifiki thamani ya milioni moja huku majambazi makubwa yanayoiibia nchi matrion na matirion na fedha kama yalivyotajwa na CAG yakiendelea kuvimba mtaani huku yakitembelea V8 na ulinzi wa hali ya juu ukisindikizwa na ving'ora.
 
Mijizi ya CAG mnaiacha inadunda mtaani mnakuja kumfunga Mwanamke ambaye hata hakujua ni nyama ya nini, mwanamke ambaye hata huyo swala hasingeweza kumkamata, mwanamke ambaye pengine yeye na Familia yake wanalala chini, mlo mmoja, kaletewa nyama ya mbuzi auze kumbe ni ni swala, yeye ni mkemia mpaka ajue huyu ni Swala?

Miaka 22 kwa nyama yenye thaman ya laki tisa?

Kwamba kupitia hiyo nyama, angekuwa tajiri kama walivyo majizi yenu ya CAG?

Upumbavu, ufedhuli, ujinga, ukosefu wa Hekima na Busara aliouonesha huyu Hakimu unaadhihirisha aina ya Wanasheria uchwara tulionao hapa Nchini.

View attachment 2805999
Waarabu wanawaswaga hao swala bila kuchukuliwa hatua yoyote!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Mambo madogo madogo kama haya nadhani huwa yanatakiwa kumalizwa hukohuko eneo la tukio kabla hayajafika huko mahakamani au kwenye vyombo ya juu vya sheria.

Sitaki kuamini kwamba huyu mama angeonywa kwa faini aua ka adhabu nyingine inayoendana na kipato chake pamoja afya yake kwamba angegomea hiyo adhabu.


Some times sheria huwa zina kifungu cha kuangalia ubinadamu kwanza ndipo hukumu katili dhidi kosa kam hilo kutolewa. Anyway,Mungu akuongoze vyema huko gerezani mama mpambanaji🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom