Kumiliki nyumba au ardhi haviwezi kukupa utajiri bali vinalaza hela, fuatana nami ujifunze experience yangu ya umiliki wa hizi mali

Kumiliki nyumba au ardhi haviwezi kukupa utajiri bali vinalaza hela, fuatana nami ujifunze experience yangu ya umiliki wa hizi mali

Well said Mkuu
Najiuliza hiyo biashara ambayo unazungusha unapata faida ambayo ni mara mbili ya mtaji sipati jibu.

Kila biashara na tija na changamoto zake:
Ardhi!
Tija ya Ardhi inategemea na factor kuu tatu, location kwa maana market value ya eneo (Kata), location kwa maana ya mtaa ardhi ilipo na locality kwa maana sehemu gani ya mtaa (je ni beach plot! corner plot! au kinagusa barabara kuu maarufu). Ukifanya maamuzi sahihi kuhusu hili umetoboa. Kibiashara, villa ya vyumba 4 iliyopo Beach Masaki/Oysterbay ina thanani kubwa mara 50 zaidi kuliko kipato cha nyumba ya aina hiyo iliyopo bunju/kimara. ujanja upo katika kununua kiwanja na siyo kujenga. Hivyo hata ujenge jengo zuri kiasi gani kama ulikosea kununua kiwanja imekula kwako. Ndio maana Ubungo plaza, Dege Beach NSSF na Kijichi NSSF projects zimekuwa feilure kubwa kibiashara. Changamoto ya ya investment kwenye ardhi ni initial investment cost ni kubwa na return ni 10 -20 yrs. tija yake ni kuwa baada ya 10-20 ambapo mwenye nyumba huwa anaonekana kula super normal profit with minimum risk and management cost.

Biashara nyinginezo!
Biashara za kuzungusha zina faida na hasara katika muda mfupi. Uzuri wa biashara ya kuzungusha unaweza kuanza na na mtaji mdogo baadaye ukapanda na kuwa mkubwa ndani ya miaka michache (initial investment cost siyo lazima iwe kubwa). Changamoto zake ni pamoja na risk inakuwa kubwa kwa kadiri unavyofanya biashara yenye super normal profit, competition inaibuka na kuua profit kila unapopata mafanikio hivyo mafanikio always ni ya muda mfupi. Hivyo suala la kupata na kukosa vina uzito unaofanana. Ili ufanikiwe kwenye biashara ni sharti kufanya maamuzi sahihi katika wakati sahihi na utekeleze mipango kwa usahihi. Kwenye maamuzi na mipango ndipo panaposababisha faida au hasara, na ndipo panapofanya baadhi wafanikiwe na wengine washindwe. Biashara pekee ambazo zina faida kubwa sawa au zaidi ya mtaji uliowekeza ni illigal business mifano kutoa rushwa ili upewe sehemu nono ya mgodi ambapo inabidi uwadhurumu wananchi na serikali, dawa za kulevya n.k

Hivyo inaweza isiwe sahihi kusema kwa ujumla kuwa biashara ya kuzungusha ni rahisi au inalipa zaidi kuliko kuwekeza kwenye ardhi. Maamuzi na mipango ndio siri ya kutoboa! hivyo tufanye utafiti kabla ya maamuzi ili tufanikiwe.

Mungu atusaidie
Nikweli mkuu, ukitaka kuona hela mingi fanya maseto/kachumbari business yaani unafanya biashara nyingi tofautitofauti lakini moja haitatosha kukupa pesa mingi
Watu wengi wanapoteza ramani kwa kuwaza biashara yenye faida kubwa kitu ambacho sio sahihi
 
Ndio maana wazungu wengi hawajihangaishi kujenga.

Wazungu wengi ulaya na Amerika wanaishi kwenye apartments.

Pia wengi wana nunua nyumba na kulipa mortgage.

Wanao jenga ni wachache sana.

Wao muda mwingi ni kufanya kazi, wakipata fedha ni kula bata na kusafiri.

Waafrika ndio wanajihangaisha kujenga wakihofia eti watoto watalala wapi.

Kwa wazungu, mtoto akishafika umri wa kujitegemea anaenda kwenye apartment yake na yeye. Akapambane kulipa bills.
Sasa wewe wa Tandale unaleta mambo ya ulaya bongo?.Hatufanani nao hata nusu
 
Kuna kitu kikubwa mnoo mleta mada unakosea, umechanganya vitu viwili tofauti kwenye kapu moja.

Kujenga nyumba ya kuishi sio mbadala wa kufanya biashara, na kufanya biashara sio mbadala wa kumiliki nyumba. Watu wanafanya biashara ili kupata pesa za kuweza kumiliki nyumba za wao kuweza kuishi kwa raha, uhuru na uhakika leo, kesho na keshokutwa. Kuna muda unaweza kufikia wewe na jamii yako ukashindwa kufanya biashara (kwa sababu ya umri, afya nk) lakini bado ukahitaji kuishi kwa raha, furaha, uhuru na uhakika, na hilo litafanikiwa ukiwa na nyumba yako.

Jiulize hili swali, ukiweza kulijibu utakuwa umeelewa kitu. Unasaka pesa (kuwekeza au kufanya biashara) ili ukija kuzipata uzifanyie nini?
 
Kununua 2014, kuuza 2024
Siyo lazima iwe hivyo. Kuna kiwanja nilinunua mil 8 kwa jamaa alikuwa na uhitaji wa pesa ya haraka. Baada ya wiki 2 narudia wiki 2, akapatikana mteja wa 15mil.

Kuna Real estate broker alinunua eneo maeneo ya pugu kwa raisi kwa mil 100 watu wakamuona kichaa, jamaa alikata vipande ndani ya miezi mi3 akaviuza kwa zaidi ya mil 150.

Hilo biashara hakikisha una mziko wa kutosha, kisha kazi yako ni kudeal na watu wenye uhitaji wa pesa ya haraka. Wanauzaga kwa bei za kutupa. Kisha wewe uza ukiwa umerelax, utapata super profit mpaka wengine uwaone wamekuja mjini kudhurula
 
Utatunza milion mia kwenye laini
💯
Ni watu tu wanachukulia poa mitandao ya simu lakini unaweza kutunza mamilioni ya hela kwenye Mobile Money sio kwenda kusumbuana na bank kila kukicha mara ufike uambiwe mtandao upo chini mara foleni mara wakupangie kiasi cha kuchukua kana kwamba unaomba
 
Ni kweli kabisa Mkuu. Mfano ni Dodoma, sasa hivi viwanja vya mjini kati havikamatiki. Hata fremu za biashara ni bei mbaya sana. Uchaguzi wa sehemu ya kuwekeza kwenye masuala ya ardhi ni muhimu sana.
Ardhi ukiwa na subra utaona hela yake kwa vichaa wa hela za motomoto ambazo hazijapoa tunateseka sana kusubiri ndio tatizo letu lilipo
Kuna kitu kikubwa mnoo mleta mada unakosea, umechanganya vitu viwili tofauti kwenye kapu moja.

Kujenga nyumba ya kuishi sio mbadala wa kufanya biashara, na kufanya biashara sio mbadala wa kumiliki nyumba. Watu wanafanya biashara ili kupata pesa za kuweza kumiliki nyumba za wao kuweza kuishi kwa raha, uhuru na uhakika leo, kesho na keshokutwa. Kuna muda unaweza kufikia wewe na jamii yako ukashindwa kufanya biashara (kwa sababu ya umri, afya nk) lakini bado ukahitaji kuishi kwa raha, furaha, uhuru na uhakika, na hilo litafanikiwa ukiwa na nyumba yako.

Jiulize hili swali, ukiweza kulijibu utakuwa umeelewa kitu. Unasaka pesa (kuwekeza au kufanya biashara) ili ukija kuzipata uzifanyie nini?
Binadamu anasaka hela apate za kuboresha maisha na kufanya maendeleo
 
Hao wazungu Kama hawajengi wanaishi wapi? Kwenye nyumba zinazomilikiwa na real estate kwahiyo hiyo ndiyo biashara ya kijanja pata picha unamiliki gorofa pale posta au chanika stendi au mjiwowote sehemu iliyochqngamka swala la msingi ni location ya nyumba yako.
Donard Trump na Robart Kiyosaki ndio biashara zao hizo tafuta location yenye soko Jenga nyumba kula Kodi,
 
Hao wazungu Kama hawajengi wanaishi wapi? Kwenye nyumba zinazomilikiwa na real estate kwahiyo hiyo ndiyo biashara ya kijanja pata picha unamiliki gorofa pale posta au chanika stendi au mjiwowote sehemu iliyochqngamka swala la msingi ni location ya nyumba yako.
Donard Trump na Robart Kiyosaki ndio biashara zao hizo tafuta location yenye soko Jenga nyumba kula Kodi,
💯
 
Kuna assets ambazo hazishuki thamani mfano ardhi!"anyway kila mtu anacho kipaumbele chake,,,,, ! Kuna mtu anahonga mademu alafu mama yake mzazi hana sukari ya chai,,, ! Huyo anaehonga anaona utelezi ni wa maana kuliko mzazi,,,, Same scenario na hoja yako, kila mtu ana kipaumbele chake !
Ardhi huwa pia inaweza ukashuka thamani, mfano serikali ikidesignate sehem iliyo karibu na ww kuwa mayb Dampo la jiji, au sehem ambayo inapatwa na majanga mara kwa mara kama kujaa maji , tetemeko la ardhi nk…huwa ardhi inaweza kushuka thamani ingawa ni mara chache
 
Nahisi kuna siri au kitu fulani kilimiss kwenye mfumo wako. Kuna password fulani uliikosa. Je kwanini matajiri wengi wa kibongo wana viwanja vingi. Unakuta tajiri ana viwanja 20 au 70 hadi 100+ anajenga nyumba, fremu,stoo,maduka, shule n.k nahisi kuna siri fulani uliikosa kwenye mfumo wako wa kimaisha na kibiashara. Labda kuchagua kiwanja au matumizi ya kiwanja au kwenye mikopo ya benki uliikosa password fulani
Yuko sawa nimjibie hili...hivyo anavyoviita asset ukweli sio asset...NI luxury liability...asset NI mpaka pale vinapoanza kuongoza hela...ardhi inatunza dhamani ya hela uliyonunulia sio inapanda dhamani kwa utafiti lakini...inapanda dhamani pale demand inapopanda na Kuna some rare case inapoteza dhamani.. mf.. sehemu kulikuwa na mradi Fulani Kama nzega palipokuwa na mine viwanja vilipaa Bei Ila Sasa mgodi umefungwa viwanja vipo chini sana pamoja na nyumba zipo chini sana...misigiri ilipokuwa onatumika barabara moja kabla ya manyoni tabora kufunguliwa palikuwa na demand kubwa ya nyumba na viwanja kuliko ilivyo leo..
Nyumba inashuka thaman sana kuliko eneo...Kuna watu wananunua nyumba Ila wanatagert eneo...hao matajiri unaosemea wanahifadhi hela ya ziada kwenye maeneo sio unachukua hela ya mtaji kununua ardhi NI kujipiga Pini....au hela ya mtaji kujengea nyumba ya kuishi...Bora ingekuwa ya biashara frem au lodge..
 
Ardhi huwa pia inaweza ukashuka thamani, mfano serikali ikidesignate sehem iliyo karibu na ww kuwa mayb Dampo la jiji, au sehem ambayo inapatwa na majanga mara kwa mara kama kujaa maji , tetemeko la ardhi nk…huwa ardhi inaweza kushuka thamani ingawa ni mara chache
Labda utupe mfano uliowahi kutokea.
 
Back
Top Bottom