Ngambo ipi tufafanulieSio tu bongo hata N'gambo hakuna Uhuru wa habari.....
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ngambo ipi tufafanulieSio tu bongo hata N'gambo hakuna Uhuru wa habari.....
Kufuatia sakata la picha liyopigwa ikionesha wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sinde wakiwa wamekaa wakisoma chini bila madawati na Serikali ikionekana kung'aka kwa kumuweka ndani anayesemekana kupiga picha hiyo ni sawa na mbuni kujifunika kichwa huku mwili ukiwa nje na akidhani kajificha. Soma Mbeya: Mwalimu aliyesambaza picha za Wanafunzi wamekaa chini, aingia matatani
![]()
Kwa Tanzania hii siyo Sinde pekee ambayo watoto wanasoma wakiwa chini bila madawati hivyo hata serikali ikijaribu kumtoa kafara huyo mpiga picha na raia mwema ili iweze kuficha aibu yake ni sawa na bure kwa kuwa ukweli ni kuwa hali hiyo ipo kwa shule nyingi nchini japo makujwaani mnajinadi kuwa mmeboresha mazingira ya elimu ila ukweli ni kuwa watoto wanasoma katika mazingira magumu sana.
Turudi Sinde, imeonekana baada ya Viongozi kufika hapo shuleni madawati yalikuwepo darasani hivyo kuonekana huyo mpiga picha anayedaiwa kuwa ni mwalimu wa shule hiyo alizusha ili kuleta taharuki.
Najiuiliza nani anadanganya kati ya Mwalimu na Serikali?
Baada ya sinema hii nini kitajiri, iwapo Serikali itafanikiwa katika hili basi ni wazi watu wataingia ganzi kufichua madhaifu au uovu wowote hata unaoonekana kwa macho na kufanya jamii ibaki katika giza na maumivu ya kuishi na uduni kwa kuwa ukisema inabadilishwa na unakuwa mhalifu na kushikwa na polisi.
- Je, Mwalimu alitoa madawati na kuwaamuru wanafunzi wakae chini ili apige picha asambaze uongo?
- Je, baada ya Serikali kuona taarifa imefika kwa wananchi wakaweka madawati ili waweze kukanusha taarifa ya awali ionekane alizusha na aadhibiwe ili kuwatia hofu wengine wasifichue maovu?
Iwapo Mpiga picha au picha ikaweza kuthibitisha kuwa ni kweli walikuwa wanakaa chini kwa kukosa madawati basi ni wazi Serikali itapata aibu na itakuwa imejishushia zaidi heshima na kufanya hata ikiwa wanakanusha kitu hata kama ni kweli kilizushwa jamii ione wanadanganya kama ambavyo imekuwa hapo zamani.
Leo tukisema kila shule ilete takwimu za watoto wanaokaa chini au picha nchini hapa Serikali itaweka ndani nchi nzima kwa kuwa ni nyingi na si Sinde pekee, au kwakuwa anatoka Spika wa bunge ndio maana Serikali imeona haifai taarifa hii itoke kwa umma? Shule nyingi hazina madawati japo tumejaza misitu na tunajimwambafai kuupiga mwingi katika elimu.
Badala ya Serikali kuhangaika na watoa taarifa kuwakamata iboreshe shule zote kwa kuhakikisha zina miundombinu inayotakiwa kuanzia madawati, vyoo, madarasa na vifaa vya kufundishia kwa kuwa naamini uwezo huo upo ila havifanyiki kwa kuwa hakuna anayeona maumivu ya mtoto wa kitanzania kukaa chini kwa kuwa watoto wa wenye mamlaka hawasomi shule za Serikali.
Pia soma:
Mwongo mkubwa wewe! 1977 darasa moja lilikuwa na wanafunzi wasiozidi 45 na serkali ilihakikisha madawati, meza na vitu vya kukalia walimu vipo muda wote! Hiyo shule uliyosoma wewe hapo Kinondoni haikuwahi kuwa na upungufu wa madawati kwa mwaka huo. Tafuta uongo mwingine!1977 nilitumia darasa kama hilo!
Halafu Waziri ana gari la milioni 600.
Refer awamu ile ndo walileta hii mamb ya Kivuli cha mzalendo ili wapige vzrMzalendo ndio nani wanaosema ukweli au wanaibia nchi??
Mzarendo kweri kweri nimeflahi sana nasema uongo ndugu zangu??Refer awamu ile ndo walileta hii mamb ya Kivuli cha mzalendo ili wapige vzr
Ndio maana mkoloni alitutawala vibaya kabisa, hamna shule hapo, hilo ni pango la panya katikati ya shamba la mahindi…Shule ya Msingi Muyombo Kata ya Lwamgasa Busanda Geita wanafunzi wakiwa wamekalia madawati ya kisasa kabisa
View attachment 2510173
Tukisema Sukuma Gang nyie mataahira mnasema mnatukanwa, lakini kwa post hii na thread husika ni dhahiri nyie wote mna mtindio wa ubongo. Hamna uwezo wa kujibu hoja yoyote au sijui ni uvivu wa kusoma na kuelewa hoja iliyopo mezani mnakurupuka kuihusisha Chadema na mada ambayo haiwahusu.CHADEMA mlisema amekufa Magufuli haya hayakuwepo tena nchi imetulia
USSR
Mleta mada hauogopi kukamatwa?watoto wa wenye mamlaka hawasomi shule za Serikali
Halafu kwenye NECTA mnatangaza eti shule inayoongiza ni FEZA, kwa usawa upi kwa kupewa elimu?
AbroadNgambo ipi tufafanulie
Where abroad please be specificAbroad
Asiye jua maana haambiwi maana....misemo ya wahenga....Where abroad please be specific
Kwa maoni yangu watu wote au walimu wote ambao wanafundisha shule zote ambazo baadhi ya wanafunzi wanakaa chini ni busara sana na wao wakapiga picha na kutuwekea hapa ili jamii ione, na nafikiri ndio njia mojawapo sahihi pia ya kumsaidia mwalimu aliyejitoa mwanga.Kufuatia sakata la picha liyopigwa ikionesha wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sinde wakiwa wamekaa wakisoma chini bila madawati na Serikali ikionekana kung'aka kwa kumuweka ndani anayesemekana kupiga picha hiyo ni sawa na mbuni kujifunika kichwa huku mwili ukiwa nje na akidhani kajificha. Soma Mbeya: Mwalimu aliyesambaza picha za Wanafunzi wamekaa chini, aingia matatani
![]()
Kwa Tanzania hii siyo Sinde pekee ambayo watoto wanasoma wakiwa chini bila madawati hivyo hata serikali ikijaribu kumtoa kafara huyo mpiga picha na raia mwema ili iweze kuficha aibu yake ni sawa na bure kwa kuwa ukweli ni kuwa hali hiyo ipo kwa shule nyingi nchini japo makujwaani mnajinadi kuwa mmeboresha mazingira ya elimu ila ukweli ni kuwa watoto wanasoma katika mazingira magumu sana.
Turudi Sinde, imeonekana baada ya Viongozi kufika hapo shuleni madawati yalikuwepo darasani hivyo kuonekana huyo mpiga picha anayedaiwa kuwa ni mwalimu wa shule hiyo alizusha ili kuleta taharuki.
Najiuiliza nani anadanganya kati ya Mwalimu na Serikali?
Baada ya sinema hii nini kitajiri, iwapo Serikali itafanikiwa katika hili basi ni wazi watu wataingia ganzi kufichua madhaifu au uovu wowote hata unaoonekana kwa macho na kufanya jamii ibaki katika giza na maumivu ya kuishi na uduni kwa kuwa ukisema inabadilishwa na unakuwa mhalifu na kushikwa na polisi.
- Je, Mwalimu alitoa madawati na kuwaamuru wanafunzi wakae chini ili apige picha asambaze uongo?
- Je, baada ya Serikali kuona taarifa imefika kwa wananchi wakaweka madawati ili waweze kukanusha taarifa ya awali ionekane alizusha na aadhibiwe ili kuwatia hofu wengine wasifichue maovu?
Iwapo Mpiga picha au picha ikaweza kuthibitisha kuwa ni kweli walikuwa wanakaa chini kwa kukosa madawati basi ni wazi Serikali itapata aibu na itakuwa imejishushia zaidi heshima na kufanya hata ikiwa wanakanusha kitu hata kama ni kweli kilizushwa jamii ione wanadanganya kama ambavyo imekuwa hapo zamani.
Leo tukisema kila shule ilete takwimu za watoto wanaokaa chini au picha nchini hapa Serikali itaweka ndani nchi nzima kwa kuwa ni nyingi na si Sinde pekee, au kwakuwa anatoka Spika wa bunge ndio maana Serikali imeona haifai taarifa hii itoke kwa umma? Shule nyingi hazina madawati japo tumejaza misitu na tunajimwambafai kuupiga mwingi katika elimu.
Badala ya Serikali kuhangaika na watoa taarifa kuwakamata iboreshe shule zote kwa kuhakikisha zina miundombinu inayotakiwa kuanzia madawati, vyoo, madarasa na vifaa vya kufundishia kwa kuwa naamini uwezo huo upo ila havifanyiki kwa kuwa hakuna anayeona maumivu ya mtoto wa kitanzania kukaa chini kwa kuwa watoto wa wenye mamlaka hawasomi shule za Serikali.
Pia soma: