Uchaguzi 2020 Kumkata Paul Makonda kwenye Kura za Maoni CCM, siyo maamuzi yenye akili

Uchaguzi 2020 Kumkata Paul Makonda kwenye Kura za Maoni CCM, siyo maamuzi yenye akili

Hatutaki wabunge ambao CV zao zina utata. Hii ni 2020 (karne ya 20) siyo 1990 (karne ya 19) ambao watu kama Kihiyo walioghushi elimu zao. Bahati mbaya pamoja na mapugufu mengi ya kijana huyu hakuna mtu mwenye ubavu wa kukata jina lake!
 
Unamharibia kijana wetu. Itachukuliwa km unampigia kampeni kabla ya kipyenga kupulizwa, na wengine wanaweza kudhani kuwa amekutuma, na hivyo umemtia doa. Kila kitu kwa wakati wake, CCM ya sasa ni makini sana.

Nimejaribu kueleza umuhimu wa Makonda kwa siasa za sasa nchini kwetu
 
Hayo ni mawazo yako ukiona shida saana mpe ubunge kwako kisha umpe uwaziri kwa familia yako.
CCM ina utaratibu na sio watu kuwaza vyeo tu, hayo mawazo yako ndo yalihalibu chama huko nyuma.
Kama atachaguliwa si lazima awe waziri, kwa kuwa hata huo ubunge anaweza kutumikia watu na kuwapa maendelei bila kuwa waziri.


Hata haya ni maoni yako Boss, ahsante kwa mchango
 
Tutaona na

Tutaona na kusikia Fasihi nyingi tata kama hii,walioilewa fasihi hii kutoka kwa Taikon wanaweza kufafanua.Nimesoma bila kuelewa kuwa wewe ndiye Makonda,unamfanyia kampeni ya kumsifia na kumponda kwa wakati moja?


Kuandika ni jukumu langu, kuelewa namuachia msomaji Mkuu
 
Una matatizo makubwa .
Unaandika utafikiri hilo jimbo halina mwenyewe.
Dr Ndugulile yupo.
Makonda arudi kuomba Ukuu wa Mkoa amekuwa akiteuliwa siku zote.
Tunataka ateuliwe Balozi wetu Marekani.


Mkuu, nilichoandika ni sehemu ya sifa za Makonda. Ni Muhimu kuzisoma na kuzitafakari
 
Yote ni kweli kwa yale tunayoyaona lakini upande mwingine tusioujua hasa hili la kuwekewa vikwazo na Taifa kubwa kama Marekani na ambalo hajatoka hadhani kulitolea maelezo.Kwangu mimi naamini Makonda hawezi kufutika kwenye siasa kirahisi as long as JPM yupo madarakani lakini kwa ubunge nahisi hafai kutokana na arrogance.


Hata ingekuwa ni wewe, mtu ajipendekeze kwako, awe mtii kwako alafu usimpe upendeleo. Inawezekana kweli?
 
Back
Top Bottom