Kumuona Kuhani Mussa wa Kimara kwa haraka ni Tshs Laki 2

Kumuona Kuhani Mussa wa Kimara kwa haraka ni Tshs Laki 2

Ukifika pale Temboni unataka kumuona Kuhani Mussa Richard, kuna dau kama ilivyo kwa manabii wengine ila jamaa kaongeza kitu kinaitwa FAST TRACK. Hiyo ukitoa haina foleni, ile unamaliza kuhesabu pesa tu huyu hapa anakufanyia maombi.

Ila msisahau kubeba pesa za kununulia vifaa vya kiroho ambayo pia vina grade zake. Kuna vya matokeo ya papo hapo, na vile vya gradually Yaani mdogo mdogo.
we jamaa!!!!!
 
Mkuu, Imani yangu ni level za juu, siongei kwa hisia Nina nguvu za Rohoni...

Naweza kuona kuwa huyu ni Nabii feki au sio...

Hata wewe tukikutana na wewe nakujua mpaka ukoo wako...

Huna mamlaka ya kumuita mtu Wakala wa Ibilisi wakati hujapima Roho kwa njia ya Roho Mtakatifu
Una uhakika gani kuwa nguvu hizo za rohoni mwako hazina uhusiano na Lucifer? Yule baba wa Roho za Giza?
 
Ukifika pale Temboni unataka kumuona Kuhani Mussa Richard, kuna dau kama ilivyo kwa manabii wengine ila jamaa kaongeza kitu kinaitwa FAST TRACK. Hiyo ukitoa haina foleni, ile unamaliza kuhesabu pesa tu huyu hapa anakufanyia maombi.

Ila msisahau kubeba pesa za kununulia vifaa vya kiroho ambayo pia vina grade zake. Kuna vya matokeo ya papo hapo, na vile vya gradually Yaani mdogo mdogo.
Utapeli tu huo.
 
Ndo hivyo wajinga ndio waliwao..na siku ya jumapili ukipita pale nje temboni kuna watu kibao wako na bahasha wanagawa huruhusiwi uende kanisan kwake bila kuwa na bahasha uweke hela yaani pale bahasha kwanza ndio kiapumbele.
Sasa kinachonisikitisha sijawahi ona gwajiama au mwamposa au huyo mwasha labda akishiriki ibada ya kuzika labda kafa muumini wake haijawahi tokea.
Ukifa utajijua mwenyewe.
Ukionewa huruma sana utazikwa na Chawa wake, hapo uwe maarufu kidogo na zaka utoe za kutosha ndipo uzikwe na chawa
 
Aiseeee ..bora wewe umesema umeshawai kwenda ! Shida ni wengine kusema hawajawai gusa uko kote…….
Watu ni wanafiki. Sema wanaume wengi hawaendi kwa waganga ukilinganisha na wanawake. Wanawake wanaenda sana kwa waganga kuloga kwa mambo mengi. Kuloga waume zao ndo jambo kubwa zaidi. Inashauriwa mwanaume kwenye familia uwe mchawi zaidi ya mkeo au uwe mcha Mungu zaidi ya mkeo. Ukiyumba lazima utajuta baadae kwasababu wanawake kwenda kukuloga ni rahisi sana.
 
Namaanisha kuwa hawa wauni wanaibia watu mchana kweupe wakisingizia kuwa wanamhubiri/tangaza Yesu ambaye aliwakataza wasitoze watu pesa.
Unfortunately utapeli wao uko wazi hawamuhubiri Yesu maana wangekuwa wanamtangaza Yesu kwanza wangeacha uzinzi pili wangeacha kutoza watu pesa kwa mgongo wa vifaa vya kiroho.
Shenzi kabisa
Hua najiuliza mtu unaambiwa toa sadaka utabarikiwa Hali yakua ww Maisha magumu kwan sadaka zenyew hua zinapelekwa wapi nachojua sadaka ni utoe kwa wasiojiweza ,mayatima na kwengine lkn sio ya uhaini kama ivi 😂
 
Mkuu, Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo ni Mungu Mkuu kuliko miungu yote unayoijua wewe, anaweza tatua changamoto yako chini ya sekunde, ila ana kanuni zake: Mwamini Yesu Kristo na uishi maisha matakatifu. Yeye ameweka free-will, halazimishi mtu ila ukifa hatokuwa na huruma na wewe maana ulikataa maarifa na atakukataa wewe usiingie Mbinguni.
Eti mungu anaweza kutatua shida zako ndani ya sekunde!


Mamia ya wagonjwa walioko Muhimbili mbona hatujaona wakitatuliwa shida zao ? Au wote hawaishi katika huyo kristo ?


Kwanini huyo mungu wa Yakobo hakuzuia Hamas Wasiende kuvamia Lile tamasha la muziki pale Israel na wakaua watu 200 on sport siku ile tarehe 7 October 2023
 
Ukifika pale Temboni unataka kumuona Kuhani Mussa Richard, kuna dau kama ilivyo kwa manabii wengine ila jamaa kaongeza kitu kinaitwa FAST TRACK. Hiyo ukitoa haina foleni, ile unamaliza kuhesabu pesa tu huyu hapa anakufanyia maombi.

Ila msisahau kubeba pesa za kununulia vifaa vya kiroho ambayo pia vina grade zake. Kuna vya matokeo ya papo hapo, na vile vya gradually Yaani mdogo mdogo.
Mganga wa kienyeji?
 
Back
Top Bottom