Kuna delutional theory imesambaa kwenye jamii zetu za kiafrika kwamba kuoa kunafungua milango ya mafanikio

Natafuta Ajira

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
9,016
Reaction score
24,650
Kuna delusional theory imesambaa kwenye jamii zetu za kiafrika kwamba kuoa kunafungua milango ya mafanikio kwa mwanaume. Kwa kijana yoyote wa kiume kama wewe ni muumini wa iyo nadharia basi leo nakufungulia code kwamba umedanganywa.

Vijana wengi mmejazwa uongo vichwani mwenu kwa kuaminishwa kwamba mafanikio yenu yatapatikana kwenye ndoa. Sikiliza kijana, kabla ya kuoa ndio muda unaotakiwa kufungua milango ya mafanikio yako, huo ndio muda wa kufurahia maisha na uhuru wako kwa sababu ukioa hautapata iyo nafasi.

Kuoa ni kujivalisha minyororo ya utumwa, na katika kutimiza utumwa huo ipasavyo jamii na mamlaka za kiserikali zitakua macho kuakikisha hautoki nje ya mstari. Jaribio lolote la kujitoa kwenye utumwa huo matokeo yake ni jela au kufilisika.

Ndoa haimuongezei mwanaume chochote chenye thamani, tofauti na mwanamke ambae kwake ndoa ni ajira ya kudumu, ni mradi wa kibiashara na njia rahisi ya kuwa entitled kwenye mali za mwanaume bila kuchangia chochote kifedha au kitaaluma.

Takwimu zinaonesha 92% ya wanawake mabilionea wamepata utajiri wao kupitia talaka. Waliolewa na wanaume matajiri, wakadai talaka, wakapata mgao wa mali.

Hakuna mwanamke anaekuja kwenye maisha yako na solutions za changamoto zako au kukuwezesha kuyapata hayo mafanikio unayoambiwa utayapata ndoani. Siku zote mwanamke anakuja kwenye maisha yako ili wewe umpe suluhisho la matatizo yake na umfanyie kazi ili yeye aweze kuishi maisha rahisi kadiri iwezekanavyo.

Mwanamke hatafuti mpenzi, anatafuta mtumwa. Anataka mtumwa atakae gharamia lifestyle yake, atakaelipa bills zake na kusuluhisha matatizo yake yote hapa duniani.

Huyu mtumwa anapata nini in return? nothing beneficial, ni hasara, maangaiko, maumivu na majuto tu, kwa sababu huyu mwanamke hana chochote chenye thamani cha kuleta mezani. Mwanaume kataa kuwa mtumwa.

Mafanikio ya mwanaume ni mchakato wa nidhamu, jitihada, vikwazo na muda, sio ndoa. Mwanamke utakaemuoa hatokupa hela ya mtaji wa biashara au connection ya kazi nzuri zaidi ya uliyonayo, isipokua atakuongezea stress na gharama za maisha tu.
 
Maisha ni 50/50
Wapo watakaofanikiwa na wapo watakaopoteza cha muhimu cheza karata zako vizuriiii .... pata maarifa .. andika mali kwa majina ya watoto ama familia ... ongeza hekima na weka akiba yako binafsi (me & ke) pasipo tatizika
 
Kama sijakosea, Nafikiri hili bandiko ni la Kampeni ya Kataa ya Ndoa.
 
Team "punyeto" wanazidi kupata credit
 
Kuto Kuoa ama Kuoa hakuwezi kukufanya ufanikiwe ama ushindwe.

Japo Kuoa Kuna nafasi kubwa sana za kukufanya Ufanikiwe.

~Unapooa, kama hujanunua kiwanja utaanza kufikiria kununua na kujenga
~Utaachana na kubadirisha Wanawake, hivyo utakuwa na nafasi ya kutulia na Mwanamke mmoja ambaye mtafanya naye maisha
~Kama ulikuwa na kawaida ya kukesha Baa, Unapooa lazima utaacha hiyo tabia hivyo kukufanya upate muda mwingi wa kujiuliza na kutafakari kuhusu maisha na kuja na mawazo mbadala ya kufanya kuongeza kipato
~Unapata heshima tofauti na ukiwa single, hivyo ni rahisi kuaminiwa Kwa nafasi mbalimbali Kazini hata biashara. Nafasi ambazo zinaweza kukuongezea kipato n.k

Vijana oeni Kwa mustakabali wa maisha yenu ya sasa na baadaye
 
Hizo points zote mtu makini na aliye serious na maisha anaweza kuzifanya hata akiwa single.

kama hivyo vitu kuvifanya ni mpka uoe basi utakuwa una tatizo mahali. Na unaingia nalo kwenye ndoa.
 

Waafrica tunaenda kinyumenyume tu kila kituπŸ˜›
 
Jichanganye uoe bila kujipanga🀣🀣🀣🀣🀣
 
Mimi naona kuoa sio tatizo, tatizo lipo kwenye sheria kandamizi upande wa mwanaume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…