robert sendabishaka
JF-Expert Member
- Dec 11, 2015
- 3,111
- 3,294
Ninapohudhuria misa za maziko kwa dhebu la mtoa mada napata hasira. Ati baada ya kuaga mwili wanaweka kikapu cha sadaka ya kumuombea marehemu (hii kiongozi aliyeendesha misa anaondoka nayo), kisha kinakuja kikapu cha rambirambi.Kuna ile ya kuwataka waumini waliofiwa na wapendwa wao eti watoe sadaka kubwa kubwa kadri wawezavyo kama kikokotoo cha kuwawezesha hao wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki kupata ahueni ya maisha huko kaburini. Yaani mimi hii haijawahi kuniingia akilini kabisa.
imetabiliwa watu watapenda pesa kuliko kitu chochoteLeo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.
To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.
Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.
Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.
Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?
Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.
Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.
Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.
Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?
Tumsifu Yesu kristu.
Ukifiwa,ukitaka kubatiza,kuoa au kuolewa hupewi huduma mpaka michango ya nyuma ukamilisheUzuri wake ni kuwa usipotoa si kosa la jinai.
Usisahau kanisani muhimu kuliko yote huwa tunafuata neno, sasa haiwezekani injili ihubiriwe dakika 20 halafu misa itumie masaa karibu matatu kuendesha harambee ndani ya kanisa.Usilalamike sana, chukua hatua zifuatazo.
1. Acha kutoa hizo sadaka (michango), au toa ile inayokugusa tu, mingine kaa kimya, hakuna mtu wa kukufanya lolote.
2. Tafuta chenji za kutosha ukiwa unakwenda kanisani. Kama ukikuta sadaka za kutoa ni tano na wewe ulipanga kutoa sadaka ya jumla ya shilingi mia tano tu, basi chenji hiyo mia tano ili kupata sarafu za mia mia ziwe tano, kisha kila ukitakiwa kutoa sadaka unadondosha jiti tu kwenye chombo cha sadaka.
Chief mbona vitamu vipo vingi sana na vinaruhusiwa ndani ya dini ya kiislamu....unaweza ku giveup kitimoto na still uko fine tu! Karibu kwenye uislamuOna waislam duniani kote wanajijua Kuna wale wajahidina na wasio wajahidina hata uende wapi duniani ukikuta muslam atakuwa kundi moja hapo ndio maana warabu wanawajengea misikiti, mda huu wa mwezi mtukufu Kuna misikiti Kila siku inatoa pesa kwa watu wasiojiweza kwenda kununua futari umeona hapo kwanini hawajaingiza ubinafsi na umimi kwenye Imani njoo kwetu Sasa
Kanisa la masanja mkandamizaji
Kanisa la mc pilipili
Kanisa la gwajima
Kanisa la mzee wa upako
Kanisa la mwamposa
Kanisa la kakobe
Na bado Kuna utitiri wa makanisa na bado wanapigana vijembe unasali wapi wewe ukisema kwa MC pilipili wanaanza kusengenya njoo uku yani
ingekuwa kula kitu moto inaruhusiwa uslam unaenda uko sema kiti moto kuacha dah ngumu, maana nishaionja Sasa kuacha ngumu
The same guy loved Africa and was born there but hated Africans. He was a racist and a Hindu."I love christianity but I hate Christians"....Gadhi.
Hapo kwakweli hawajafanya vizuri.Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!
Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.
Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!
Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
Mhh... hilo limetokea wapi ? Ushahidi tafadhaliSiku hizi mamilooo, usipotoa ni kosa kwani wanaangalia registaa, hivyo huduma za kikanisa kama vile ubatizo, ndoa nk haupati.
Huku uchaggani picha linaanza kwanza Padri anaheshimika Kama mungu.Kweli michango imezid na inakera. Unatoa sadaka kabla hata kanisani hujafika na kabla hujashiriki mtiririko mwingine wa ibada.
Japo siwez hama kwa hizo sababu lakin inabid warekebishe mahali wanatukwaza waumini.
Kama hauamini kwamba utapata ufalme wa Mungu kanisani basi taka sana kuzifahamu kazi za roho mtakatifu. Yesu Kristu Katika mafundisho yake neno kanisa alilitaja mara moja tuu RejeaNikisema nifuate ushauri wako na kufuata kanuni za Mungu basi hata sadaka ninayotowa sasa hivi hawataipata nitapeleka direct kwa yatima na wajane na kanisani sintokanyaga tena.
Siendi kanisani kuutafuta ufalme wa mbinguni haupatikani pale, nakwenda kanisani kuwa connected na jamii yangu ambao tunaamini katika kristu.
Mimi siamini katika kuuona ufalme wa mbinguni kwa kwenda kanisani au kunipa maandiko ili kuhalalisha uharamia wenu?
Mbona maandiko mnachaguwa ya kutumia wakati Timotheo wa pili imeandikwa wazi atamaniye kazi ya uaskofu basi atamani kazi njema, basi imempasa Askofu awe mume wa mke mmoja, sasa mbona kanisa katoliki limekumbatia useja kinyume na mafundisho wa biblia?
Ninapohudhuria misa za maziko kwa dhebu la mtoa mada napata hasira. Ati baada ya kuaga mwili wanaweka kikapu cha sadaka ya kumuombea marehemu (hii kiongozi aliyeendesha misa anaondoka nayo), kisha kinakuja kikapu cha rambirambi.
[emoji23][emoji23] haya masihala sasa mtani. Kiingiacho halimtii mtu najisi bali kitokachoOna waislam duniani kote wanajijua Kuna wale wajahidina na wasio wajahidina hata uende wapi duniani ukikuta muslam atakuwa kundi moja hapo ndio maana warabu wanawajengea misikiti, mda huu wa mwezi mtukufu Kuna misikiti Kila siku inatoa pesa kwa watu wasiojiweza kwenda kununua futari umeona hapo kwanini hawajaingiza ubinafsi na umimi kwenye Imani njoo kwetu Sasa
Kanisa la masanja mkandamizaji
Kanisa la mc pilipili
Kanisa la gwajima
Kanisa la mzee wa upako
Kanisa la mwamposa
Kanisa la kakobe
Na bado Kuna utitiri wa makanisa na bado wanapigana vijembe unasali wapi wewe ukisema kwa MC pilipili wanaanza kusengenya njoo uku yani
ingekuwa kula kitu moto inaruhusiwa uslam unaenda uko sema kiti moto kuacha dah ngumu, maana nishaionja Sasa kuacha ngumu
Kitanda usichokilalia hujui kunguni wake!Bora Anglicana
Naunga mkono hoja ila siku hizi usipotoa hizi za mabahasha unatishiwa kunyimwa huduma za kikanisa ukizihitajiUzuri wake ni kuwa usipotoa si kosa la jinai.
Hizo huduma za kiroho ni ngumu tatizo sisi tunaenda kanisani na mitizamo ya kibinadamu/kipagani. Huyu Mungu tunayemtafute/tuitafute kweli mioyoni mwetu na tuijue. Huduma za kiroho ni gharama hakuna cha bure isipokuwa kusali tu unapokuwa wewe mwenyewe.Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??
Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia
Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.
Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.
Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.
#MaendeleoHayanaChama
...Ni Mpigaji TU kama Kondakta wa Daladala anavyosema hakuna Nauli Bali ni Mchango wa Mafuta TU! Yote ni Upigaji TU!Yule moigaji TU,
Anasema Hakuna sadaka, ila Kuna michango[emoji4]
Alizisoma nyakati akabaini taabu na kero za machangizoHahah, mzee baba siku hizi nasikia kuna kanisa linaitwa sijui Free Church la yule jamaa wa Ze Comedy, ukitaka kusali unaibuka tu hakuna sadaka za mafungu mafungu...
[emoji851][emoji851][emoji851][emoji851]Alie design hiyo business model ya church business ni genius ndio maana alihakikisha kuna njia za kukubana ili usiache kutoa hela maisha yako yote.
Kwanza kabisa wanaanzia mbali kwa kukuingiza kwenye system tangu ukiwa mtoto mchanga kwa ubatizo. Pili unaaminishwa kwamba bila kubatizwa kanisani na kupewa sakramenti wewe si mkristo. Hiyo yote unajengwa kisaikolojia ili uje upigwe vizuri. Baadae unaaminishwa kwamba ili uwe mkristo lazima utoe sadaka na michango yote ili "kueneza injili" na kusaidia jamii wakati kiuhalisia hamna kitu kama hicho. Mwisho unaambiwa usipotoa michango hautazikwa na kanisa na unatishiwa usipozikwa na kanisa unaenda motoni..!!! Yaani system ipo self contained mwanangu kila kitu ni mumo kwa mumo..!
Yaani mtu unafika mahali unajua kabisa hapa napigwa, ila huna pa kutokea dadeki..!
Uzuri padri hashiko septu wala jembe wala habebi jeneza na mfu hayatambui yanayojiri. Sasa sijui hofu i wapi?Usipotoa ni Bora hata kanisani usiende kwasababu huduma za kanisa hutapewa.
Hata kuzikwa Padre anaweza asije
Padre hashiki Jembe lakini ana uwezo wa kuwaambia watu wasishike wakakubali.Uzuri padri hashiko septu wala jembe wala habebi jeneza na mfu hayatambui yanayojiri. Sasa sijui hofu i wapi?
Okonkwo atabaki kuwa shujaa wangu japo ni fixious myth!