Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
This is very sad. Michango imekua Mingi sana makanisani na ukiwa mtoaji ndio unaonekana mkristo kamili.
 
Wakati unatusifia Waislamu, sisi huku wenyewe tunatamani tungekuwa na moyo wa kutoa sadaka kama wenu.

Sisi ni changamoto watu wazito kutoa sadaka, madrasa na misikiti mingi inahitaji ukarabati na shule pia. Ila watu wetu wazito mno wa kutoa sadaka. Sadaka mpaka zitokee kwa waarabu ndio madrasa zijengwe
Daaah we jamaaa wewe..umegonga mfupa..lkn sasa huku watu wana moyo wa kutoa...sasa huo moyo wanaubadili maana hari imekuwa tete mnooo. Sasa unatoa sadaka 7 kwa day moja hapo uko na mke nae 7...vijana wa sunday school unao wa4 nao sadaka...walau uwe na 100,000k ya sadaka siku hiyo.
 
Kuna ile ya kuwataka waumini waliofiwa na wapendwa wao eti watoe sadaka kubwa kubwa kadri wawezavyo kama kikokotoo cha kuwawezesha hao wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki kupata ahueni ya maisha huko kaburini. Yaani mimi hii haijawahi kuniingia akilini kabisa.
Du! huu sasa ndo WIZI... 🤣 🤣
 
Opera Snapshot_2022-04-20_120056_www.jamiiforums.com.png
 
Hii nimeipenda maana rambirambi zinaweza kuokoa jahazi. Ni uchuro kwa ndugu waliobaki kuona ndugu yao hakuzikwa na Padre!
Mimi nikifa wakaamua kutonizika ni wao. Roho yangu itakua mahali pengine na harufu itawatesa wao. Siwezi kujinyenyekeza ili wanizike as if wao ndio final say huko peponi
 
Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??

Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia

Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.

Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.

Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.

#MaendeleoHayanaChama
Mtoa mada hajasema hana hela ya kutoa au tusitoe sadaka. Hoja ni kuwa Sadaka na Michngo sasa hivi imekuwa mingi mno mpaka inatuchanganya waumini. Kama sisi sasa hv ukifika tu kanisani inabiidi ukachukua bahasha ya zaka..maanake sasa Zaka inalipwa kila jumapili badala ya mwisho wa mwaka au mara moja kwa mwaka, hii ni tofauti na sadaka unayotoa kwenye kikapu. Ukianza hesabu mlolongo wa michango mpaka unajiuliza..Hv mbona huku kazini tunavyolipwa mishahara huwa atuambiwi hii ni ya umeme, hii ni ya chakula, hii ni ya ada, hii ni usafiri, hii ni michango ya harusi? unalipwa mshahara then utachambua mwenyewe kipi ni muhimu katika mahitaji yako..Vivyo hivyo nafikiri Catholics wangefanya hivyo tutoe Sadaka na labda mchango wa pili (ujenzi wa kanisa au kusaidia maskini) wao wakikusanya ndio wakagawe kama hii ni ya tengeneza jimbo, hii ya kupeleka Bethsaida etc. Kingine miradi ya Catholics haisadii au kuwanufaisha walioijenga hao wakatoliki wenyewe. Shule wamejenga kwa michango na sadaka zetu lakini nenda kaulize ada zao? hazina tofauti na za private..basi hata sisi tuliochangia ujenzi wa shule hizo au hosptali tupewe kipaumbele au commission fulani ya unafuu kupata huduma hizo..Nenda Agha Khan hospital uone mhindi anavyopewa kipaumbele akifika pata matibabu kulinganisha na wewe mswahili! Kunahitajika mabadiliko kidogo ndani kanisa kuendana na hali ya maisha ya sasa!
 
Toa ndugu toa ndugu..ulichonacho..halafu unataka usitoe hilo kanisa litapelekaje injili..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje wahudumu..unataka usitoe hilo kanisa litalipaje bills tofauti kama umeme na maji...unataka usitoe hilo kanisa litafanyeje logistics mbali mbali...unataka usitoe maintaince na repairs ya vifaa na miundombinu mbalimbali utatoa wewe.??

Acha kulalamika sana kama huna hela kaa kutulia

Uzuri hujalazimishwa..ila mkristo wa kweli hawezi kuona kama ni wizi mana hayo ndio mahitaji muhimu ya kuendesha taasisi.

Kingine kutoa ni upendo..kiwango itachojaliwa kutoa kinatosha sana.

Kama unaona hufiti nenda huko ambako hawatoi sadaka..hakuna aliyekushikiria unabaki kanisani.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote.

#MaendeleoHayanaChama
Ila wewe ni mbugila.maendeleo hayana vyama,kauli ya kilofa sana hii.na ilitolewa na mnafiki mwandamizi
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Umeandika kwa muhemuko sana ... Tatizo ni lipi? Kama ni sadaka .. Wewe hujaenda kanisani muda, unaenda kwa kubeep.. Sasa kuna shida gani kama watu wenyewe wanapenda kutoa sadaka? Ingekuwa shida kama unalazimishwa na kama huna labda unafukuzwa au kutolewa nje .

Kama una imani ya kweli hiyo haiwezi kukuzia kwenda kanisani au kuweka jumuisho kuna shida kwenye ukatoliki..Basi ungetafuta kanisa ambalo ni kamilifu uende ukasali huko..Huwezi kupata kanisa kamilifu, ndio maana Kristo ndiye kanisa halisi na yupo kwa watu wanaomtafuta.
Umedai waislam wako sahihi , mbona umefanya kwa ujumla? unawaongelea waislam wapi? Wapo madhehebu tofauti tofauti .. Shia, Suni na ipo misikiti tofauti tofauti na wana taratibu za kuomba au kukusanya sadaka zao.. Je ulitembelea na waislam?

Kama wako vizuri, mbona hujaenda kuungana nao katika imani yao?
Imani ni yako, kanisa ni jukwaa la kuonyesha au kuungana na wengi kufanya kazi ya mwili wa Kristo.. Hata siku moja , hutaweza kupata kanisa la namna hiyo au mtumishi mkamilifu... Ukamilifu upo kwa Kristo peke yake ..... Amani ya Bwana itawale.
 
Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
Hili swala huwa linanifikirisha sana....
 
Unaendaje kanisani na buku 5 mkuu? Wakati baa mnaingia na laki beba kuanzia hamsini ukiona unahoji mambo ya sadaka jua umekufa kiroho toa ulichonacho huna tulia Mungu anakuona matumiz ya sadaka hayatuhusu imarisha uhusiano wako na Mungu kwa kutoa
Mchango ya malofa Huwa kama ulivyoandika .
 
Acha moyo mbaya toa Kama ipo ,mbona kwenye. Baa unatimia hata laki kwa Mambo yasiyo na maana,hata Kama Kuna ujenzi kanisani kwenu haiwezi kuwepo Kila siku,ukitoa Mungu ananibariki,ibada Ni pamoja na kutoa
 
Jiulize hyo elfu kumi yako unatimia shs ngapi,mbona watu wanatoa zaidi y a elfu kumi kwenye ibada moja,?Mtu asiyejua uwepo wa Mungu ndiyo alalamike hiyo
 
Cha msìngi beba mia 7 yani shilingi mia ziwe 7,kuanzia sadaka ya kwanza adi ya 7 unanyanyuka tu na washirìka wanakuona umetoa!
Wala hutaumia,kikubwa Mungu anaona moyo wako!
 
kwani ukifa wasipo kuzika hautaoza??kwani wasio enda kanisani hawafi na kuzikwa??
 
Back
Top Bottom