Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Ukifa hawakuziki. Hapo ndipo wametushika pabaya
Hizo ndizo bhangi za madhehebu tunazovutishwa waumini.

Kwani wasipokuzika wao, jamii imekwenda wapi?

Kitendo cha kusitiriwa kaburini hakichukui hata zaidi ya nusu saa na baada ya hapo hakuna alama inayobaki kaburini kwamba huyu marehemu kazikwa kwa mtindo gani.
 
Wakati unatusifia Waislamu, sisi huku wenyewe tunatamani tungekuwa na moyo wa kutoa sadaka kama wenu.

Sisi ni changamoto watu wazito kutoa sadaka, madrasa na misikiti mingi inahitaji ukarabati na shule pia. Ila watu wetu wazito mno wa kutoa sadaka. Sadaka mpaka zitokee kwa waarabu ndio madrasa zijengwe
Nadhani pia hii inatokana na kuwa hatujawekewa vikwazo au kulazimishwa kutoa ndio mana tunakuwa wagumu.
Kiukweli upande wetu kwenye suala la kutoa ni changamoto.
Hata hawa wanaolalamika kama wangekuwa hawajabanwa wasingekuwa wanatoa ila ni kwasababu tu wamewekewa utaratibu wanajikuta ni lazima watoe
 
Kuna ile ya kuwataka waumini waliofiwa na wapendwa wao eti watoe sadaka kubwa kubwa kadri wawezavyo kama kikokotoo cha kuwawezesha hao wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki kupata ahueni ya maisha huko kaburini. Yaani mimi hii haijawahi kuniingia akilini kabisa.
Hii kali
Toeni bwana muwafanyie wepesi wapendwa wenu huko kaburinj
 
Mkuu unaweza nisaidia sadaka hizi tisa zilikua zipi na mlitoa kwa wakati gani?. Ili ni muhimu usiache kujibu.

Mimi kwangu ilishabaki na sali sala binafsi nyumba. Ikiwa tofauti mara moja moja naenda kanisani nasali na kuondoka. Ukweli michango imekua mingi imefika hatua hadi kanisa wanajisajili kulipa kwa mpesa au tigo pesa. Huwa siaangaiki ata na mchango mmoja. Utasikia kanisa halijaisha, shule ya chekechekea, nyumba ya sisters.

Swala la zaka sijawai toa na sitarajii kama ntakuja kutoa. Ile asilimia 10 ya kipato cha mtu inatofauti gani kodi wanayotoza TRA katika kila faida anayopata mtu. Ni onyonyaji.

Nafikiri hofu ya wengi huwa wana hofu padri hasipokuja siku ya maziko yako. Kwangu ili si hofu maana ntakua mfu sitojua walinitupa au walinivisha nguo gani. Nani alikuja msibani nani hakuja

Hapa ndio naona dini wakati mwingine ni mchongo. Haiwezekani wao wakitaka gari aua nyumba tuwachangie. Ila sisi wauumini tukitaja gari au nyumba tupige magoti tuombe sana.
Well said mkuu.
 
Ningependa kujua ni jimbo gani.

Nimekaa jimbo la Morogoro,jimbo la moshi, jimbo la Arusha na jimbo la dar es laam sijawahi kusikia huo mchango wa ada ya kua kikatoliki.
Ingawa kila jimbo lina utaratibu wake.
 
Ukishaingia mfumo wa jumuia lazima utowe pesa ya kuwa mkatoliki kila mwezi.

Pili harambee za kipuuzi na sadaka nyingi kwenye ibada inaondoa system ya kikatoliki ambayo tulizoea ibada ya misa ya jumapili ni lisaa limoja na nusu tu na ikizidi kwa special case ni masaa mawili tu, sasa kwa huu upumbavu ulioanza ibada inakwenda mpaka masaa matatu, misa ya kwanza mnaingia saa 12 asubuhi mnatoka saa mbili na kitu.
Maana ake iyo tuiite Ni tozo ya ukatoriki[emoji28]
 
Makanisa sasaivi yamekumbwa na pepo la fedha zamani kidogo katoliki ilikua nzur sana lakini walipoingia ma padre weusi ndipo dhahama ilipoingia kanisani,,siku za mwisho hizi shetani anajiinua kupita kiasi lengo lake kuu ni kuharibu kabisa amani ya kanisa,,sote tunafahamu madhara ya pesa katika dini hivo nae anapenyeza wajumbe wake kuharibu kanisa.usivunjwe moyo na michango we toa ulichobarikiwa asante.
 
Ukiona huko Katoliki na Lutheran sadaka zinakutisha na kukuchosha basi jaribu makanisa ya Pentekoste ndio utakiona cha mtema kuni.

Huko Pentekoste utatakiwa kutoa
1. 10% ya kipato chako chochote (kama una mshahara wa 1m kwa mwezi, basi kila mwezi laki moja lazima pastor aikunje mfukoni, na pastor atataka kuona mpaka salary slip)

2. Kuna sadaka za shukrani kila unapofanikiwa jambo lolote (na hii inapaswa kuwa sadaka nono fulani)

3. Kuna sadaka ya kusindikizia maombi yako kila unaposaka kuombewa mambo yako. (Hapo utapigwa mikwara kibao)

4. Kuna sadaka ya kuchangia shughuli mbali za kanisa (kuanzia ujenzi, vyombo vya muziki, uinjilisti, suti ya mchungaji, gauni la mama mchungaji nk)
 
Ni vigumu kwa vijana wa kizungu kuwaswaga kama tunavyofanyiwa waumini wa Tanzania.

Uzuri wa wazungu wana reasoning, ndio maana hata walipoleta hii dini walikuwa wanajenga wao makanisa na hospitali target yao ilipotia wakavuta end break.

Sasa ajitokeze mkatoliki hapa leo anieleze miradi mikubwa ya kanisa chuo kikuu cha SAUT mashule, mahospitali mahostel yana faida gani kwetu kama waumini tunaendelea kukamuliwa hivi?

Maana hata Martin Luther alipojitenga na Vaticano na yeye kuna mambo ya kipuuzi yalimkwaza.
Point[emoji106]
Wakikujibu nitag
 
Mavuno nadaiwa laki mbili mwisho mwezi wa sita.....
Nadaiwa zaka sijarudisha bahasha hii lazima nitoe.......
Leo jpili lazima nizame kanisani na sadaka 3
Nadaiwa laki mbili mchango wa gari la Paroko...nili-pleadge......
nisipotekeleza haya nitaonekana sio mkristo
Ha ha ha.....
Yaan Usipolipa utaonekana si mkristo[emoji28]
 
Lakini kuna sinodi ya maaskofu inayoendelea hio ilitoa nafasi kwa waumini kutoa dukuduku lao, mawazo yao, maoni yao na vile wanavyoliona kanisa leo na kesho.

Kwa vile ndugu mleta mada umekiri sio mhudhiriaji wa kanisani na jumuiyani hio nafasi imekupita.


Hata hivyo mapinga vikali michango mikubwa na isio mikubwa ilio mingi ndani ya parokia zetu, haswa kukukiwa na ujenzi wa kanisa, hapo panakua ni chanzo cha mapato na fursa kwa baadhi ya wengi.
 
Kuna ile ya kuwataka waumini waliofiwa na wapendwa wao eti watoe sadaka kubwa kubwa kadri wawezavyo kama kikokotoo cha kuwawezesha hao wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki kupata ahueni ya maisha huko kaburini. Yaani mimi hii haijawahi kuniingia akilini kabisa.
Ha ha ha.....
Maana ake iyo sadaka kubwa ndo inwatuliza uko kaburini au?[emoji28]
 
Sisi parokia yetu imezaa parokia tatu, unaweza kuelewa machozi na damu tuliyopitia.

Tuna nyumba ya masista, tuna nyumba ya mapadri ya zamani, ikajengwa ghorofa likaja hilo ghorofa likaonekana dogo utadhani mapadre wetu ni matembo tukajenga ghorofa nyingine mpya kubwa.

Tumemnunulia paroko Prado, tuna dispensary tuna maternity tuna Ambulance tuna nursery school, kama hiyo haitoshi kuna nyumba nne jirani tumezinunuwa tumevunja ndio umeanza upuuzi eti tujenge nyumba ya mama bikira Maria.

Yani the way nilichojifunza hakuna kipindi mtaachwa mpumuwe ni kutwishana mizigo mwaka mzima.
[emoji3][emoji3][emoji3] nyumba ya kufikia bikira maria! Huo wizi wa mchana kweupe kabisa.
Alafu ukute paroko na prado lake anakuja kung'oa wake zenu na mabinti zenu.
 
Back
Top Bottom