Hapo kwenye dilution sasa ndo unatoka njiani.
Ni hivi.
Kila mtoto anapoingia duniani, mtoto ambaye ni pure human hajachanganya uzao na mapepo, hatma ya maisha yake Huwa Inajulikana, NDOA pia Huwa Inajulikana. Tena NDOA yenyewe ni ya mke mmoja na mme mmoja.
Wapo watakaohoji iweje wanawake wawe wengi Duniani kuliko wanaume, kwamba hao waliozidi wataolewa na nani?
Jibu ni Rahisi. Uzao wa WANADAMU wasiochanganya uzao na mapepo ni Wachache kuliko uzao wa mapepo ktk mwili wa mwanadamu.
Na wanawake nusu mtu nusu Pepo ndo wengi kuliko wanaume nusu mtu nusu Pepo.
Waliookoka Wana solution ya kudumu.
Waliookoka tuna uwezo wa kujua nani Hasa ni ubavu wa mtu mume au mtu mke kupitia maombi.
Binti mmoja aliyeokoka alikuwa katika maombi, alimuuliza Mungu amuonyeshe Mume wake aliyeumbiwa Yuko wapi na alijibiwa.
Jibu lilikuja katika maono, aliambiwa mumuwe yupo Mkoa mwingine tena watakuja kukutanishwa baada ya miaka miwili ijayo.
Binti yule baada ya hapo hakujisumbua kutafuta au kusikia offer za wachumba wengine Hadi mumewe alipoletwa baada ya muda huo kufika na wakaoana sawa na Neno la BWANA.
Binti mwingine alichumbiwa na mchumba tajiri, bt alipoingia ktk maombi, Mungu alimwambia huyo Si ubavu wako, na Hana maisha marefu sababu atafariki baada ya miezi kadhaa sababu ndiyo hatma yake, so what if angekubali kuolewa, angekuwa mjane baada ya muda mfupi.
Ushauri.
Kama wewe ni Mwana wa Mungu,Usitende kuuliza Kwa mganga akusomee nyota,
Waislamu wanaAMINI katika Mungu lakini wanafail Kwa kuamini Waganga pia.
Mganga ni agent wa Ufalme wa chini, kama mtu ni uzao wa kipepo,ruksa kwenda Kwa mganga kuuliza mkewe kinyota kama wanaendana.
Bt kama ni uzao Kutoka juu, Mungu ana majibu yote.
Nawasihi Binti za Mungu, msikate tamaa mnapoona ubavu wenu hatokei Kwa wakati, yaezakuwa mumeo ameenda kuoa Pepo bila kujua, hivyo UKIOMBA Mungu, Mungu ataingilia kati na kuvunja NDOA ya kipepo Ili mtu sahihi arudi kufunga NDOA ilokusudiwa tangu Kuzaliwa.
Ameen