Kuna pepo likiingia kwenye familia hutafuna vizazi vingi

Kuna pepo likiingia kwenye familia hutafuna vizazi vingi

Ndiyomaana huwa namwomba sana Mungu kuniepusha na majanga ya kuendekeza vimada kila kona ya nchi maana mengine ndiyo hayo mapepo yenyewe
Dunia ina mambo mengi mazito mkuu, wakati mwingine ni kama mkosi au nuksi yaani unaingia tu kwa mara ya kwanza unakutana na balaa. Lakini nilichojifunza, kabla ya kufanya jambo lolote baya huwa Kuna sauti ya ndani inaonya wazi wazi ila kwa ukaidi na tamaa zetu tunajikuta tumeshaingia kwenye mtego
 
Hii kitu unayoisema nimepata uzoefu nayo kwa sehemu. Miaka ya nyuma huko nilipata girlfriend mzuri, anaakili ya kimaisha na ya ziada. Ila hiyo ya ziada ni ya gizani. Pia nilikuja kugundua ni mtu mwenye muunganiko mkubwa sana na mapepo/majini. Sababu aliwahi kuniambia mwenyewe baadhi ya matukio ya ndoto na linalokuja kutukia physically. Tulikuwa tukivutana sana kama wote ni wanaume na Kuna wakati alikuwa na utisho. Alikuwa ni mwanamke anayetaka kuniinamisha kitu ambacho sijawahi kuota katika maisha ya mume na mke. Nikaachana naye maisha yakaendelea, lakini Kuna matukio kadhaa yalikuwa yakinitokea kwenye ndoto hata baada ya muda wa miaka zaidi ya mitano tuliyoachana! Tangu hapo naheshimu sana mambo ya uhusiano wa mwanamke na mwanaume na hata mwingiliano wa kawaida tu wa wanaume wenzangu kama marafiki. Bila shaka naeleweka vizuri na watu wenye upeo wa ziada.
Ni makosa makubwa pia kuamini kuwa ulipoachana nae physically ndo umemaliza.

Fuatilia vizuri ndoto unazoota, Bado Huwa anakujia na mnatenda tendo,

Kuna vinasaba amekuachia vitakavyoenda kuathiri Hadi uzao unakuja BAADAYE.

Ongeza bidii kuhakikisha umekata hizo connection zote zote za KUZIMU, maana watu hao ni vinganganizi sana. Maombi serious ukifanya utafanikiwa.

Ikishindwa, watafute watumishi wa Mungu wa Kweli wakusaidie, Usitende Kwa manabii wa uongo, utapotea zaidi.
 
[emoji1545][emoji817] umeongea kiroho zaidi.. I wish haya masomo ya utambuzi wa kiroho yangekuwa yanafundishwa kwenye taasisi zetu za elimu
Kabisa mkuu,sijui kwa nini elimu ya utambuzi imefichwa mnoo kias kwamba access yake ni ngumu mnoo.

Nasikitika mnoo,imefikia hatua mtu ananzishiwa dawa za schizophrenia kwa kukosa tu mtu wa kunotice kwamba vile anavyo feel ni source of awakening to the highest Consciousness.

Maana dalili za spiritual awakening zinafanana kabisa na yule anaye anza kuumwa kichaa.
 
Dunia ina mambo mengi mazito mkuu, wakati mwingine ni kama mkosi au nuksi yaani unaingia tu kwa mara ya kwanza unakutana na balaa. Lakini nilichojifunza, kabla ya kufanya jambo lolote baya huwa Kuna sauti ya ndani inaonya wazi wazi ila kwa ukaidi na tamaa zetu tunajikuta tumeshaingia kwenye mtego
Sauti hiyo inaitwa WILL au dhamira. Mungu ameiweka ndani ya Kila mtu.

Ukikutana na mtu ukajikuta unakosa Amani naye na hujui sababu, muepuke.
 
Ni makosa makubwa pia kuamini kuwa ulipoachana nae physically ndo umemaliza.

Fuatilia vizuri ndoto unazoota, Bado Huwa anakujia na mnatenda tendo,

Kuna vinasaba amekuachia vitakavyienda kuathiri Hadi uzao unakujia BAADAYE.

Ongeza bidii kuhakikisha umekata hizo connection zote zote za KUZIMU, maana watu hao ni vinganganizi sana. Maombi serious ukifanya utafanikiwa.

Ikishindwa, watafute watumishi wa Mungu wa Kweli wakusaidie, Usitende Kwa manabii wa uongo, utapotea zaidi.
Huhitaji kwenda kwa wachungaji mkuu,kuna procedure za kurelease karmic energy ambazo umezibeba kwa kufanya Yoga au Meditation ingawa ni very painful process.

Jifunze maana ya yoga na meditation.
Mshana Jr
 
Dunia ina mambo mengi mazito mkuu, wakati mwingine ni kama mkosi au nuksi yaani unaingia tu kwa mara ya kwanza unakutana na balaa. Lakini nilichojifunza, kabla ya kufanya jambo lolote baya huwa Kuna sauti ya ndani inaonya wazi wazi ila kwa ukaidi na tamaa zetu tunajikuta tumeshaingia kwenye mtego
Hiyo sauti ya ndani ndio sauti ya Mungu na ndio jicho la kiroho huona zaidi ya kuona. Ila ujuaji wa kibinadamu ndio hutupofusha na kututia nta masikioni
 
Ni makosa makubwa pia kuamini kuwa ulipoachana nae physically ndo umemaliza.

Fuatilia vizuri ndoto unazoota, Bado Huwa anakujia na mnatenda tendo,

Kuna vinasaba amekuachia vitakavyienda kuathiri Hadi uzao unakujia BAADAYE.

Ongeza bidii kuhakikisha umekata hizo connection zote zote za KUZIMU, maana watu hao ni vinganganizi sana. Maombi serious ukifanya utafanikiwa.

Ikishindwa, watafute watumishi wa Mungu wa Kweli wakusaidie, Usitende Kwa manabii wa uongo, utapotea zaidi.
Kuna picha tulizowahi kupiga pamoja, nilipooa niliendelea kuzihifadhi. Mke wangu akaniambia siyo vizuri kuzihifadhi hizi picha huwa zinaambatana na roho. Basi kwa Imani yangu nikaomba na kuvunja mahusiano yangu na wanawake niliokuwa nao hapo kabla, Kisha nikazichana na kuzitupa hizo picha zote. Mambo ya ajabu ni kwamba hata mke wangu alikuwa akipata ndoto kadhaa kuhusu mwanamke huyu, huyu tu wala si hao wengine niliokuwa nao kabla ya mwanamke huyu na kbla ya kuoa huyu mke wangu. Ndoto za kukutana naye kimwli ni nyingi tu nilikuwa nikiota mpaka nilipochukua hatu ya kumwomba Mungu. Ndiyo maana nawaogopa wanawake na kukaa nao mbali sababu najua kwa sehemu matokeo ya baadaye. Haijalishi ni mzuri au ana mvuto kiasi gani, najua Kuna kilichopo cha ziada nyuma yake.
 
Kama ni hivo basi Yesu inabidi aje Tena. Maana yake pamoja na hadi kusurubiwa msalabani lakini bado shetani anatamba tu.

Sipendi watu wanaohusisha changamoto na Imani. Nyumbani wananiambiaga Nina Pepo la ubishi, na Mimi nawaambia Kwa hiyo nyinyi mna malaika wa kukubalikubali Kila kitu bila logic
 
Mfanya biashara ya ngono anaanzaje kuzaa kirahisi namna hii asimjue mhusika? Labda kama mhusika alimkimbia
Kama ananunuliwa na wateja kadhaa kila siku atajuaje?
Cheki mfano hapa..
 
Kuna picha tulizowahi kupiga pamoja, nilipooa niliendelea kuzihifadhi. Mke wangu akaniambia siyo vizuri kuzihifadhi hizi picha huwa zinaambatana na roho. Basi kwa Imani yangu nikaomba na kuvunja mahusiano yangu na wanawake niliokuwa nao hapo kabla, Kisha nikazichana na kuzitupa hizo picha zote. Mambo ya ajabu ni kwamba hata mke wangu alikuwa akipata ndoto kadhaa kuhusu mwanamke huyu, huyu tu wala si hao wengine niliokuwa nao kabla ya mwanamke huyu na kbla ya kuoa huyu mke wangu. Ndoto za kukutana naye kimwli ni nyingi tu nilikuwa nikiota mpaka nilipochukua hatu ya kumwomba Mungu. Ndiyo maana nawaogopa wanawake na kukaa nao mbali sababu najua kwa sehemu matokeo ya baadaye. Haijalishi ni mzuri au ana mvuto kiasi gani, najua Kuna kilichopo cha ziada nyuma yake.
Ungejielimisha jinsi gani ndoto inatokea kisayansi, ungeanza mwenyewe kujiona ulikuwa mjinga
 
Ni muhimu sana kufanya vetting ya kutosha kwenye kutafuta mwenza mwenye background yenye afya kiroho kwenye familia atokayo ili kuweza ku dissolve hiyo hali.. Lakini hii ni njia mojawapo tu
Hujawahi kuona kwenye familia yenye shida tangu kwa mababu, baba anachepuka na kuzaa mtoto anayekuwa tofauti na wengine na kuja kuwa mkombozi wa familia ama akawa kimeo

Bro mshana umezungumza kitu cha maana sana. Family background is everything, inaweza kupa picha halisi mtu unae ishi nae mbeleni atakuwaje
 
Hapo kwenye dilution sasa ndo unatoka njiani.

Ni hivi.

Kila mtoto anapoingia duniani, mtoto ambaye ni pure human hajachanganya uzao na mapepo, hatma ya maisha yake Huwa Inajulikana, NDOA pia Huwa Inajulikana. Tena NDOA yenyewe ni ya mke mmoja na mme mmoja.

Wapo watakaohoji iweje wanawake wawe wengi Duniani kuliko wanaume, kwamba hao waliozidi wataolewa na nani?

Jibu ni Rahisi. Uzao wa WANADAMU wasiochanganya uzao na mapepo ni Wachache kuliko uzao wa mapepo ktk mwili wa mwanadamu.

Na wanawake nusu mtu nusu Pepo ndo wengi kuliko wanaume nusu mtu nusu Pepo.

Waliookoka Wana solution ya kudumu.

Waliookoka tuna uwezo wa kujua nani Hasa ni ubavu wa mtu mume au mtu mke kupitia maombi.

Binti mmoja aliyeokoka alikuwa katika maombi, alimuuliza Mungu amuonyeshe Mume wake aliyeumbiwa Yuko wapi na alijibiwa.

Jibu lilikuja katika maono, aliambiwa mumuwe yupo Mkoa mwingine tena watakuja kukutanishwa baada ya miaka miwili ijayo.

Binti yule baada ya hapo hakujisumbua kutafuta au kusikia offer za wachumba wengine Hadi mumewe alipoletwa baada ya muda huo kufika na wakaoana sawa na Neno la BWANA.

Binti mwingine alichumbiwa na mchumba tajiri, bt alipoingia ktk maombi, Mungu alimwambia huyo Si ubavu wako, na Hana maisha marefu sababu atafariki baada ya miezi kadhaa sababu ndiyo hatma yake, so what if angekubali kuolewa, angekuwa mjane baada ya muda mfupi.

Ushauri.

Kama wewe ni Mwana wa Mungu,Usitende kuuliza Kwa mganga akusomee nyota,

Waislamu wanaAMINI katika Mungu lakini wanafail Kwa kuamini Waganga pia.

Mganga ni agent wa Ufalme wa chini, kama mtu ni uzao wa kipepo,ruksa kwenda Kwa mganga kuuliza mkewe kinyota kama wanaendana.

Bt kama ni uzao Kutoka juu, Mungu ana majibu yote.

Nawasihi Binti za Mungu, msikate tamaa mnapoona ubavu wenu hatokei Kwa wakati, yaezakuwa mumeo ameenda kuoa Pepo bila kujua, hivyo UKIOMBA Mungu, Mungu ataingilia kati na kuvunja NDOA ya kipepo Ili mtu sahihi arudi kufunga NDOA ilokusudiwa tangu Kuzaliwa.

Ameen
Uko nondo sana, hongera sana kwa kutupatia madini haya Chifu.
 
Kama ni hivo basi Yesu inabidi aje Tena. Maana yake pamoja na hadi kusurubiwa msalabani lakini bado shetani anatamba tu.

Sipendi watu wanaohusisha changamoto na Imani. Nyumbani wananiambiaga Nina Pepo la ubishi, na Mimi nawaambia Kwa hiyo nyinyi mna malaika wa kukubalikubali Kila kitu bila logic
Kila jambo ni vema kulipima, hasa mambo nyeti yanayohusu Imani. Changamoto unayoweza kuipata katika kutafuta usahihi ni namna unavyotenga utulivu wa kuisikia sauti ya kweli (sauti ya ndani) kwa sababu wakati mwingine unaweza kujikuta unavutana na mtu aliyeendelea sana kiakili na kiufahamu kuliko wewe, hivyo akawa na hoja zinazoonekana zina nguvu zaidi kuliko hoja zako, ingawaje hoja zake haziwezi kupingana na ukweli unaosikia ndani yako
 
Lile nalo ni pepo baya sana hasa kama una familia
Imagine mwanamke unayemnunua ana joto na vinasaba vya wanaume wangapi aliolala nao? Kwahiyo unaingizwa kwenye mnyororo bila kujua
Mbaya zaidi sio wanaojiuza wote ni kwa ajili ya umasikini na kipato wengine ni ma agent wapo kuvuna manii kwa matumizi ya kishirikina

Kudumu na huyo mwenye hizo changamoto pia ni tatizo kwakuwa kuna mambo utafanya hayaendi na yakienda ni kwa msuli mkubwa sana

Unapata kipato kizuri lakini huna cha maana ulichonacho
Una kazi nzuri lakini hali yako na familia yako havilingani na hadhi ya kazi yako
Ni rahisi kutengeneza michongo ya pesa lakini pesa ukiitia tu mkononi kuna kitu cha dharura kinahitaji pesa kinatokea na kinakuhusu asilimia 100
Una pesa, una maisha mazuri lakini ndani ya familia kila siku ni changamoto haziishi nknk
Ni kweli Ke wa kununua wanaweza kumtupia Mtu pepo la ugumba hata kama alitumia kondomu?
 
Lile nalo ni pepo baya sana hasa kama una familia
Imagine mwanamke unayemnunua ana joto na vinasaba vya wanaume wangapi aliolala nao? Kwahiyo unaingizwa kwenye mnyororo bila kujua
Mbaya zaidi sio wanaojiuza wote ni kwa ajili ya umasikini na kipato wengine ni ma agent wapo kuvuna manii kwa matumizi ya kishirikina

Kudumu na huyo mwenye hizo changamoto pia ni tatizo kwakuwa kuna mambo utafanya hayaendi na yakienda ni kwa msuli mkubwa sana

Unapata kipato kizuri lakini huna cha maana ulichonacho
Una kazi nzuri lakini hali yako na familia yako havilingani na hadhi ya kazi yako
Ni rahisi kutengeneza michongo ya pesa lakini pesa ukiitia tu mkononi kuna kitu cha dharura kinahitaji pesa kinatokea na kinakuhusu asilimia 100
Una pesa, una maisha mazuri lakini ndani ya familia kila siku ni changamoto haziishi nknk
Watu wengi sana wanapitia haya wasijue sababu ni nini
 
Katika hiyo familia mmoja anaweza kuwa mshirikina na kuwaletea Pepo la kuwamaliza ili yeye mambo yake yaende. Kuna mtu anaishi mjini na starehe zake ila wazazi na ndungu zake wanateseka kijijini. Akienda chap, anawapa wazaze wake pesa kidogo kwa kutumia mkono wa kushoto. Hilo ni pepo!!
 
Back
Top Bottom